Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Pamoja na mambo yote ambayo husemwa kuhusu wapinzani lakini ukweli ni kuwa nchi yetu imetekeleza na inaendelea kutekeleza sera zilizobuniwa na wana CCM na sheria zilizopitishwa na bunge la CCM na marais wa CCM. Miaka nenda rudi mafanikio yote ambayo tunayaona katika sekta mbalimbali ni mazao ya CCM na serikali yake na kinyume chake pia ni kweli - kwamba madudu yote tunayoyasikia na kuyaona ni mazao ya CCM hiyo hiyo.
Haiwezekani hata kwa mbali kuilaumu CHADEMA kwa matatizo ya sekta ya afya, kilimo, miundo mbinu n.k Haiwezekani na kwa kweli haiingii akilini kabisa kuilaumu CDM, CUF au chama kingine chochote kwa matatizo mbalimbali tunayoyana nchini - yawe ya hali, utu, nafasi n.k YOte haya yametokeana na yanaendelea kutokea chini ya CCM chama ambacho kimeshikilia Bunge na Urais kwa miaka 50!
Kama hili ni kweli - na hakuna namna ya kuonesha kuwa siyo - wale ambao waliichagua CCM mwaka 2010 na ambao wanaendelea kuichagua CCM huku wakiona yote haya huwa wanajisikiaje? Hivi wanaweza kulalamika wakiambiwa kuwa serikali haina fedha, au wakiona madudu mbalimbali? Hivi wenzetu hawa huko waliko yawezekana kabisa wanaamini kuwa labda huko mbele ya safari atakuja mwana CCM mwingine kutengeneza kilichoharibiwa na CCM? Kweli ndugu zetu hawa wapendwa huko waliko wanaweza kuamini kabisa kuwa yupo mwana CCM ambaye anaweza kuja na kufanya tofauti na kilichofanywa na wana CCM wenzake kwa miaka hamsini ijayo?
Kweli kabisa ndugu zetu hawa bado wanaamini na kuombea kuwa uongozi ujao uwe wa CCM? Ni kitu gani kinawapa matumaini hivi wakati wana historia ya miaka hamsini nyuma yao? Sisemi kwamba wana CCM wote ni wabaya au kwamba hawafai lakini bahati nzuri sana tunayo rekodi; angalia wanavyozungumza Bungeni, wanavyoonekana kabisa kuwa wako kwa mujibu wa ibara ya 15.1 (kama siyo ya 14.1) ya Katiba yao kwa kweli.
Sasa huko waliko wanavyoona yote yanayotokea nchini huwa wanafikiria nini kwamba yawezekana "shetani ameingilia chama" au kuwa ni "bahati mbaya" tu?
Haiwezekani hata kwa mbali kuilaumu CHADEMA kwa matatizo ya sekta ya afya, kilimo, miundo mbinu n.k Haiwezekani na kwa kweli haiingii akilini kabisa kuilaumu CDM, CUF au chama kingine chochote kwa matatizo mbalimbali tunayoyana nchini - yawe ya hali, utu, nafasi n.k YOte haya yametokeana na yanaendelea kutokea chini ya CCM chama ambacho kimeshikilia Bunge na Urais kwa miaka 50!
Kama hili ni kweli - na hakuna namna ya kuonesha kuwa siyo - wale ambao waliichagua CCM mwaka 2010 na ambao wanaendelea kuichagua CCM huku wakiona yote haya huwa wanajisikiaje? Hivi wanaweza kulalamika wakiambiwa kuwa serikali haina fedha, au wakiona madudu mbalimbali? Hivi wenzetu hawa huko waliko yawezekana kabisa wanaamini kuwa labda huko mbele ya safari atakuja mwana CCM mwingine kutengeneza kilichoharibiwa na CCM? Kweli ndugu zetu hawa wapendwa huko waliko wanaweza kuamini kabisa kuwa yupo mwana CCM ambaye anaweza kuja na kufanya tofauti na kilichofanywa na wana CCM wenzake kwa miaka hamsini ijayo?
Kweli kabisa ndugu zetu hawa bado wanaamini na kuombea kuwa uongozi ujao uwe wa CCM? Ni kitu gani kinawapa matumaini hivi wakati wana historia ya miaka hamsini nyuma yao? Sisemi kwamba wana CCM wote ni wabaya au kwamba hawafai lakini bahati nzuri sana tunayo rekodi; angalia wanavyozungumza Bungeni, wanavyoonekana kabisa kuwa wako kwa mujibu wa ibara ya 15.1 (kama siyo ya 14.1) ya Katiba yao kwa kweli.
Sasa huko waliko wanavyoona yote yanayotokea nchini huwa wanafikiria nini kwamba yawezekana "shetani ameingilia chama" au kuwa ni "bahati mbaya" tu?