Waliyoteta Odinga, Upinzani yafichuka

Kithuku, Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya hayati Mwl. Nyerere kuwa upinzani wa kweli kwa CCM utatoka ndani ya CCM yenyewe. Kwa hakika level ya upinzani Tz kwa sasa ni sawa sawa na hakuna wengi wa wanaojiita wapinzani ni watu waliozidiwa na tamaa au njaa kiasi kwamba wanakuwa wepesi kurubuniwa na CCM. Tumeshuhudia viongozi kadhaa waliokuwa katika vyama vya upinzani wakihama vyama vyao na kurudi CCM kwani wengi wao waliotokea huko. Ipo mifano kama akina Masumbuko Lamwai, Dr. Kaborouna wengi wenye nyadhifa na wanachama wa kawaida.

Pia suala la vyama vya upinzani kuungana bado ni kitendawili kwani hao viongozi wana ubinafsi na tamaa za kutaka kuingia ikulu kitu ambacho hata Nyerere alikishangaa sana. Na aliwahi kusema kuwa hata kama wananchi wameamua kusukuma gari la kiongozi wa upinzani kwa nderemo na vigerere wawaache tu kwani alijua kuwa hawatafika mbali na sasa tunashuhudia upinzani ukielelea kufa kifo cha asilia. Kwa hiyo hata huyo Odinga anachowashauri hao ndugu ni wastage of time and energy tu lakini nadiriki kusema upinzani Tanzani "MUFIRISI".....
 
Tatizo ni ruzuku, na hiyo ndio chambo walioiweka CCM. Wapinzani njaa yao ndio inawafarakanisha kila uchao.

Kama wanashindwa kuelewana kuweka mgombea mmoja Tarime au kwenye viti vya madiwani hawataweza kuweka mgombea mmoja wa Urais katu!
 
Kama hii ni kweli basi kazi ipo. Nilishaweka hapa habari kuhusu Mtikila kuwashambulia CHADEMA. Na nikauliza je Mtikila kapewa bulungutu na RA ili awashambulie CHADEMA? Maana miaka yote target ya mashambulizi ya Mtikila ilikuwa ni CCM ghafla tu imebadilika na kuwa CHADEMA. Na ukitilia maanani RA alianika hadharani kwamba Mtikila alienda kuomba michuzi kwa RA, basi kuna uwezekano mkubwa kwamba Mtikila kishatiliwa kitu kikubwa na RA na CCM ili awashambulie CHADEMA. Kweli siasa ni mchezo mchafu sana.

Unaweza kupata picha halisi kuwa RA ana mkono wake kwa Mtikila. Katika watu Mtikila anawashutumu kwa mauaji ya Wangwe yumo Reginald Mengi. kama unakumbuka pale Kilimanjaro Hotel, RA alitupa 'vijembe' vingi tu Mengi ingawa hakumtaja moja kwa moja. Hivi ugomvi wa RA na Mengi unahusu nini?
 
Kama hii ni kweli basi kazi ipo. Nilishaweka hapa habari kuhusu Mtikila kuwashambulia CHADEMA. Na nikauliza je Mtikila kapewa bulungutu na RA ili awashambulie CHADEMA? Maana miaka yote target ya mashambulizi ya Mtikila ilikuwa ni CCM ghafla tu imebadilika na kuwa CHADEMA. Na ukitilia maanani RA alianika hadharani kwamba Mtikila alienda kuomba michuzi kwa RA, basi kuna uwezekano mkubwa kwamba Mtikila kishatiliwa kitu kikubwa na RA na CCM ili awashambulie CHADEMA. Kweli siasa ni mchezo mchafu sana.

Heshima kwako mkuu Bubu,
Natanguliza shukrani zangu za dhati kwa kazi unazofanya hapa.Naomba kupingana na wewe kuhusu dhana ya siasa ni mchezo mchafu.Mimi binafsi naamini siasa ndio msingi imara wa kupitisha mawazo endelevu kwa faida ya jamii inayohusika.Ni siasa inayopanga kuwa huyu apate hiki na yule apate kile.
Tatizo linakuja pale watu wenye nia mbaya wanapovamia siasa.Na mara nyingi wahalifu hawa wanatumia udhaifu wa walipakodi kutoelewa dhana nzima ya sera na uongozi bora.Mwalimu Nyerere alihubiri sana dhana ya vitu vinne ili kufikia maendeleo endelevu.
Tatizo la siasa ni mchezo mchafu linachochewa na Transitional societies kama vile Afaghanistan kulikuwa na utawala wa Taliban ambao ulikuwa wa kikatili na jamii ile kwenye enzi za ujima,lakini bahati mbaya wale wananchi wakipewa nafasi ya kupiga kura wanaweza kuwachagua Taliban ili waepukane na bughudha za kulipuliwa na mabomu.
Ndio maana hapa hayatumiki mabomu,zinatumika fedha ambazo walipakodi wa Tanzania wameibiwa BOT kununua ushindi kwa kuwatumia mawakala wa siasa kama Mtikila.
Nakataa kabisa kuwa siasa ni mchezo mchafu.
 
Vyama vya upinzani vimekosa mwelekeo kwa sababu ya vipandikizi ndani ya vyama hivyo. Hakuna wapinzani wa kweli. Walopo labda ni wachache sana ambao wamekerwa na sera chafu za CCM na ndio wanapigana kiume. Wengine wote ni vibaraka tu. Mfano mmoja ni huyo Mtikila.

wengi wetu tunaopenda mabadiliko tuko nje. Huwezi kuwa nje ukaleta mabadiliko ya dhati katika nchi yako. Tunahitaji turning point sasa. Vinginevyo tutaishia kulalamika tu. Wasomi, wanamapinduzi wakweli tuingie katika siasa ili tuokoe nchi yetu.

Tunasema sana humu, lakini kazi hiyo tumemwamini nani atufanyie? Ni Mbowe, Ni Zito, ni mama Kilango?
 
Mazingira ya Kenya kuelekea uchaguzi mkuu 2002 yalikuwa hayana tofauti na ya sasa Tanzania kuelekea general election 2002
 
Sina hakika kama Raila hamjui RA... nadhani hata RA amekwama baada ya leo Mwanahalisi kuandika habari nzito kumhusu. Bahati mbaya Mwanahalisi halimo katika mtandao, lakini kwa wenye kuweza kutusaidia nyumbani wange scan na kuiweka humu.
wote ni kingmakers

naamini rostam kujivua gamba kuna faida tele, coz he feels bertrayed, na waliomsaliti sasa ndio mwanzo wa kuvuana nguo
 
Kwa mujibu wa katiba ya sasa ni vigumu mno vyama vya kisiasa kuungana. CCM hili walijua linaweza kutokea wakapiga ribiti lisije kutokea vyama kuungana. NIFAFANUE,iko namna hii:
Chama che usajili kamili kinaposimamisha wagombea katika nafasi ya ubunge na urais kinapata ruzuku kwa aslimia ya ushindi wake.

Na chama kitakacho simamisha mgombea kwa nafasi ya rais, na ikatokea mgombea huyo akapa kura kwa zaidi ya asilimia 5 ya kura zote za urais, chama chake kitapata ruzuku kwa ushindi huo.

TATIZO: fedha za ruzuku ambazo chama hupata haziruhusiwi kugawiwa chama kingine au kutumika vinginevyo zaidi ya kukiendeleza chama husika.
Kwa mantiki hiyo, vyama vya upinzani havina vyanzo vya mapato. Vinategemea ruzuku za ushindi wa viti vya ubunge na ruzuku kupitia kura za urais. Viongozi wetu wanajali vyama vyao zaidi kuanzia ccm,maslahi ya chama yako mbele kuliko ya wananchi. Angalia bunge utayaona hayo.
 
Kithuku, Hapa ndipo ninapokumbuka maneno ya hayati Mwl. Nyerere kuwa upinzani wa kweli kwa CCM utatoka ndani ya CCM yenyewe. Kwa hakika level ya upinzani Tz kwa sasa ni sawa sawa na hakuna wengi wa wanaojiita wapinzani ni watu waliozidiwa na tamaa au njaa kiasi kwamba wanakuwa wepesi kurubuniwa na CCM. Tumeshuhudia viongozi kadhaa waliokuwa katika vyama vya upinzani wakihama vyama vyao na kurudi CCM kwani wengi wao waliotokea huko. Ipo mifano kama akina Masumbuko Lamwai, Dr. Kaborouna wengi wenye nyadhifa na wanachama wa kawaida. Pia suala la vyama vya upinzani kuungana bado ni kitendawili kwani hao viongozi wana ubinafsi na tamaa za kutaka kuingia ikulu kitu ambacho hata Nyerere alikishangaa sana. Na aliwahi kusema kuwa hata kama wananchi wameamua kusukuma gari la kiongozi wa upinzani kwa nderemo na vigerere wawaache tu kwani alijua kuwa hawatafika mbali na sasa tunashuhudia upinzani ukielelea kufa kifo cha asilia. Kwa hiyo hata huyo Odinga anachowashauri hao ndugu ni wastage of time and energy tu lakini nadiriki kusema upinzani Tanzani "MUFIRISI".....
Pole sana zoba. Kwa taarifa yako upinzani wa kweli nchi hii hautatoka ccm. Mi na wenzangu wengi tu tunaomaliza vyuo sasa hatujawahi kuwa ccm hata kidogo na sasa tuko chadema. Na nakuhakikishia mkakati wetu ni kuipoteza kabisa hiyo ccm yako kwani hata wanachama mlionao wanaomaliza vyuo sasa ni wajinga wajinga tu kama wewe, hivyo tuna hakika hawawezi kuongoza nchi hawa. Nyerere(namheshimu) alikuwa binadam kabisa mwenye pum.bu mbili kama wewe hivyo maneno yake hayakuwa maandiko matakatifu. Upinzani wa kweli nchi hii hata sasa unatoka chadema, hilo usijifanye haulioni. Hao mamluki wanaoamia ccm wala siyo kitu cha ajabu ndo demokrasia na isitoshe wanaotoka ccm na kuja chadema ni wengi zaidi kama edwin mtei, wilbroad slaa, alkado ntagazwa nk.
 
Back
Top Bottom