Albedo
JF-Expert Member
- Feb 24, 2008
- 5,559
- 1,452
Ninalo Swali jamani, linalotatiza kichwa changu
Kila lijapo mawazoni,laniongezea wazimu
Nashindwa niseme nini, nabaki ni kama bubu
Wali uliwe kwa mkono, au Kijiko Jamani?
Wa maharage fikiria, wengine wasema mandondo
Upikwe kwa jiko la mkaa, si la gesi hata oven no
Kwa nazi ukachuriziwa, watamanisha kwa Uhondo
Wali uliwe Kwa mikono , au kijiko Jamani?
Ha ha ha Wanajamvi, Naomba Mnisamehe
Nimeyataja Mandondo, Mate yawatirirka
Keyboard zapiga short, kwa Mate yatiririkayo
Wali Uliwe Kawa mikono, au kwa Kijiko Jamani?
Wali uwe wa Kyela, wa Kamsamba hata wa Rukwa
Utiwe nazi hata mafuta, wanukia kwa Maraha
Si kwa Mandondo peke yake, Dagaa nao watia For a
Wali Uliwe kwa Mikono, au kwa Kijiko Jamani
Wengine wauta pilau, wengine sijui biriani
Uwe wa Kempisk hata Royal palm, Mama Cheusi naye anatisha
Mhhh jamani wali mtamu, upikwe na fundi kweli
Wali Uliwe kwa Mikono, au kwa Kijiko Jamani?
Malenga nawachia swali, naombeni jibu haraka
Nashikwa na Kigumumuzi, maana sahani I mezani
Nipeni jibu Haraka, Nianze kuufakamia
Niule wali kwa Mkono, au Kijiko cha nauliza?
Kila lijapo mawazoni,laniongezea wazimu
Nashindwa niseme nini, nabaki ni kama bubu
Wali uliwe kwa mkono, au Kijiko Jamani?
Wa maharage fikiria, wengine wasema mandondo
Upikwe kwa jiko la mkaa, si la gesi hata oven no
Kwa nazi ukachuriziwa, watamanisha kwa Uhondo
Wali uliwe Kwa mikono , au kijiko Jamani?
Ha ha ha Wanajamvi, Naomba Mnisamehe
Nimeyataja Mandondo, Mate yawatirirka
Keyboard zapiga short, kwa Mate yatiririkayo
Wali Uliwe Kawa mikono, au kwa Kijiko Jamani?
Wali uwe wa Kyela, wa Kamsamba hata wa Rukwa
Utiwe nazi hata mafuta, wanukia kwa Maraha
Si kwa Mandondo peke yake, Dagaa nao watia For a
Wali Uliwe kwa Mikono, au kwa Kijiko Jamani
Wengine wauta pilau, wengine sijui biriani
Uwe wa Kempisk hata Royal palm, Mama Cheusi naye anatisha
Mhhh jamani wali mtamu, upikwe na fundi kweli
Wali Uliwe kwa Mikono, au kwa Kijiko Jamani?
Malenga nawachia swali, naombeni jibu haraka
Nashikwa na Kigumumuzi, maana sahani I mezani
Nipeni jibu Haraka, Nianze kuufakamia
Niule wali kwa Mkono, au Kijiko cha nauliza?