nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
Tanzania Daima
KATIBU Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Luteni Yusuf Makamba na Katibu Mkuu Mstaafu wa chama hicho, Philip Mangula, wamezawadiwa mashangingi mapya, aina ya V8, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Habari ambazo gazeti hili imezipata, zimesema kuwa magari hayo yametolewa na chama kwa watendaji hao wastaafu ili kuuenzi mchango wao.
Wakati Makamba akiwa ameachiwa gari jipya alilokuwa akilitumia, Mangula amepewa gari jipya kabisa.
Mbali ya Mangula na Makamba, Makatibu wa NEC kwenye sekretarieti nao wamepewa mashangingi mapya aina ya V8.
Habari zinasema kuwa mashangingi hayo ndiyo yaliyotumika wakati wa kampeni za kumnadi mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Mbali ya Katibu Mkuu, Willison Mkama na Naibu wake, John Chiligati, wengine waliopewa magari hayo kwa ajili ya shughuli zao za kuimarisha chama ni Nape Nnauye (Itikadi na Uenezi), Januari Makamba (Siasa na Mambo ya Nje) na Lameck Mwigullu Mchemba (Uchumi na Fedha).
Akizungumzia hali hiyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amesema kuwa huo ni utaratibu wa kawaida kwa chama kuwaenzi watendaji wake.
Ni utararibu wa kawaida wa chama. Hata Mangula alipoondoka, gari alilokuwa akilitumia alikabidhiwa, lakini sasa limeharibika na chama kimeamua kumpa lingine, Makamba naye ameachiwa gari alilokuwa akilitunia, alisema Nape.
Mangula ambaye alienguliwa kwenye nafasi ya ukatibu mkuu, alitumikia nafasi hiyo kwa muda wa miaka kumi chini ya mwenyekiti wake, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa.
Nafasi ya Mangula ilichukuliwa na Luteni Makamba ambaye ameitumikia nafasi hiyo kwa miaka sita hadi wiki iliyopita nafasi yake ilipochukuliwa na Mukama.
Wakati huohuo, siri ya Rais Jakaya Kikwete kumteua Mukama kurithi mikoba ya Makamba, imebainika.
Vyanzo vyetu vya habari vilisema kuwa Mukama amepewa nafasi hiyo kwani ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa tume iliyoundwa kwa siri na Rais Kikwete kufanya tathmini ya Uchaguzi Mkuu na sababu za chama kupoteza umaarufu.
Ripoti ya Mukama ambayo ilisheheni wanazuoni, ndiyo iliyopendekeza mabadiliko makubwa ya kujivua gamba kwa kuwavua baadhi ya viongozi kwenye nafasi zao na kupendekeza watuhumiwa wa ufisadi waliokifikisha chama mahala kilipo sasa, wajiondoe au wangolewe baada ya miezi mitatu.
Mukama ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa tume hiyo na imekuja na mapendekezo mengi, hivyo Rais Kikwete ameamua ampe nafasi hiyo Mukama ili apate nafasi ya kuyatekeleza aliyoyapendekeza kwenye tume yake, kilisema chanzo chetu cha habari.
Mbali ya kupendekeza fumua fumua na kutaka mafisadi wangolewe, mapendekezo mengine ya tume ya Mukama ni kutaka wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) wachaguliwe kutoka kwenye wilaya zao badala ya mkutano mkuu ili kukiweka chama karibu na wananchi. Pia kimependekeza utaratibu na vigezo vya kumpata mgombea wa kiti cha urais ambavyo ni tofauti na utaratibu wa zamani wa chama hicho.
KATIBU Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Luteni Yusuf Makamba na Katibu Mkuu Mstaafu wa chama hicho, Philip Mangula, wamezawadiwa mashangingi mapya, aina ya V8, Tanzania Daima Jumatano limebaini.
Habari ambazo gazeti hili imezipata, zimesema kuwa magari hayo yametolewa na chama kwa watendaji hao wastaafu ili kuuenzi mchango wao.
Wakati Makamba akiwa ameachiwa gari jipya alilokuwa akilitumia, Mangula amepewa gari jipya kabisa.
Mbali ya Mangula na Makamba, Makatibu wa NEC kwenye sekretarieti nao wamepewa mashangingi mapya aina ya V8.
Habari zinasema kuwa mashangingi hayo ndiyo yaliyotumika wakati wa kampeni za kumnadi mgombea wa CCM, Rais Jakaya Kikwete.
Mbali ya Katibu Mkuu, Willison Mkama na Naibu wake, John Chiligati, wengine waliopewa magari hayo kwa ajili ya shughuli zao za kuimarisha chama ni Nape Nnauye (Itikadi na Uenezi), Januari Makamba (Siasa na Mambo ya Nje) na Lameck Mwigullu Mchemba (Uchumi na Fedha).
Akizungumzia hali hiyo, Katibu wa Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, amesema kuwa huo ni utaratibu wa kawaida kwa chama kuwaenzi watendaji wake.
Ni utararibu wa kawaida wa chama. Hata Mangula alipoondoka, gari alilokuwa akilitumia alikabidhiwa, lakini sasa limeharibika na chama kimeamua kumpa lingine, Makamba naye ameachiwa gari alilokuwa akilitunia, alisema Nape.
Mangula ambaye alienguliwa kwenye nafasi ya ukatibu mkuu, alitumikia nafasi hiyo kwa muda wa miaka kumi chini ya mwenyekiti wake, Rais mstaafu, Benjamin Mkapa.
Nafasi ya Mangula ilichukuliwa na Luteni Makamba ambaye ameitumikia nafasi hiyo kwa miaka sita hadi wiki iliyopita nafasi yake ilipochukuliwa na Mukama.
Wakati huohuo, siri ya Rais Jakaya Kikwete kumteua Mukama kurithi mikoba ya Makamba, imebainika.
Vyanzo vyetu vya habari vilisema kuwa Mukama amepewa nafasi hiyo kwani ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa tume iliyoundwa kwa siri na Rais Kikwete kufanya tathmini ya Uchaguzi Mkuu na sababu za chama kupoteza umaarufu.
Ripoti ya Mukama ambayo ilisheheni wanazuoni, ndiyo iliyopendekeza mabadiliko makubwa ya kujivua gamba kwa kuwavua baadhi ya viongozi kwenye nafasi zao na kupendekeza watuhumiwa wa ufisadi waliokifikisha chama mahala kilipo sasa, wajiondoe au wangolewe baada ya miezi mitatu.
Mukama ndiye aliyekuwa mwenyekiti wa tume hiyo na imekuja na mapendekezo mengi, hivyo Rais Kikwete ameamua ampe nafasi hiyo Mukama ili apate nafasi ya kuyatekeleza aliyoyapendekeza kwenye tume yake, kilisema chanzo chetu cha habari.
Mbali ya kupendekeza fumua fumua na kutaka mafisadi wangolewe, mapendekezo mengine ya tume ya Mukama ni kutaka wajumbe wa Halmashauri Kuu (NEC) wachaguliwe kutoka kwenye wilaya zao badala ya mkutano mkuu ili kukiweka chama karibu na wananchi. Pia kimependekeza utaratibu na vigezo vya kumpata mgombea wa kiti cha urais ambavyo ni tofauti na utaratibu wa zamani wa chama hicho.