Waliowahi kushika uongozi wa serikali ya wanafunzi vyuo vikuu wafuate nyayo za Zitto Kabwe

Kwa ujumla hii thread imevuta hisia za wengi, na pia imetukumbusha mengi hata kufahamu wengine wamefariki kwa kweli hii mada imenipa faraja na huzuni.
 
Njoka Ereguu;3998102]Kwa ujumla hii thread imevuta hisia za wengi, na pia imetukumbusha mengi hata kufahamu wengine wamefariki kwa kweli hii mada imenipa faraja na huzuni Aisee hii habari kwakweli Personally imenisononesha sana, Mpiganaji Mkili alishatutoka kumbe? Duh VERY VERY SAD, na kumbe Ruge alishajaribu jimbo la Mkenge! Very good kutukubusha majina mengine kama vile Makamu Emily Kivugo,Kashube, na Makabwe. Makabwe nadhani ndiye alikuwa waziri wa fedha DARUSO Mwaka 2000, na alikuwa na influence kubwa sana Nkrumah. Duh ila Kifo cha Mkiili aisee ni pigo kubwa sana kwa wapiganaji.
 
Kengele yuko kwenye timu ya magamba, kaligombea kura za Maoni Ukonga akashindwa. Sasa ni mjasiriamali mzuri na ulabu wake kama kawaida. Lakini umeamsahau chacha Mwikwabe alikuwa rais kipindi cha 2000. Wengine wako kama Dr. Kitila, ni matunda pia, yoko huyo jamaa wa Ulabu, bosi Serengeti na hata Batungirehi, yuko huyo jamaa wa CUF, Makamu wa Sefu nk. list ni ndefu
 
Kengele yuko kwenye timu ya magamba, kaligombea kura za Maoni Ukonga akashindwa. Sasa ni mjasiriamali mzuri na ulabu wake kama kawaida. Lakini umeamsahau chacha Mwikwabe alikuwa rais kipindi cha 2000. Wengine wako kama Dr. Kitila, ni matunda pia, yoko huyo jamaa wa Ulabu, bosi Serengeti na hata Batungirehi, yuko huyo jamaa wa CUF, Makamu wa Sefu nk. list ni ndefu

Mwenye data za walifukuziwa Sua plz atupe, kuna wapiganaji vichwa walianzia udsm na kwenda sua na moto uleule hasa dhidi ya cost sharring. Walikuwa na ushawishi mkubwa sana kiasi cha serikali na uongozi wa chuo kuogopa nguvu na hoja zao za kutetea umma kwa gharama yoyote. Walikuwa vichwa sana katika taaluma pia. Serikali ya mzee ruksa ikawafukuza maskini.
Kuna kijana mmoja sikumbuki jina lake,yeye alitokea udsm ambako alipigania sana na kubadilisha upepo ghafla pale nkruma katika kutetea haki za wanachuo na hali bora. Akahamia sua na kuongoza harakati dhidi ya cost sharring. Waziri wa elimu ya juu kipidi ile dr shija hatamsahu huyu kijana jasiri. Naye alifukuzwa kwa barua yenye muhuri wa siri wa ikulu! Huyu alikuwa mtaalamu wa mapinduzi.
Nchi hii bwana! Imepoteza watu na vipaji vyao muhimi sana.
Ni miaka ya tisini.

Mungu awbariki hawa watu. Walijitoa sadaka kwa manufaa ya taifa letu.
 
mgomo wa mwaka 1999 - 2000 uliacha majeruhi wengi MUCHS akiwepo Dux, Alex Kazula na wengine wa mlimani kama akina Galan Mashenene...hawa ndg waliwekwa ndani kwa muda wa kutosha na benchi kwa muda mrefu, nadhani karibu a full academic year
 
HKigwangalla;4007387]mgomo wa mwaka 1999 - 2000 uliacha majeruhi wengi MUCHS akiwepo Dux, Alex Kazula na wengine wa mlimani kama akina Galan Mashenene...hawa ndg waliwekwa ndani kwa muda wa kutosha na benchi kwa muda mrefu, nadhani karibu a full academic year


Hebu DR. tufahamishe huyu bwana Galan Mashenene yuko wapi kwa sasa, nilipoteza mawasiliano naye Mwaka 2000, kama kuna mtu ana contacts zake naomba, ni rafiki yangu sana, huwa namtafuta si mpati.
 
Matiko Matare hakuacha kwa hiari ila alifukuzwa baada ya kuongoza mgomo mkubwa wa 1990 uliotikisa nchi kwani ulikuwa una lengo la kumwondoa Mwinyi madarakani. Sikumbuki kama Luhanga ndiye alikuwa VC. But I remember VC alikuwa Mmari. Luhanga ameanza 1991. Matiko alipelekwa kijijini kwao kwa helkopta ya serikali na kuwekewa kizuizi cha kutotoka kijijini kwao for 5 yrs. Baada ya 5yrs serikali iliendelea kumfuatilia sana kupitia idara ya usalama wa taifa hata alipokwenda kufundisha Musoma techical sec school (zamani maarufu kama musoma alliance) na baadaye mwembeni sec school hapo hapo musoma.baadhi ya watu waliokuwa wanamfuatilia ninawafahamu.Yeye nimewahi kuongea naye mara nyingi lakini nashukuru kwa kufahamu alipo sasa. Frankly speaking, yule jamaa ana uwezo mkubwa kichwani.

Umenena ukweli...Matiko amenifundisha musoma tech high school...kulitokea fujo kubwa sana...uongozi ukamtimua kuwa ndie anaetuhamasisha kugoma in 2004!
 
John Kengele au kama alivyokuwa akipenda kuitwa "Mzee'' Alisababisha dada Halima Dendego atoe jina lake katika kinyang'anyiro cha Umakamu wa daruso,maana alielezwa kengele angemmumbua pale nkrumah uhusiano wake aliokuwa nao na mmoja wa wawaliokuwa akitegemewa kugombea ukuu wa kaya!Ikabidi Dendego ateme Mzigo,Sasa halima ni DC tanga!!!!
 
Nimempigia Matiko Matare kwa namba hii tuliyopewa hapa JF, kumbe ni kamanda tangu enzi za Edwin Mtei, na amesema ana mwanae yuko hapa UDSM engineering anaitwa Julius Matiko. Nimemshawishi ajiunge JF tena kwa ID yake ya Matiko Matare akakubali kwahiyo tujiandae kupokea kamanda wetu.

Wengi mtashangaa nimehamasikaje, ukweli ni kwamba kuna kaka yangu alikuwaga anasoma hapo Mlimani enzi hizo tuko wadogo akawa anakuja kutupa habari za huyu mtu, nikawa naguswa na harakati zake ila baadae nikasikia kajinyonga kumbe yuko hai ni njama za magamba tu

Sent from my BlackBerry 9910 using JamiiForums
 
hii post imenifurahisha sana,BIG UP ALL THEN LEADERS,kweli kwa namna hiyo mlifanya kazi kubwa sana,I wish wote wangekuwa kwenye harakati za ukombozi zinazoendelea nchini kwa sasa.nimeona kwa namna gani ss viongozi wa serikali za wanafunzi vyuon kwa sasani kama hatuna impacts kwa TAIFA compared kwa yaliyofanywa na wenzetu wa kwanzia 1990'S mpaka 2005'S
 
Huu Uzi usipotezwe ni moja kati ya uzi kali sana na utachangiwa kiakili zaidi nafikiri utaleta uhamasisho mkubwa na ujasiri wa hali ya juu. Big up JF kwakutuunganisha na tunaombeni mtuletee mashujaa wengine na harakati zao ili tupate historia zaidi
 
Umenena ukweli...Matiko amenifundisha musoma tech high school...kulitokea fujo kubwa sana...uongozi ukamtimua kuwa ndie anaetuhamasisha kugoma in 2004!

Nakumbuka kipindi hicho nilikua naingia form 6 ndo tukasimamishwa masomo kwa muda usiojulikana kisha tukarejeshwa baadaye. Mi nilikua nasomea darasa lililokua next to lango la giningi halafu kadarasa ketu kalikua na wanafunzi 21 tu. Vilevile kuna mwanafunzi alidondoka uwanjani siku ya michezo jioni akafariki palepale. Tulimpeleka kwao ukerewe. Jamani musoma tech naikumbuka sana.
 
Msaliti John Kusaja yupo UDOM siku hizi...... msimsahau kamanda mwingine Dr. Kitila Mkumbo ambaye sasa ni mkuu wa idara kule Taasisi ya elimu UDSM.......kuna Julius Mtatiro ambaye yuko CUF.....
 
Wana JF, kuna Vijana wanaharakati enzi zile miaka ya 2000-2003, Chuo Kikuu cha Dsm tuliwahi kuwa na Viongozi shupavu sana ambao waliwahi kuweka ndani pamoja na kutimuliwa Chuo Kikuu cha DSM kwa kuongoza migomo ambayo tulifukuzwa chuo kizima na tukarudi nyumbani takribani miezi mitatu,

Uongozi wa DARUSO ulikuwa unaongozwa na msaliti mmoja aliyekuwa anaitwa Julius Kusaja, ambaye alijitoa kwenye mgomo na baada ya hapo katibu wake Mr. Gervas Mkili na Makamu aliongoza migomo mpaka wakawekwa ndani na baadaye wakatimuliwa, ila kwa baadaye tuligoma tena wakarudishwa Chuo.

Kati yao walikuwemo Zitto Kabwe, Gervas Mkili mwenyewe, Julius Rugemarila, Waziri fulani wa Fedha jina ilimenitoka, na wengine wengi. Lakini ni Zitto peke yake ambaye tayari matunda yake tunayona hadi sasa, ila wengine mlipotelea wapi baada ya Chuo maana mlikuwa very strong kuliko hata Zitto kama vile Gervas Mkili ( Shy/Khm) na Julius Rugemarila (Mwz/Bukoba).

Je kuna mwana JF yoyote ambaye anatarifa nao? tunapenda wajitokeze ili tuendelee na hii M4C ili tuweze kuwabadilisha wa Tz na kujihakikishia ushindi wa kishindo 2015, twendeni tukiunganisha nguvu kwa pamoja siyo msubiri tu 2015 baada ya ushindi ndo mjitokeze.

Ila yeye Kusaja nadhani yuko kigambagamba alitusaliti na akabakishwa UDSM utawala.

Nawasilisha ili ujumbe uwafikie michango yao ni muhimu sana.

Bwana skalulu sijaelewa nia yako ila naona unataka "trouble makers" wote wa vyuoni wajiunge CDM; mkianza kutofautiana humo ndani ya chama nani atakuwa msuluhishi?
 
Last edited by a moderator:
HKigwangalla;4007387]mgomo wa mwaka 1999 - 2000 uliacha majeruhi wengi MUCHS akiwepo Dux, Alex Kazula na wengine wa mlimani kama akina Galan Mashenene...hawa ndg waliwekwa ndani kwa muda wa kutosha na benchi kwa muda mrefu, nadhani karibu a full academic year


Hebu DR. tufahamishe huyu bwana Galan Mashenene yuko wapi kwa sasa, nilipoteza mawasiliano naye Mwaka 2000, kama kuna mtu ana contacts zake naomba, ni rafiki yangu sana, huwa namtafuta si mpati.

Robert Mashenene Galani ni Mwalimu CBE pale Dodoma! Piga general line ya chuo utampata!
 
historia ya kufukuzwa chuo inachekesha viongoz wa DARUSO 2012 KAMA DANIEL NAFTAL,ANOLD PETER,MKENDA PAUL,GASTON GARUBIND na walafukuzwa kwa uchadema kisa walishinikiza utawala kwa mgomo iwarudishe wanafunz 48 waliofukuzwa 14/12/2011 this is very bad indeed:A S 465::A S 465:
 
Oh yeah, plz kuna wapiganaji makini wa miaka ya tisini katika vyuo vikuu waliopigania mfumo wa vyama vingi na kupinga cost sharing katika vyuo vikuu. Udsm,ardhi,sua,mzumbe na dar-tec. Kwa kweli walikuwa vichwa darasani na nje ya darasani lakini serikali kama kawaida iliwafrustrate kwa kuwafukuza vyuoni na kuwanyima kila nafasi ya kuendelea isipokuwa kwa wale ambao wazazi wao walikuwa na uwezo au majina na nafasi kubwa.
Wana jf wanao jua hawa mashujaa waliosahauliwa watuambie wako wapi na wanafanya nini sasa, kulikuwa na vichwa vya ajabu sana pale udsm na sua.
mzee ruksa alipata shida sana na vijana wale jinsi walivyokubalika na wasomi wenzao kwa maslahi ya taifa hili, waliweza kupindua serikali zao zilizokua vibaraka na kuunda serikali za vyuo imara. Waliadhibiwa kwa kutetea maslahi mapana ya taifa.

Anaye wafahamu atujuze tafadhali kwa manufaa ya kumbukumbu na historia ya mwanzo wa mapambano mapya ya ukombozi wa pili wa taifa hili baada ya uhuru.
James Mbatia alikua mmoja wapo na mangi mwenziwe Kimaro alikua pale Muhimbili sijui Kimaro kaishia wapi Mbatia naona bado yupo ngangari
 
UDSM (Wanafunzi 10 waliofukuzwa tarehe 10 February 1992)

1. James Mbatia-Mbunge Simu: 0787 979068
2. Mosena Nyambabe-Mfanyabiashara (anakaa Ukonga Mombasa)-Amepambana mara 3 na Dr. Wanyancha katika ubunge huko Serengeti. Kwa mara ya mwisho aligombea kwa tiketi ya CUF.
3. Kelvin Mmari-Lecturer Oregon University huko Marekani. Ana uraia wa Marekani na kati ya wataalam wa kompyuta wanaoheshimika huko Marekani.
4. Fabian Lutalemwa-Sina habari naye tangia miaka ya 90.
5. Ludovick Bazigiza-Marehemu
6. Idrisa Ruta Alnoor-Marehemu
7. Jasson Kaishozi-Marehemu (Alikuwa wakili wa Serikali kesi ya Zombe)
8. Aroun Kimaro-Marehemu (Alikuwa Daktari Bingwa Zimbabwe na Mfanyabiashara mashuhuri. Alipitia mkono wa Mchungaji Mtikila)
9.Rwekamwa Rweikiza-Mhasibu. Alipata CPA mwaka 1996, nimesoma naye MBA pale UDSM na sasa anasoma digrii ya kwanza ya Sheria OUT. Vile vile ana PGDHRM ya IFM. Yuko Dar (Simu-0754 275 305)
10. Kimweri-Marehemu (Alimalizia Digrii yake ya uchumi Makerere University. Alifariki kwa ajali ya gari miaka ya 90 akiwa njiani kuelekea Zimbabwe kwa Kimaro)

Wengine

1. Matiko Matare-Aliongoza mgomo wa mwaka 1990 uliosababisha chuo kifungwe kwa mwaka mmoja. Aliacha UDSM kwa hiari kipindi kile ambapo kuliwa na njaa kali kule Musoma. Alimwambia mkuu wa Chuo (Luhanga) ampe nauli aende nyumbani kwa sababu hakuona haja ya kusoma wakati ndugu zake wanakufa kwa njaa, vingineyo angejinyonga. Wakati huo alikuwa mwaka wa 3. Mkuu wa Chuo alitii amri. Baadaye alijiunga OUT na kuwa mwanafunzi wa kwanza kumalizia digrii ya sheria kwa miaka 3. Baadaye alisoma MA (Distance Learning) hapo hapo OUT. Yuko Songea. Namba yake ni 0757 282151. Anajiandaa kurudi katika siasa kwao mkoani Mara.


DIT

1. Mtoka Mtwangi-Sina mawasiliano naye tangia miaka ya 90. Alimalizia Advanced Diploma yake Kenya Polytechnic College.
Halafu watu wanasema mzee ruksa alikua mzuri. Mzuri kivipi kafunga wanafunzi wengi kuliko rais yeyote hapa Tanzania. Jamaa huwezi jua kama alikua mwalimu, nilidhani mwalimu tawapenda wanafunzi huyu jamaa sijui ni mwalimu wa madrasa sijui maana madrasa peke yake mwalimu anaruhusiwa kupiga watoto kama mbwa
 
Watanzania walikuwa(na baadhi yao bado) na upeo mdogo sana wa kuyaona mambo yanavyokwenda mrama wakati wa utawala wa mzee Mwinyi. Mwinyi hakuwa kiongozi mzuri, siyo tu ndani ya serikali ya JMT bali hata katika chuo kikuu UDSM. Hakufika na wala hakuja hata siku moja kuzungumza na wanafunzi wa UDSM ingawa yeye alikuwa ndiyo mkuu wa chuo hicho, alionyesha udhaifu mkubwa sana yeye akiwa kama kiongozi, hata baada ya kuombwa na wanafunzi aje kuonana nao, yeye aliendelea kukataa kata kata. Madudu yaliyokuwa yakifanyika ndani ya serikali na kufichuliwa na wanafunzi wa UDSM na kuwa na ushahidi wote ndiyo uliyomfanay Mzee ruksa akatae kabisa kuja pale maana ingekuwa ni aibu na angeshindwa kuzungumza lolote, na hata hao washauri wake ambao ndiyo walikuwa wakiyalinda madudu hayo, walimshauri hivyo. Kwa hiyo alichukua hatua za mabavu za kuwafukuza wanafunzi wote na kuwaweka "kifungo cha nje". Wanafunzi hawakuwa wakorofi, walikuwa ni wasomi wazuri tu na walikuwa wanaona mbali na walikuwa na uchungu sana na hivyo kutaka watanzania wote wafaidike na matunda ya nchi yao, kinyume na viongozi wabadhirifu waliokuwepo wakati huo, ambao waliona kuwa wanafunzi walikuwa wanataka kuwaamsha wantanzania ambao walikuwa wamelala!! Matiku Matale alikuwa kiongozi wa wanafunzi, kiongozi mzuri tu. Bazigiza alionewa na hata kuwekwa ndani kwa ujinga wa baadhi ya viongozi kwa kuwa tu alisema ukweli (pyongyang). Mashuhuda wa waliyoyaona yote haya bado wapo, kama Prof Shivji, na wengine wameshaenda mbele ya haki (Prof. H Othman) RIP, hao na wengine walikuwa ni watetezi wa wanyonge na wasema kweli, na hata wao walipoitwa Ikulu walitishwa na mzee Ruksa na kuwaonya kuwa watapoteza kazi zao endapo wataendelea kuwa pamoja na wanafunzi na kusema ukweli.Namkumbuka pia (yeye hakuwa kiongozi) Ali Saleh, kutoka zanzibar, alivyokuwa anasakamwa na usalama wa taifa mpaka uongozi wa chuo ulipoingilia kati suala hilo. Matiku alitekwa (alichukuliwa kwa nguvu) na vijana wa usalama wa taifa ndani ya campus ya UDSM na kupelekwa kwa Warioba kuzungumza naye. sasa mzee Mwinyi ndiye aliyeanza kuiharibu TZ, alikuwa ni against na wasomi (yeye mwenyewe hakuwa msomi) na kuwasaidia na kuwapa favor watu wake. Viongozi wa wanafunzi pale chuoni wa muda wowote, walikuwa ni vichwa na wazalendo. Na kama wangekuwa ndani ya uongozi wa serikali basi sasa hivi tungekuwa mbali, akina Magufuli walikuwa wako wengi lakini walikuwa hawatakiwi kwa sababu tu ya kuwatetea watanzania masikini na wanyonge. Mh. magufuli watafute vijana hao na wape shughuli wafanye halafu uone matokeo yake.
 
Back
Top Bottom