Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,144
Mwalimu Alini Brito kushoto na mwalimu Cindy Mauro kulia
Walimu wawili wanawake wa nchini Marekani wamesimamishwa kazi baada ya kufumaniwa wakiwa uchi wa mnyama wakisagana darasani.
Mfanya usafi wa shule hiyo alimfumania mwalimu mwanamke wa somo la kifaransa Cindy Mauro mwenye umri wa miaka 33 na mwalimu mwingine mwanamke wa somo la Kihispania Alini Brito mwenye umri wa miaka 29, wakiwa uchi wakisagana ndani ya darasa moja la shule ya sekondari ya James Madison High School iliyopo Brooklyn, New York nchini Marekani.
Kwa mujibu wa gazeti la New York Daily News, walimu hao walikuwa wakipeana raha huku wanafunzi wakishuhudia shoo hiyo ya kikubwa kupitia darasa la pembeni yake.
Walimu hao wamesimamishwa kazi huku uchunguzi zaidi wa tukio hilo ukiendelea.
Tukio hilo lililotokea tarehe 20 mwezi uliopita, limewafanya wanafunzi waanzishe makundi kwenye Facebook wakiwazungumzia walimu wao.
"Tunatamani tungekuwa tumeweka kamera kwenye madarasa yetu kabla ya tukio lile", alisema mmoja wa wanafunzi ambaye hakutajwa jina lake katika kundi la Facebook lenye wanachama 500.
Mwalimu mkuu wa shule hiyo alikataa kusema chochote lakini mume wa mwalimu Brito alielezea kustushwa na tukio hilo.
Walimu hao walikuwa ni maarufu sana shuleni hapo kutokana na vibwanga vyao.
Mwalimu Mauro alikuwa ni mcheshi na aliyependa kuvaa nguo kama msichana mdogo akionyesha maumbile yake.
"Mwalimu Mauro alikuwa akivaa sketi fupi au jeans fupi na vitopu vinavyoishia kitovuni, alikuwa ni mrembo kweli", alisema mwanafunzi Eddie Ramirez mwenye umri wa miaka 18.
Mwanafunzi huyo alisema kuwa uvumi ulisambaa kwa kasi kuhusiana na mahusiano ya walimu hao lakini walimu wengine walijaribu kulizima soo hilo lisibumburuke.
Msemaji wa kitengo cha elimu, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na amesema kuwa walimu wote wawili wamesimamishwa kazi wakati uchunguzi ukiendelea.