Waliouawa na polisi maandamano Chadema Arusha watajwa

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
POLISI mkoani Arusha imewataja watu wawili waliouawa na askari wake kwa risasi za moto katika vurugu zilizotokana na maandamano yaliyofanyika juzi mkoani hapa.

Mbali na watu hao, Denis Maiko na George Mwita Waitara wote wakazi wa Sakina jijini hapa, watu wengine wanane wakiwemo askari watatu walijeruhiwa katika vurugu hizo huku wengine 49 wakishikiliwa na polisi.

Kutokana na ufinyu wa nafasi katika kituo cha Polisi, wafuasi 49 wa Chadema waliokamatwa walilazimika kulala ndani ya karandinga usiku kucha hadi jana walipoachiwa baada ya kupewa dhamana na Mahakama.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye amethibitisha hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa majeruhi hao wanane wamesambazwa katika hospitali mbalimbali kwa matibabu zaidi.

Mbali na vifo na majeruhi hao, pia mali mbalimbali ziliharibiwa kutokana na kurushiwa mawe na raia wakati walipokuwa wakirejea kutoka mkutanoni.

Mali zilizoharibiwa kwa mawe ni pamoja na magari ya Polisi, jengo la CCM Mkoa pamoja na magari yaliyokuwemo ndani ya jengo hilo na jengo la mfanyabiashara maarufu jijini Arusha, Salum Ally lililopo mtaa wa Bondeni.

Polisi wanaendelea kufanya tathmini ya hasara na uharibifu uliotokana na vurugu hizo za juzi ambapo jana walionekana katika jengo la CCM wakichukua picha za video kwa ajili ya ushahidi wa hasara.
 
POLISI mkoani Arusha imewataja watu wawili waliouawa na askari wake kwa risasi za moto katika vurugu zilizotokana na maandamano yaliyofanyika juzi mkoani hapa.

Mbali na watu hao, Denis Maiko na George Mwita Waitara wote wakazi wa Sakina jijini hapa, watu wengine wanane wakiwemo askari watatu walijeruhiwa katika vurugu hizo huku wengine 49 wakishikiliwa na polisi.

Kutokana na ufinyu wa nafasi katika kituo cha Polisi, wafuasi 49 wa Chadema waliokamatwa walilazimika kulala ndani ya karandinga usiku kucha hadi jana walipoachiwa baada ya kupewa dhamana na Mahakama.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Thobias Andengenye amethibitisha hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari na kusema kuwa majeruhi hao wanane wamesambazwa katika hospitali mbalimbali kwa matibabu zaidi.

Mbali na vifo na majeruhi hao, pia mali mbalimbali ziliharibiwa kutokana na kurushiwa mawe na raia wakati walipokuwa wakirejea kutoka mkutanoni.

Mali zilizoharibiwa kwa mawe ni pamoja na magari ya Polisi, jengo la CCM Mkoa pamoja na magari yaliyokuwemo ndani ya jengo hilo na jengo la mfanyabiashara maarufu jijini Arusha, Salum Ally lililopo mtaa wa Bondeni.

Polisi wanaendelea kufanya tathmini ya hasara na uharibifu uliotokana na vurugu hizo za juzi ambapo jana walionekana katika jengo la CCM wakichukua picha za video kwa ajili ya ushahidi wa hasara.
Hasara hiyo mbona nadhani ni ndogo? Inatakiwa kuwe na hasara kubwa kiasi cha kutisha. Mi sijaona hasara yoyote.
 
Hasara kubwa ni kupoteza maisha ya watu waio na hatia

sure,hope hlo litamsumbua kila mmoja aliye kwenye system,kumwaga damu bila hatia ni risk n cost!wale wameacha watu wanaowategemea,itakuaje?JINAMIZI HILO LITAWASUMBUA SANA,TENA SANA!
 
Nawaomba waJFwenye wenye taarifa sahihi kwa maana ya majina au watu waliokufa au kujeruiwa tuweke wazi majina ya wahanga hao hapa JF.

Waliouwawa....
Denis Shirima - huyu ni fundi magari
George Mwita Waitara
........
........


Majeruhi
........
........
 
Back
Top Bottom