Walimu watangaza mgomo nchi nzima

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,883
6,883
CHAMA cha Walimu Tanzania (CWT) kimeipa serikali mwezi mmoja kuanzia jana, kuwalipa Sh13 bilioni wanazodai walimu vinginevyo itatangaza mgogoro utakaosababisha walimu kugoma nchi nzima.Hatua hiyo inatokana na kikao cha dharura cha baraza la taifa la CWT, kilichofanyika wiki hii mkoani Morogoro ambacho kilijadili matatizo ya walimu. Rais wa CWT, Gratian Mkoba akizungumza na wanahabari jana jijini Dar es Salaam, alisema fedha hizo ni madeni yanatokana na malimbikizo ya mishahara na madai mengine.“Miongoni mwa matatizo makubwa yaliyojadiliwa ni malimbikizo ya madeni ya walimu yanayozidi kuongezeka siku hadi siku,” alisema Mkoba.

Mkoba alisema madai mengine ni ya walimu waliopandishwa madaraja lakini hawajarekebishiwa mishahara yao kuanzia tarehe ya kupandishwa.Madai mengine alisema yanawahusu walimu waliopandishwa madaraja na kurekebishiwa mishahara yao lakini hawajalipwa fedha za malimbikizo yao kuanzia siku walipopandishwa. Aliongeza kuwa madai mengine wanayodai ni ya walimu ambao mishahara yao haikutolewa kwa wakati na hivyo kuwa na malimbikizo ya mishahara ambayo haijatolewa kipindi cha nyuma. “Kama nilivyotaja matatizo hayo ya walimu, kama hayatakuwa yamepatiwa ufumbuzi ifikapo Julai 31 mwaka huu, CWT kitatangaza mgogoro dhidi ya serikali kwa mujibu wa sheria za nchi,” alisema Mkoba.

Ikiwa walimu watafikia uamuzi wa kugoma, upo uwzekano mkubwa wa kuathiri mitihani ya taifa ya darasa la saba ambao hufanyika kati ya mwezi Agosti na Septemba, na ule wa kidato cha nne ambao hufanyika kati ya mwezi Septemba na Oktoba kila mwaka.
Walimu ndio wasimamizi wakuu wa mitahi hiyo ya kitaifa ambayo kwa darasa la saba hutumika kupatikana kwa wananfunzi wa kuingia kidato cha kwanza, wakati ule wa kidato cha nne hutumika kupata wananfunzi wa kujiunga na kidato cha tano.

Matatizo mengine
Aidha Mkoba alisema tatizo jingine ambalo linakikabili chama hicho ni baadhi ya walimu kutopandishwa madaraja licha ya kustahili kama miongozo inavyosema. “ Hivi sasa lipo tatizo kubwa la walimu walioajiriwa mwaka 2007 au kabla yake ambao hawana matatizo ya kiutumishi lakini hadi sasa hawajapandishwa madaraja, ” alisema Mkoba. Aidha, Mkoba alisema sababu nyingine iliyosababisha kufikia aumuzi huo ni kutokana na waraka wenye kumbukumbu namba A/AC44/45/01/84 wa Desemba 2009 ambao unawashusha walimu vyeo.“Walimu hawa baada ya kumaliza masomo ya shahada ya kwanza, waraka huo unawataka kuanza kazi kwa vyeo vya daraja la D wakati walikwishalipitia kabla hawajaenda vyuoni,” alisema Mkoba.

Mkoba alisema walimu wengi walioathirika na waraka huo ni wale ambao kimuundo walikuwa walimu au maafisa elimu wasaidizi ambao wamefanya kazi muda mrefu. “Tunaona kwamba haki ya walimu inazidi kupuuzwa siku hadi siku licha ya mchango wao mkubwa wanaoutoa katika jamii, sasa tunaona umefika wakati wa kuchukua hatua kama serikali itaendelea kupuuzwa,” alisema Mkoba Serikali ya awamu ya nne imekuwa ikijikuta ikiingia kwenye mgogoro na walimu mara kwa mara kwa kile kinachoelezwa kuwa serikali inapuuza sekta hiyo. Mara kadhaa serikali imechukua hatua za kuwalipa walimu malimbikizo lakini inaishia kueleza kwamba baadhi ya madai ni ya udanganyifu jambo ambalo bado limekuwa likiendelea kujenga uhasama baina yao. Wakati wakilipwa malimbikizo yao miaka miwili iliyopita, baadhi ya walimu walilalamika kwamba walikuta viwango vya malimbikizo yao vikiwa vimepunguzwa na kulazimishwa kusaini ili wachukue kiwango walichandikiwa.

Gazeti hili liliwahi kumnukuu Mkoba mwaka 2009 akilalamika kwaba fedha ambazo zilitolewa kwa ajili ya kulipa madai ya walimu zilikuwa Sh32 bilioni, lakini hazikutumika zote na badala yake zilipindishwa na kulipwa tofauti na madai halisi ya walimu. Alifafanua kuwa Sh18 bilioni zilizotakiwa kutolewa kwa ajili ya malipo ya walimu wa sekondari, hazikutolewa kabisa.“Kutokana na hali hiyo, uvumilivu wa walimu walio chini ya katibu mkuu umekwisha," alisema wakati akisisitiza walimu kuchukua hatua ya kugoma. Alielezea madai ya wakati huo 2009 kuwa licha ya baadhi ya walimu kulipwa na kupewa barua za kupandishwa madaraja, kulipwa malimbikizo ya mishahara na madeni mengine, mpango huo kwa walimu wa sekondari haukwenda vizuri kutokana na mishahara mingi kuwa haijarekebishwa na malimbikizo yake bado yalikuwa hayajalipwa.

CWT na serikali
Tamko la kusudio la walimu kuchukua hatua dhidi ya kutolipwa haki zao na Serikali limekuja baada ya kuwepo kwa kimya cha muda mrefu kuhusu madai yao hayo tangu mwishoni mwa mwaka 2009.Tishio la kuwemo mgomo mkubwa wa walimu lilitolewa maraya mwisho Novemba 2009, mwaka ambao uligubikwa na vita ya maneno baina ya CWT na serikali, huku kukiwa na matishio mengi ya walimu kugoma. Kadhalika Oktoba 2008 kulikuwa na tishio la walimu kugoma kutokana na kuwepo kwa matatizo ya muda mrefu ya walimu, lakini mgomo huo ulizimwa na taarifa ya aliyekuwa Waziri wa Elimu, Profesa Jumanne Maghembe ambaye alieleza jinsi Serikali ilivyokuwa ikishughulikia matatizo hayo.

Mwananchi
 
Kila kona ya nchi ni malalamiko tu, hii serikali inafanya shughuli kwa masilahi ya nani?
 
Hawa walimu wachovu sana. Hawana maana, maneno mengi, kazi kidogo. Fanyeni uamuzi unaoeleweka. Kama ni kugoma gomeni mpate haki zenu. La sivyo; fanyeni kazi kwa bidii kwa maana ualimu ni wito. Kuna baadhi ya walimu ni waoga kweli kudai haki yao. Lakini wa kwanza kukinga mikono. Haki hupatikana kwa ncha ya upanga; haiji hivi hivi.

My take: Walimu wote tafuteni zenu hata kwa ncha ya upanga. Kama hamuwezi chapeni kazi kwa bidii, na Mungu atawalipa.
 
Mimi nashangaa sana, kila mara walimu wanatangaza mgomo, utekelezaji wa mgomo zero, hebu amueni sasa kuchezea digital number either 0 or 1. Siyo nusu nusu, mnatuchefua sana. Inawezekana viongozi wamefanya dili.
 
Hawa walimu wachovu sana. Hawana maana, maneno mengi, kazi kidogo. Fanyeni uamuzi unaoeleweka. Kama ni kugoma gomeni mpate haki zenu. La sivyo; fanyeni kazi kwa bidii kwa maana ualimu ni wito. Kuna baadhi ya walimu ni waoga kweli kudai haki yao. Lakini wa kwanza kukinga mikono. Haki hupatikana kwa ncha ya upanga; haiji hivi hivi.My take: Walimu wote tafuteni zenu hata kwa ncha ya upanga. Kama hamuwezi chapeni kazi kwa bidii, na Mungu atawalipa.
Naunga mkono ushauri wako 100%!
 
wanatangaza mgomo lakini hawagomi hawa wenzetu,
ni kama mme wa salma, ahadi kibao lakini no utekelezaji
 
Mkoba na walimu kwa ujumla vijana ndio tumeingia kwenye career hii hivyo hatutaki danganya toto sisi tumegraduate toka vyuo vikuu tunataka tuludishe heshima ya mwalimu
 
Mkuu Pota. Nimeipenda avatar yako na kauli yako ya kama mume wa salama kondo...... (salma). Siyo siri. Hawa jamaa wa CWT wanaudhi kweli. Wapuuzi wakubwa. Vitisho vingi lkn wapi masikini ya Mungu. Aibu kubwa kwa walimu. Ushauri wa Gobret ni wa mbolea. Fanyeni mgomo mpate haki au kama hamuwezi basi fanyeni kazi zenu kwa bidii. ipo siku Mungu stasikia kilio chenu. Amini Mungu si Athumani
 
ni kweli wanapaswa wawe serious. mara mbili tatu wanatangaza azma ya kufanya mgomo kushinikiza jambo mara unakuta kimya.imekuwa janja tu sasa ya kutishia nyau. hatuwaelewi, mwisho tutakuwa hatuwaamini kabisa kabisa! haya mambo yanahitaji uamuzi firm. si kuwa unatishia tishia tu mara kwa mara
 
Hivi mshahara wa mwalimu ni sh ngapi? Wameridhika nao? Maana wabunge hawaridhiki na posho!

Ushauri kwa wote tutakao mabadiliko, in case wakigoma na sisi tuingilie hapo hapo (tahrir), kwani hata kama sisi si walimu, lakini ni wazazi wa wanafunzi!

Muda wa action umefika, uoga ni ugonjwa wa watanzania wengi si walimu tu!
 
walimu kwa mikwala bana

hivi hawaoni wenzao wa kenya? wakisema tunagoma wanagoma kweli

lakini walimu wetu hawa wa bongo wao huweka mikwala mbele,fanyeni kweli,tupo nyuma yenu
 
Wanacheleweshewa stahiki zao na kulipwa mishahara midogo sababu serikali inataka wawe walimu milele kwan ikiwalipa sana watakuwa wafanya biashara na kuacha ualimu! VYP WASIRA NA SERIKALI YAKO CHADEMA ITAKUWA IMECHOCHEA TENA NINI?!
 
Walimu jamani mbona kila siku mnatishia nyau tuu, sioni actions zozote za maana aaaagh mnaniudhiii
 
Hawa walimu wachovu sana. Hawana maana, maneno mengi, kazi kidogo. Fanyeni uamuzi unaoeleweka. Kama ni kugoma gomeni mpate haki zenu. La sivyo; fanyeni kazi kwa bidii kwa maana ualimu ni wito. Kuna baadhi ya walimu ni waoga kweli kudai haki yao. Lakini wa kwanza kukinga mikono. Haki hupatikana kwa ncha ya upanga; haiji hivi hivi.My take: Walimu wote tafuteni zenu hata kwa ncha ya upanga. Kama hamuwezi chapeni kazi kwa bidii, na Mungu atawalipa.
Waalimu wengi wameingia kwenye taaluma ya ualimu baada ya kukosa sifa za kuingia kwenye fani nyingine. Aidha pia kuna kundi ambalo linatumia vyeti fake au vya ndugu zao. So bado wana ile mentality ya kuona serikali inawapa favour.
 
kwanza ualimu si wito ni ajira na proffesion, na sasa hivi ndugu zangu haturudi nyuma wasipotulipa std 7 na form 4 hawatafanya mitihani tatizo lililokuwepo hadi migomo haifanikiwi ilikuwa ni ubinafsi wa viongozi wa CWT, wakuu wa shule na maafisa elimu wao pia wamechangia sana kwa kuwagawanya walimu wa msingi na sekondari pamoja na kuwatisha walimu wasiojua haki zao.
Kwa nini nina uhakika mgomo utafanikiwa mwaka huu: kwa miaka hii miwili 2010/11 kumekuwa na mabadiliko sana walimu vijana wenye sifa na elimu wameongezeka sana mwaka huu almost 5000 ya walimu kutoka vyo vikuu wameajiriwa na wameleta new challenge mashuleni.
kutokana na kashkash za walimu vijana hasa ajira mpya za mwezi wa 2 walimu wengine wameona jinsi hawa vijana walivyoungana na kudai stahili zao bila woga asilimia 60 ya stahili hizo zililipwa na wengine sasa wamejua bila kuungana hakuna haki na haki hailetwi bali inadaiwa
Pia ktk sehemu nyingi walimu wamekuwa wakiwapasha ukweli viongozi wa CWT na kuwaita wasaliti na kumekuwa na tishio la walimu kutaka kukataa kuchangiia michango ya CWT. Huku mambo yamechange na kuzingatia walimu wengi tuna experience ya migomo toka vyuoni lazima huu ufanikiwe la sivyo mtasikia mapinduzi makubwa sana CWT tukimaliza la madai tunaamsha la kupandishwa mishahara. Anyway passive mgomo mbona uko tangia 2009 na impact yake inaonekana ktk matokeo yani morali iko chini saana. Walimu this time tutaonyesha njia. Kuingia kwa wingi kwa vijana ktk profession ya ualimu ndo ukombozi wetu
 
kwa huu mgomo tuko tayari kuwachapa bakora viongozi wa cwt, wakuu wa shule na walimu ''waoga'' since wengi wetu tumequalify na hatutumii vyeti vya marehemu hatuogopi na bado tunataka board ya walimu ka TLS kwa wanasheria, nbaa kwa wahasibu ili kuweka vigezo na kulinda profesiion yetu tuwe sawa na magraduate wengine wa fani zingine. Serikali iwaulize maafsa elimu mishemishe za walimu wasomi vijana watawaambia na bado madarasani tunawaeleza wanafunzi ubaya wa ccm na wengi wa mastdent wetu 2015 watavote
 
Back
Top Bottom