Walichosema CUF - Nyaraka

Source: Habari Leo
Shadrack Sagati
Daily News; Thursday,May 15, 2008 @00:01

Katibu Mkuu wa CCM, Yusuf Makamba


“Mimi nilikataa kwa sababu kuundwa serikali ya kitaifa ni pale tu ambako kuna mgogoro wa siasa, lakini Zanzibar hakuna kitu kama hicho, kujadili suala kama hili wakati kuna serikali ambayo iko madarakani kwa halali ni sawa na uhaini,” alisema Makamba.

Katika watu wanaotia aibu na huruma katika siasa za Tanzania ni huyu Makamba. Sasa angalia hapo juu anasema nini. Kama Zanzibar hakuna mgogoro, kwa nini walikuwa wanakaa kwenye haya mavikao? Hebu tuanze kuwajibisha wanasiasa wetu kwa maneno yao. Kipimo kimojawapo kikubwa sana cha udhaifu wa JK ni kitendo chake cha kumteua Makamba kuwa Katibu Mkuu wa chama chake na sijui itawachukua miaka mingapi CCM kujua kwamba Makamba ni mzigo mzito kwa chama chao. Kwa kweli ilikuwa ni kumuonea sana kumteua Makamba kwenye nafasi hii kwa sababu imefanya hata wale waliokuwa hawajui wajue kiwango cha ununda wake!

Then, CCM wanapenda kutumia maneno loosely tu hivihivi, kila mara wakibanwa wanaibuka na neno uhaini, this is pathetic!
 
Ah Jobo nawe. Kwani anayechagua Rais ni Wabunge (Wawakilishi) au ni wananchi katika ujumla wao.

Ndugu yangu ni vyema ukajua siasa za kileo! Majority votes (kura nyingi) kinaweza kisiwe kigezo kizuri cha kukubalika kwa kiongozi pale ambapo rais huyo anaongozwa maeneo mawili tofauti. Wakati Al Gore aliposhindwa Marekani hakushindwa kwa sababu Wamarekani waliowengi hawakumpa kura, alishindwa kwa sababu hakupata kura nyingi kwenye majimbo mengi. Hivyo hivyo na John Kerry. Sasa kwa upande wa Zanzibar, huyo Hizbula Karume alipata kura Unguja na akala ghalasha Pemba. Seif, kwa upande wake, alipata kura nyingi pande zote za visiwani. Kwa maneno mengine, yeye anakubalika zaidi (in terms of proportionality) kuliko karume. And by the way, bila Wabunge huwezi kutawala, labda uwe utawala wa kijeshi.
 
Marufuku kuwaona

2008-05-15 09:14:57
Na Dunstan Bahai


Jeshi la Polisi nchini, limesema halitawaruhusu ndugu wa watuhumiwa wa `uhaini` waliokamatwa kisiwani Pemba kwenda kuwajulia hali mahala wanakohifadhiwa.

Aidha, jeshi hilo limesema ndugu hao wasiwe na wasiwasi kwani ndugu zao wako salama na wakiumwa wanapatiwa huduma za kimatibabu kama binadamu wengine.

Kauli hiyo ilitolewa na Kamishna wa Polisi wa Zanzibar, Bw. Khamis Mohammed Simba, wakati akizungumza na gazeti hili kwa njia ya simu.

Bw. Simba alikuwa ameombwa aeleze waliko watuhumiwa hao na kama ndugu wanaweza kwenda kuwajulia hali.
 
Katika watu wanaotia aibu na huruma katika siasa za Tanzania ni huyu Makamba. Sasa angalia hapo juu anasema nini. Kama Zanzibar hakuna mgogoro, kwa nini walikuwa wanakaa kwenye haya mavikao? Hebu tuanze kuwajibisha wanasiasa wetu kwa maneno yao. Kipimo kimojawapo kikubwa sana cha udhaifu wa JK ni kitendo chake cha kumteua Makamba kuwa Katibu Mkuu wa chama chake na sijui itawachukua miaka mingapi CCM kujua kwamba Makamba ni mzigo mzito kwa chama chao. Kwa kweli ilikuwa ni kumuonea sana kumteua Makamba kwenye nafasi hii kwa sababu imefanya hata wale waliokuwa hawajui wajue kiwango cha ununda wake!

Then, CCM wanapenda kutumia maneno loosely tu hivihivi, kila mara wakibanwa wanaibuka na neno uhaini, this is pathetic!

Huyu Makamba ni aibu tupu kwa ccm na Kikwete!
 
Akizungumza kwa kujiamini, Jussa, mmoja wa viongozi wenye ushawishi ndani ya CUF, aliwataja Rais mstaafu wa Awamu ya Pili, Ali Hassan Mwinyi na mke wa Rais wa Zanzibar, Shadya Karume, kuwa wana CCM wawili wenye uhusiano ama wa kikazi au kinasaba na chama hicho cha kisultani cha Hizbu.

Jussa ambaye alikuwa akikanusha madai ya kada mkongwe wa CCM aliyepata kuwa msoshalisti kiitikadi, Kingunge Ngombale-Mwiru, aliyeihusisha CUF na U-Hizbu, alisema chama hicho tawala ndicho ambacho kina historia ya kuwa na uhusiano na chama hicho cha kisultani.

Alisema inapofika mahali mtu mzima kama Kingunge akasema uzushi, ni dhahiri chama hicho (CCM) kimefikia mahala pagumu na kimepoteza dira na mwelekeo.

"CCM ndiyo ina sifa zote za mahusiano na Hizbu, na si CUF. Na kwa msingi huo, kama kuna hoja pia ya kurudisha Waarabu, hilo linapaswa kuhofiwa kutoka CCM na si kutoka CUF.

"CUF kiliasisiwa mwaka 1992, na viongozi wake wanne wakuu kutoka Zanzibar ni Seif Sharif Hamad, Ali Haji Pandu, Shaaban Khamis Mloo na Machano Khamis Ali. Wote ni wana-ASP wasio na chembe ya shaka.

"Lakini mawaziri wa Zanzibar wa hivi sasa, yupo ambaye anajulikana kuwa alikuwa mwanachama wa Hizbu. Waziri wa Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi, Mansour Yusuf Himid, ambaye ni ndugu wa mama mmoja na Shadya Karume, mke wa Amani Karume, wote wawili ni wajukuu wa Sheikh Mohammed Salim Jinja, ambaye alikuwa mwasisi wa Hizbu na ambaye wenyewe Hizbu wakimwita '‘Founding Father of Zanzibar Nationalism,"alisema Jussa.

Pia alisema yupo waziri mmoja katika Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka Zanzibar ambaye amekuwa akiandika makala katika magazeti kuipinda CUF, alipata kuwa mwanachama wa Umoja wa Vijana wa Hizbu uliokuwa ukijulikana kama Youth Own Union (YOU).

Ingawa hakumtaja kwa jina, waziri anayetoka Zanzibar ambaye amekuwa akiandika makala kuiponda CUF kupitia magazetini ni Muhammad Seif Khatib, ambaye sasa ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais anayeshughulikia Muungano.

Khatibu kabla ya kuingia serikalini alipata kuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM (zamani UVT) kwa muda mrefu, miaka ya 1980.

Mbali na hao, alisema viongozi wastaafu, kama Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi na Spika mstaafu wa Baraza la Wawakilishi, Mzee Ali Khamis Abdallah, baada ya Uhuru wa Desemba 1963 (miezi kadhaa kabla ya mapinduzi ya Januari 12, 1964) waliteuliwa na serikali ya Hizbu kuwa makatibu wa kwanza (First Secretaries) wa Ofisi za Kibalozi za Zanzibar huko Indonesia na Misri.

"Ni bahati mbaya sana kwamba lugha zinazochochea ubaguzi na kujidai kuwakataa ma-Hizbu zilizotolewa katika Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM hazikukemewa hata na Mwenyekiti wa CCM mwenyewe.

"Ulitumiwa Uhizbu kukataa ufumbuzi wa kudumu wa mpasuko wa kisiasa Zanzibar wakati hao waliokuwa wakiwakataa ma-Hizbu ndio ma-Hizbu wenyewe," alisema Jussa katika kauli inayoweza kuamsha mtazamo mpya wa siasa za Zanzibar siku zijazo.
Mwisho wa kuchamba kwingi ssa CCM wamezidi kutapakaa mivi.
 
sasa ina maana kuwa hizbu au kuhusiana na uhizbu si tatizo tena!

Naona unauliza kama CCM ipo katika upande gani wakati wakiitisha kura ya maoni kuhusiana na muafaka ,Mwanakijiji ukipata nafasi ya kuwahoji hawa vingunge hebu waulize kama wanaunga mkono maamuzi ya kamati mbili au wanapinga ,maana hao wanancho walio wengi huko zanzibar wapo ama CCM au CUF ,bila ya shaka wanachama wao wataunga upande kilipo chama chao ,CCM kipo wapi ?
 
Du nimesoma habari yote... nimesikitishwa kwa sababu heri mungekuwa mumesikia wenyewe... CCM waliyosema na CUF pia waliyosema...

Na kusitikitisha ni kwamba CUF walikiri kukiuka makubaliano ya kuongelea mambo ya muafaka hadharani bila kuwepo makatibu wakuu wote... lakini haikuandikwa... sasa rafiki yangu kama mwanakijiji ndio amepigwa bao hivyoo.... kwa sabubu haikuandikwa...

CUF wamesema walishakubaliana ... quote walizotoa za kuonyesha kukubalina kwa hakika ni dhaifu sana... tena kupita. kiasi...

CCM ofcourse ina mapungufu yake... lakini du CUF...

Nimeona quote ya Maalim Seif ya Kulazimishia Uwaziri Kiongozi... narudia usemi wangu Kwamba Maalim Seif ni hatari sana kwa utulivu wa Zanzibar... rudini tena muone ile quote.

Mkulu Kasheshe, sasa wametamka wao wenyewe kwenye vyombo vya habari kuwa Mwafaka ndiyo basi tena... CCM inajipanga vipi mkuu kuhandle hili sulutisho?!
 
Ni vema CUF wametambua kuwa CCM ina ridhaa halali kabisa ya kuongoza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. ingekuwa ni ajabu na kweli pale ambapo CCM ingeamua kuwasaliti wananchi na kuwapa CUF uongozi katika SMZ.
Kudhihirisha kuwa CCM ni chama makini na cheneye dhamana ya kuongoza SMZ ndiyo maana iliwaambia CUF kwamba CCM haiwezi kubadilisha uongozi wa SMZ hadi hadi ipatikane tena ridhaa ya wananchi kupitia kura za maoni. Kwa vile CUF walijua kuwa hawawezi kupewa ridhaa hiyo na wananchi ndiyo maana walikataa kuitishwa kura ya maoni, habari ndiyo hiyo. Tusibiri 2010.
 
Nami nimemaliza kuisoma hii dosier, Kwa kweli, kwa mara nyingine tena, CUF wameonyesha umakini wao na wamezidi kuanika udhaifu wa CCM. Nimefurahi zaidi pale walipowashughulikia CCM kuhusu madai yao yasiyokwisha ya u-Hizbu. Kumbe at the end of the day, kama ni u-Hizbu, CCM ni Hizbu kuliko Hizbu wenyewe. Lakini kwa jinsi CUF walivyo makini, wametoa hii historia sio kwa lengo la kuwaumbua CCM bali kwa nia ya kuonyesha jinsi ambavyo Zanzibar ni taifa la watu mchanganyiko na kwa vyovyote vile watu wengi sana kule Zanzibar hawawezi kukwepa damu ya mwarabu. Sasa huu ujinga wa CCM wa kuwalaghai watu kwamba mtu hafai kuwa kiongozi kwa sababu tu ana matone ya damu ya warabu itabidi ukome. Natazamia pia wale wajumbe wenzetu hapa JF ambao wamekuwa wakishindilia sana kwamba Salim hafai kuwa Rais wetu kwa kisingizio cha u-Hizbu itabidi wawe wastaarabu watoke hadharani hapahapa watubu, vinginevyo wanyamaze kimya milele katika hili maana inaonekana ama hawajui wanaloliongea au nao ni sehemu ya propaganda za ovyo za CCM!

Hapa kwa kweli ndugu zetu CCM wameshikwa pabaya. Ambacho hawataki kukielewa watu wa CCM ni ukweli kwamba katika ulimwengu wa leo ni vigumu mno kukalia habari. CCM wanatia huruma na kusikitisha zaidi wanapoendelea kumtumia Kingunge awatetee na kuwasemea kwenye mambo controversial kama haya. Yote hii ni kwa sababu wanafikiri watu watakubali tu kwa kuwa anayeongea ni Kingunge wasijue kwamba Kingunge mwenyewe heshima yake katika jamii ilishashuka kuliko hata ya Makamba! Bora wangewatumia Ze Comedy kuliko kumtumia Kingunge.

Hata hivyo, tusisahau hawa mabwana wa CCM wamezoea kuishi kwa ujanjaujanja wa kuwadanganya watanzania basi na mambo yamekuwa yakienda hivyohivyo. Bila ujanjaujanja, ghiliba, uongo, kujigeuzageuza CCM haiwezi ku-survive. Ndio maana sasa katika ulimwengu huu wa leo ambao huwezi ku-survive bila competence in style and substance wenzetu wa CCM inawawia ugumu.

Ngoja tusubiri watasema nini kwenye hii dosier ya CUF lakini kwa mambo yalivyo hawana hoja zaidi ya kuendeleza ujanjaujanja na ghiliba tu
Vintage professor sidhani kama sasa unaweza kuongea madini kama haya tena.... Leo hii umeenda kufanya kazi na chama hicho hicho unachokilaumu kubaka demokrasia ya visiwani.....

Kama una nia njema leo si upo serikalini kwanini basi usishauri haya yote uliopigia kelele ukiwa upinzani CCM wayafanye?? Ulipigia kelele sana pesa za ESCROW je ni lini umeshauri wanaCCM wenzako warudishe zile pesa walizochota BOT?? Ni lini umeshauri CCM iache kubaka demokrasia zanzibar??

If i ask brother.... Do you still have courage to say this again even though you know its the bitter truth??
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Unafiki Mkuu ni kitu kibaya sana watu wanaweka mbele maslahi ya matumbo yao badala ya yale ya Nchi.

Vintage professor sidhani kama sasa unaweza kuongea madini kama haya tena.... Leo hii umeenda kufanya kazi na chama hicho hicho unachokilaumu kubaka demokrasia ya visiwani.....

Kama una nia njema leo si upo serikalini kwanini basi usishauri haya yote uliopigia kelele ukiwa upinzani CCM wayafanye?? Ulipigia kelele sana pesa za ESCROW je ni lini umeshauri wanaCCM wenzako warudishe zile pesa walizochota BOT?? Ni lini umeshauri CCM iache kubaka demokrasia zanzibar??

If i ask brother.... Do you still have courage to say this again even though you know its the bitter truth??
 
Unafiki Mkuu ni kitu kibaya sana watu wanaweka mbele maslahi ya matumbo yao badala ya yale ya Nchi.
Bubu ataka kuongea,hii thread nimeichimbua maalum kwaajili ya prof. Kitila,sijui kama atakuja.
 
Back
Top Bottom