mlaizer
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 233
- 41
TANZANIA imeanza kutekeleza mpango wa kuajiri maelfu ya walimu wa masomo ya Sayansi na Hisabati kutoka nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki ikiwa ni njia ya kukabiliana na upungufu wa walimu 85,000.
Akizungumza jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa alisema
mchakato wa kuajiri walimu kutoka nchi wanachama wa jumuiya hiyo umeanza na
utakuwa endelevu mpaka hapo watakapojitosheleza.
Kwa kuwa lengo letu ni kukuza masomo ya Sayansi, tumeanza na tunaendelea kuajiri
katika nchi nne za jumuiya, sitaweza kukupa takwimu kwa sasa maana kila watu wanaajiri
maeneo yao, na naweza kukuambia leo hivi kumbe kesho imebadilika, labda mpaka
baadaye, alisema.
Mwaka jana, nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliipa kipaumbele suala la
elimu kama moja ya sekta ambayo itafaidika na soko la ajira chini ya mpango wa Soko la
Pamoja.
Awali, Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Abdallah Abdullah alisema jijini Arusha hivi karibuni kuwa, Baraza la Mawaziri la jumuiya hiyo limetoa baraka kwa Tanzania kuajiri walimu mwaka huu kwa lengo la kuziba pengo.
Ilielezwa kwamba, Serikali ina mpango wa kuajiri walimu wa Hisabati na Sayansi kwa
shule za sekondari wapatao 3,200 kutoka Kenya na Uganda.
Tanzania inahitaji karibu walimu 31, 000 wapya kwa ajili ya shule za msingi na sekondari ndani ya miaka miwili ya kutoa elimu bora kwa ongezeko la wanafunzi waliojiunga kwa miongo miwili iliyopita.
SOURCE:HABARILEO
MY TAKE:wale walimu wetu tuliokuwa tunawandaa tangu 2005 kutoka DUCE,MKWAWA,UDOM, n.k kama mkakati wa serikali kuondoa tatizo la walimu nchini wako wapi?Serikali haioni kama inajichanganya kimaamuzi?Tanzania kuna walimu wengi lakini walimu hao hawajitokezi kufundisha kutokana na maslahi duni na miundombinu mibovu ktk sehemu za kufanyia kazi.serikali na walimu wana migogoro ambayo mpaka sasa hayajatatuliwa,je kuwaajiri walimu kutoka nje inaweza ikawa ni suluhisho la matatizo?serikali haiwezi kuona kama wanaweza kuongeza mgogoro mwingine kwa walimu wa nchi za jirani(afrika mashariki)ikiwa tu imeshindwa kuwatimizia walimu wazawa?
NAWASILISHA
Akizungumza jana, Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Shukuru Kawambwa alisema
mchakato wa kuajiri walimu kutoka nchi wanachama wa jumuiya hiyo umeanza na
utakuwa endelevu mpaka hapo watakapojitosheleza.
Kwa kuwa lengo letu ni kukuza masomo ya Sayansi, tumeanza na tunaendelea kuajiri
katika nchi nne za jumuiya, sitaweza kukupa takwimu kwa sasa maana kila watu wanaajiri
maeneo yao, na naweza kukuambia leo hivi kumbe kesho imebadilika, labda mpaka
baadaye, alisema.
Mwaka jana, nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki iliipa kipaumbele suala la
elimu kama moja ya sekta ambayo itafaidika na soko la ajira chini ya mpango wa Soko la
Pamoja.
Awali, Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki Abdallah Abdullah alisema jijini Arusha hivi karibuni kuwa, Baraza la Mawaziri la jumuiya hiyo limetoa baraka kwa Tanzania kuajiri walimu mwaka huu kwa lengo la kuziba pengo.
Ilielezwa kwamba, Serikali ina mpango wa kuajiri walimu wa Hisabati na Sayansi kwa
shule za sekondari wapatao 3,200 kutoka Kenya na Uganda.
Tanzania inahitaji karibu walimu 31, 000 wapya kwa ajili ya shule za msingi na sekondari ndani ya miaka miwili ya kutoa elimu bora kwa ongezeko la wanafunzi waliojiunga kwa miongo miwili iliyopita.
SOURCE:HABARILEO
MY TAKE:wale walimu wetu tuliokuwa tunawandaa tangu 2005 kutoka DUCE,MKWAWA,UDOM, n.k kama mkakati wa serikali kuondoa tatizo la walimu nchini wako wapi?Serikali haioni kama inajichanganya kimaamuzi?Tanzania kuna walimu wengi lakini walimu hao hawajitokezi kufundisha kutokana na maslahi duni na miundombinu mibovu ktk sehemu za kufanyia kazi.serikali na walimu wana migogoro ambayo mpaka sasa hayajatatuliwa,je kuwaajiri walimu kutoka nje inaweza ikawa ni suluhisho la matatizo?serikali haiwezi kuona kama wanaweza kuongeza mgogoro mwingine kwa walimu wa nchi za jirani(afrika mashariki)ikiwa tu imeshindwa kuwatimizia walimu wazawa?
NAWASILISHA