Kizimkazimkuu
JF-Expert Member
- Nov 8, 2007
- 337
- 234
Lilikuwapo kundi kubwa la watu waliombeza sana Kocha mbrazil Marcio Maximo,hasa baada ya kushindwa michezo ya Chalenji na matokeo ya kutoridhisha katika baadhi ya mechi.Kocha alipata lawama kubwa sana katika uchaguzi wa kikosi chake.majina kama Shaban Dihile,Jerry tegete( kuna baadhi ya magazeti yalimuita mtalii),Kigi makassy,nk yalionekana hawakustahili kuwamo kwenye kikosi.
Wapo wanahabari waliodiriki kuandika kuwa maximo sio kocha ,bali ni mtaalam wa uhamasishaji,na kuwa kikubwa alichofanikiwa nchini ni kuhamasisha mashabiki kuipenda na kuishangilia timu.Kati ya watu walioongoza kumponda kocha maximo waziwazi ni Kocha 'maarufu' nchini Syllersaid Mziray kupitia makala zake kwenye magazeti.Sijui leo wako wapi hawa critics wetu wa soka la bongo?
Wapo wanahabari waliodiriki kuandika kuwa maximo sio kocha ,bali ni mtaalam wa uhamasishaji,na kuwa kikubwa alichofanikiwa nchini ni kuhamasisha mashabiki kuipenda na kuishangilia timu.Kati ya watu walioongoza kumponda kocha maximo waziwazi ni Kocha 'maarufu' nchini Syllersaid Mziray kupitia makala zake kwenye magazeti.Sijui leo wako wapi hawa critics wetu wa soka la bongo?