Waliokaa kimya hoja ya wagombea binafsi- Ndiyo imekula kwao!

Mkuu kama ndivyo basi dawa ni kurekebisha mfumo mzima wa Upigani kura za maoni na sio kupachika kiraka nje ya tobo kama style ya nguo tukidai tunaziba pengo hilo.

Mimi sitazami wagombea Binafsi kwa kuitazama CCM au kwa nini CCM hawataki wagombea binafsi isipokuwa natazama utaratibu wa kisiasa (demokrasia) ktk kuwepo wagombea binafsi. Hawa wote wanaodai kuwa wagombea binafsi wanachukua nafasi hiyo kwa sababu wanajua hawawezi kupita ktk uchaguzi wa ndani CCM. Sasa kwa nini wanabakia CCM hali wanaweza kwenda vyama vingine wakapita uchaguzi ikiwa wananchi wanawakubali?..Au onyesha utofauti wako na CCM kiitikadi bila shaka tutakuwa nyuma yako kukubali kama alivyojitangaza Rev. Kishoka.

Kama unataka kugombea Ubunge au kiti chochote cha kisasa ni lazima uwe na mtazamo tofauti na mpinzani wako kiitikadi laa sivyo tunapelekea kuamini kwamba Ni mtu anayeweza kutuwakilisha na sio sera za mtu huyo. Yale yale ya kitumwa kuamini wazungu (watu weupe) ndio wanajua kuliko weusi pasipo hata kueleza tofauti ya uwezo wao. Tukumbuke tu kwamba siasa na itikadi ni Ubunifu wa mirengo ya kuboresha maisha ya jamii zetu, sasa ikiwa tuna watu 10 wenye itikadi sawa na tuwape nafasi za wagombea binafsi hali mchango wao hauna tofauti na ule wa mgombea wa CCM tunakuwa tunapoteza muda na fedha za wananchi.
Ni sawa na utaratibu wa Taxi kuchukua abiria, kama unalo gari na unataka kulifanya Taxi nenda kasajili ktk jumuiya ya wana taxi kisha fanya biashara zako lakini sio kuomba haki ya kila mwenye gari aruhusiwe kusanya anapopenda kwa sababu tu kuna matatizo ktk mfumo wa jumuiya ya wanaTaxi. Hutaki Taxi ingia kwenye Daladala hutaki pia jaribu kufikiria kuanzisha njia usafiri mwingine utakao pingana na jumuiya zilizopo na sio kuomba kibali cha kusanya.

Wonna be a Politiacian, be a Politician kwa kujiunga na chama unachokubali sera zao au pingana na itikadi za vyama vilivyopo.Leo hii tuna vyama zaidi ya 20 tena chini ya sheria kama hii tukiachia hapo unafikiria tutakuwa na wagombea wangapi?..

Uchaguzi wa CCM tu umetuonyesha jinsi gani watu walijitokeza kugombea hali nimegundua kwamba CCM yenyewe haina hata wananchama zaidi ya millioni moja kutokana na hesabu ya wapiga kura. Matokeo yote ya kura za maoni za CCM ni ishara nzuri kwetu kutonyesha jinsi watu tulivyokuwa walafi wa madaraka badala ya uwakilishi wa wananchi kupitia chama.

Mkandara fikiria hivi, leo hii kuna watu wa Chadema wametemwa/watatemwa ili kupisha watu wengine. Watatemwa si kwa sababu walishinda vibaya au kwa rushwa bali kwa sababu watu wengine wanahitajika (kwa mfano Mpendazoe kupewa Segerea japo alishindwa). Yule aliyeenguliwa akiamini kuwa bado anakubalika na wananchi wengi (zaidi ya wanachama) anatakiwa aidha akubali tu au atafute mahali pengine pa kugombea. Sasa, matokeo yake ni kuwa mtu ANALAZIMISHWA kujiunga na chama kingine ili AGOMBEE.

Na hili tutaliona kuanzia J'pili hii, baada ya majina ya vigogo kuthibitishwa kutupwa na KK basi wataanza kukimbilia hasa Chadema (sources zangu zinanithibitishia kuwa kuna vigogo wameomba Chadema wasitangaze baadhi ya majimbo wagombea wake ili wasubiri kupata matokeo ya KK). Watu hawa kama ni waumini wazuri wa CCM wanabakia kujiuliza, je wasubiri miaka mitano mingine au waruke na waingie upinzani ili wagombee mwaka huu?

Kwa vile dirisha liko wazi kwa karibu siku nne tu (August 14-19) basi ni wazi kimbilio itakuwa ni kuwa wapinzani. Lakini si kwa sababu wanaamini au ni wapinzani kweli; la! bali ni kwa sababu ya nafasi (opportunity). Lakini kama kungekuwa na wagombea huru/binafsi wanachamah hao wanaoenguliwa wangeweza kusimama wenyewe (binafsi) bila KULAZIMISHWA kuhama vyama vyao. Na wakishinda bado wanabakia ni wanachama wa vyama vyao.

Kwanini hili ni baya?
 
wa vyama na binafsi! na akaheshimu matokeo yake.

Aliruhusu halafu akaharamisha, kama John Kerry aliye "vote for the war, before he voted against it".

C'mon, huwezi kumpa Nyerere credit ya kuruhusu wagombea binafsi / vyama vingi, alifunga milango yote hii in the 60's na haikufunguliwa tena mpaka 1992 under Mwinyi. Kama unataka kumpa mtu credit kwamba analau imetokea under his watch angalau unaweza kusema mtu huyo ni Mwinyi.
 
Aliikuta halafu akaharamisha


Alipoanza new state, alivyoviacha aliviruhusu. Naweza kusema aliruhusu kwa sababu alianza ukurasa mpya na kama angetaka kupiga marufuku from day one angeweza. It is not like alikuwa second president aliyekuta system, alikuwa first president aliyetengeneza system mpya.

From that reasoning, naweza kusema "aliruhusu halafu akaharamisha" na si "alikuta halafu akaharamisha".
 
Mkandara fikiria hivi, leo hii kuna watu wa Chadema wametemwa/watatemwa ili kupisha watu wengine. Watatemwa si kwa sababu walishinda vibaya au kwa rushwa bali kwa sababu watu wengine wanahitajika (kwa mfano Mpendazoe kupewa Segerea japo alishindwa). Yule aliyeenguliwa akiamini kuwa bado anakubalika na wananchi wengi (zaidi ya wanachama) anatakiwa aidha akubali tu au atafute mahali pengine pa kugombea. Sasa, matokeo yake ni kuwa mtu ANALAZIMISHWA kujiunga na chama kingine ili AGOMBEE.

Na hili tutaliona kuanzia J'pili hii, baada ya majina ya vigogo kuthibitishwa kutupwa na KK basi wataanza kukimbilia hasa Chadema (sources zangu zinanithibitishia kuwa kuna vigogo wameomba Chadema wasitangaze baadhi ya majimbo wagombea wake ili wasubiri kupata matokeo ya KK). Watu hawa kama ni waumini wazuri wa CCM wanabakia kujiuliza, je wasubiri miaka mitano mingine au waruke na waingie upinzani ili wagombee mwaka huu?

Kwa vile dirisha liko wazi kwa karibu siku nne tu (August 14-19) basi ni wazi kimbilio itakuwa ni kuwa wapinzani. Lakini si kwa sababu wanaamini au ni wapinzani kweli; la! bali ni kwa sababu ya nafasi (opportunity). Lakini kama kungekuwa na wagombea huru/binafsi wanachamah hao wanaoenguliwa wangeweza kusimama wenyewe (binafsi) bila KULAZIMISHWA kuhama vyama vyao. Na wakishinda bado wanabakia ni wanachama wa vyama vyao.

Kwanini hili ni baya?
Ubaya wake unakuja kwamba unataka kutunga sheria kwa sababu ya kile kinachotokea leo CCM/Chadema. Kumbuka Mgombea Binafsi ni sehemu ya Demokrasia sasa huwezi kuuweka utaratibu huu kwa sababu ya kufidia matukio kama haya ya watu kuhama CCM kuingia Chadema.

Mgombea binafsi anajisimamia kwa kufuata utaratibu iwe kuna watu wanahama chama au hawahami, iwe kuna matukio kama yetu ama hakuna. Na sifa kubwa ya Mgombea binafsi huwa ni mtu aliyekuja na fikra mpya, fikra zinazokinzana na itikadi za vyama vilivyopo ktk baadhi au sera za vyama vilivyopo.. Lakini tukitaka kuweka wagombea binafsi pasipo kuzingatia itikadi zao basi ni sawa na kukubali Wagombea binafsi kama wawakilishi wa itikadi moja ambayo haipo.

Kinachotokea kwa Chadema ni marudio ya mwaka 1995 kwani tulipounda vyama vingi utakuta waliokihama CCM ni wale waliopoteza nafasi zao wakati wa Mwinyi. Kila aliyetupwa nje ktk uongozi alijiunda chama au kujiunga na chama kingine ndivyo demokrasia ilivyoanza hata ktk nchi zilizokwisha endelea. Kwa hiyo Kama Chadema wameacha baadhi ya majimbo kuwasubiri hao watakao ondoka CCM, hiyo ni strategy yao ya Ushindi ambayo pengine will work for them.

Lakini hatuwezi kuziba kilaka hiki ati wakishindwa CCM wanaweza kuwa wagombea Binafsi hali kitendo hiki hakiwezi kubadilisha nia na dhamira ya mhusika..Kama Mpendazoe ni opportunist na hafai basi hafai hata kuwa Mgombea binafsi. Kukubali mgombea binafsi pasipo itikadi ni kuwaongezea odds zaidi hawa watu kushika madaraka hata kama wameshindwa huko walikotoka..

Maadam wananchi ndio wanachagua viongozi wao la muhimu ni kuboresha Utaratibu huu. yaliyotokea ktk kura za maoni za CCM na vyama vinginevyo iwe ni somo la kujifunza na kufanya marekebisho ktk kila hatua ya kuboresha demokrasia nchini hatua kwa hatua.
 
Learning is a process and when I was a kid somebody mentioned to me about learning curve!!! Watanzania tuko kwenye njia hiyo. Tunaendelea kujifunza. Naamini mbele ya safari people will be more cautious about rules and regulations we are setting.
Mfano mmojawapo ni huu wa mgombea binafsi na mwingine ni ule wa sheria ya rushwa wakati wa uchaguzi. Athari zake zimeanza kunusa mpaka viatu vya waheshimiwa. What do u expect? Next time they will think twice before agreeing to pass anything.
 
Back
Top Bottom