Walimu Wapya Waandamana Manispaa Arusha; Polisi Wawazingira

Albert Msando

JF-Expert Member
Nov 2, 2010
1,019
171
Walimu wapya leo hii wameandamana hadi ofisi za Manispaa Arusha kudai malipo yao. Taarifa zilizopo ni kwamba malipo hayo yamechelewa kulipwa kwa sababu Serikali kuu haina fedha hivyo ikaiomba Halmashauri ya Manispaa Arusha iwalipe. Kutokana na Halmashauri ya Manispaa kutokuwa na fedha ikaamua kuwalipa nusu ya malipo yao jambo ambalo walimu hao wamelipinga.

Huu ni uzembe na unyanyasaji. Hizi kelele za serikali kukuza elimu ni siasa. Huwezi ukawa na matokeo mabaya ya mitihani halafu bado unaendelea kunyanyasa walimu!

Malipo ya Dowans ni haki kulipwa haraka lakini ya walimu masikini ambao wanajitolea jasho na damu kufundisha watoto masikini wa kitanzania hawana haki ya kulipwa mapema!

Wanakula nini? Wanalala wapi walimu hawa? Wanafikaje kwenye vituo vyao vya kazi?

Haya sio mambo ya kuvumiliwa hata kidogo. Walimu wasiachwe pekee yao kama yatima! Wanaharakati wawasimamie haki zao, vyama vya siasa viwapiganie!
 
Mh.Diwani, serikali hii ya kishikijali wanayopeana kiawara awara ni vigumu wao kuona na kutambua matatizo yanayoukabili sekta nzima ya elimu.Ifike mahala sasa watz tuige ya Tunisia na Misri tuingie mitaani mpaka kieleweke.
 
acha tu hata sisi huku shinyanga manispaa hatujalipwa eti hela hazijatoka hazina na eti halmashauri haina fungu tumeahidiwa kesho na sisi kesho tusipopewa kesho hela zote mtaskia tu bifu aisee tunaishi kwa shida kwa wasamaria wema na hatujaanza kufundisha wakat shule hazina walimu hadi tulipwe kama hawana hela walituajiri ya nini? Na kutuwaisha vituon wengine tunatoka mbali jaman wanaharakati tusaidieni coz CWT hawana msaada tunaombeen plz coz tunaadhirika na tuko ktk nchi yetu
 
Hiyo ndo ghrama ya kuchakachua kura na kufanya mikutano ya kampeni kama sherehe za kufuru za wafalme. Na ile sheria ya gharama za uchaguzi vipi..... haitekelezeki au ilikuwa CRAAAAAP?
 
mbona land cruiser V8 zinakula mitaa full kiyoyozi mpka jumamosi na jumapili?

hizo hela wanatoa wapi washindwe za kulipa walimu? mshahara wenyewe wa mwalimu laki tatu unafika?:angry:
 
mbona land cruiser V8 zinakula mitaa full kiyoyozi mpka jumamosi na jumapili?

hizo hela wanatoa wapi washindwe za kulipa walimu? mshahara wenyewe wa mwalimu laki tatu unafika?:angry:

inashangaza sana!huu ni upumbavu mkubwa kabisa,si walikuwa wanajua kuwa walipaswa kuajiri watumishi wapya,sasa kwa nini hawakutenga fedha kuwezesha hili?serikali kuu haina fedha,mbona wamenunua ma V8,mbona wanaharakisha malipo ya dowans?hivi hivyo ndo vipaumbele vya taifa hili!Safari za nje kila kukicha halafu...aaargh!
 
CCM wameiharibu Tanzania beyond weird imaginations! Sijawahi ona Serikali dhaifu, katili, kipofu kama hii ya Kikwete. Ole wao wanaodhani ni suala la udini! Walimu ni watumishi wa umma, mazingira yao ya kazi si mazuri na wengi wao vipato ni vidogo sana....sasa Serikali (maana ya Hazina) waseme hela za walipa kodi ziko wapi mpaka kadhia hii ya walimu tuisikie huku.

Ni wazi si salama kusubiri hadi 2015, hapa katikati lazima kieleweke na kuwepo mabadiliko ya uongozi Tz.
 
tatizo la walimu ni kuwa hapa mnapiga kelele ila mlisaidia sana kwenye uchakachuaji wa kura. Na kama hamkushiriki 2015 watawahonga msaidie kuchakachua tena. VUMILIENI TU!
 
Ndio maana matokeo ya F4 Zero inaongaza kwa wingi; kama mwalimu hana hela ya kula, hana uhakika na mahali pa kulala
anawezaje kuconcetrate kwenye kufundisha ukizingatia kwa utaratibu wa Serikali mtu huyo hajaingia kwenye payroll kwa sababu ni ajira mpya
na hata pata mshara mpaka baada ya miezi 3-4.
Sina uhakika kama walimu wanaposho yoyote. Tukishirikiana pamoja tunaweza kuifanya Tanzania kuwa nchi yetu.
 
Back
Top Bottom