Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 233
Wadau, nimeipata stori hii katika Tanzania Daima ya leo uk. wa 3:
Ujanja wa CCM wagundulika
N Mwandishi wetu, Dodoma
MBINU chafu za Chama cha Mapinduzi (CCM), zinazotumika katika kukusanya na kujaza watu kwenye mikutano ya mgombea urais wa chama hicho, zimegundulika baada ya baadhi ya walimu wa shule za msingi mjini Dodoma kutoboa siri.
Ilibainishwa jana mjini Dodoma, kuwa agizo limetolewa kwa walimu wote walioko kwenye shule zilizoko kwenye mji huo, kuhudhuria kampeni za mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kesho; huku onyo likitolewa kwa watakaoshindwa kuhudhuria kuwa watawajibishwa.
Kwa mujibu wa baadhi ya walimu waliozungumza na Tanzania Daima, walimu wakuu wa shule walipokea ujumbe kutoka kwa waratibu wa elimu wa kuwataka watoe matangazo kwa walimu wao kuhudhuria mkutano huo bila kukosa.
Walimu hao, walisema baada ya kupewa tangazo na walimu wao wakuu walihoji na kuambiwa kuwa ni agizo kutoka kwa waratibu wa elimu.
Mbali ya walimu, agizo hilo limewalenga wanafunzi wa darasa la tano na la sita kwa baadhi ya shule kutokana na wanafunzi wa darasa la saba kuhitimu shule wiki chache zilizopita.
Baada ya kupata habari hizo, Tanzania Daima ilitembelea baadhi ya shule na kuzungumza na walimu na baadhi ya wanafunzi ambao walikiri kuwepo kwa hali hiyo, huku wengine wakidai hawajaelewa wanakwenda kufanya nini kwenye kampeni hizo.
Kwa upande wa wanafunzi waliozungumza na Tanzania Daima katika shule za Makole, Medeli na Nkuhungu, walisema wametangaziwa na walimu kuwa wafike nje ya Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma majira ya saa 8 siku ya Jumapili bila kukosa.
Ujanja wa CCM wagundulika
N Mwandishi wetu, Dodoma
MBINU chafu za Chama cha Mapinduzi (CCM), zinazotumika katika kukusanya na kujaza watu kwenye mikutano ya mgombea urais wa chama hicho, zimegundulika baada ya baadhi ya walimu wa shule za msingi mjini Dodoma kutoboa siri.
Ilibainishwa jana mjini Dodoma, kuwa agizo limetolewa kwa walimu wote walioko kwenye shule zilizoko kwenye mji huo, kuhudhuria kampeni za mgombea urais wa CCM, Jakaya Kikwete, kesho; huku onyo likitolewa kwa watakaoshindwa kuhudhuria kuwa watawajibishwa.
Kwa mujibu wa baadhi ya walimu waliozungumza na Tanzania Daima, walimu wakuu wa shule walipokea ujumbe kutoka kwa waratibu wa elimu wa kuwataka watoe matangazo kwa walimu wao kuhudhuria mkutano huo bila kukosa.
Walimu hao, walisema baada ya kupewa tangazo na walimu wao wakuu walihoji na kuambiwa kuwa ni agizo kutoka kwa waratibu wa elimu.
Mbali ya walimu, agizo hilo limewalenga wanafunzi wa darasa la tano na la sita kwa baadhi ya shule kutokana na wanafunzi wa darasa la saba kuhitimu shule wiki chache zilizopita.
Baada ya kupata habari hizo, Tanzania Daima ilitembelea baadhi ya shule na kuzungumza na walimu na baadhi ya wanafunzi ambao walikiri kuwepo kwa hali hiyo, huku wengine wakidai hawajaelewa wanakwenda kufanya nini kwenye kampeni hizo.
Kwa upande wa wanafunzi waliozungumza na Tanzania Daima katika shule za Makole, Medeli na Nkuhungu, walisema wametangaziwa na walimu kuwa wafike nje ya Uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma majira ya saa 8 siku ya Jumapili bila kukosa.