Walevi wanaomtuhumu Mh LOWASSA hawaniumzi kichwa

Jumakidogo

R I P
Jul 16, 2009
1,851
417
Nawachukulia wanaomtuhumu mh EL kwa wizi na ufisadi kama wanaigiza COMEDY flani hivi....Siwezi kuamini bila kuona wala kushuhudia. Siwezi kushutumu na kutoa hukumu kwa maneno ya wahuni wa kwenye vijiwe vya wavuta bangi, wacheza kamari na walevi wa dawa za kulevya. Wale waropokao baada ya akili zao kushituliwa na nguvu ya ziada kutokana na moshi wa tumbaku haramu au maji ya nafaka iliyochacha. Siwezi kushikia bango maneno ya wacheza bao na waswahili kwenye vijiwe vya kahawa mitaani. Wala siwezi kuumiza kichwa kwa uzushi na uchafu wa makusudi........VUVUZELA wameshindwa kuthibisha na kuonyesha ushahidi wa uchafu wa Mh EL, Hivi ukimshitaki mwizi mahakami halafu hakimu akataka ulete ushahidi na kithibiti, wewe ukabaki kusema tu, mwizi huyu! Mwizi huyu! Mwizi huyu... Ama kwa hakika hakimu atakuona punguani!! Bado nasubiri jasiri, mwenye ushahidi wa kuniaminisha. Auweke hadharani
 
Mkuu maneno yote ya nini?! mbona unaonekana kuumiza kichwa chako kwa maneno mengi?! WATANZANIA wenye akili mbona tunaelewa mchezo unaoendelea!. EL alithibitisha katika utetezi wake kwamba hakuna alichokifanya ambacho JK hakujua! na alitaka kuchukua hatua lkn JK akamzuia!. Kwa kuwa JK hajawahi kukanusha inaonesha EL alitegewa ili mambo yamuharibikie na awe mbali na kinyang'anyiro cha Uraisi wa 2015!. Unaweza kuona walioshiriki kumsulubu EL wote walipewa zawadi kama vile Uwaziri na ukuu wa Mkoa.!. JK ndiye mbeba dhamana ya RICHMOND! ni hatari kwelikweli kaliingiza Taifa katika deni kubwa! lakini tunarudi pia nyuma ni huyu huyu JK alililingiza Taifa katika Mkataba haramu wa Umeme kwa TAIFA na IPTL.! Kwa maana hiyo ameshiriki kulihujumu taifa kwa kiasi kikubwa kutokana na makosa yake!. Namshaurri EL awe mtulivu, maana tuliopo nyuma yake tupo wengi baada ya kuulewa ukweli!.
 
Sijui kati ya baba na mama nani alitilia nguvu suala la mimi kuzaliwa mtoto wa pili........natamani sana wao au marafiki zao waliokuwepo wanisaidie kutambua hili..........bahati mbaya mimi na wadogo zangu tunaliongelea hili mpaka tunafarakana na wazazi wanatuona wamekaa kimya....wanaojuua ukweli wanatutazama tu sijui wanataka tuuane........

Ninatamani ningekuwa mkazi wa nyumba ya jirani lakini pia sina uhakika kama ningekuwa na furaha.......watoto wa baba mdodgo wao baada ya kugombana sana juu ya mada kama ya kwetu wao wakaishia kuwaua wazazi wao ili wakae na amani......sasa hata chakula tu hawapati tena........

Aaaagh duniani kuna taabu but ndo napajua atleast.......akhera nako kuna moto na pepo

Tafakari....chukua hatua
 
Malalamiko yote hayo ya nini? mmetumwa na nani? na wagombea wa urais 2015? nyie wawili mnataka kutuchagulia Rais?tuliingizwa mkenge na vyombo vya habari mwaka 2005, haturudii makosa. waacheni wananchi wenyewe wachambue pumba na mchele.Kikwete amtegeshee Lowassa kwa maslahi gani? acheni uzushi.
 
Ni kweli na mimi nawaunga mkono huyu mzee hata mimi nilidhani ni mchafu kama ilivyokuwa inaelezwa lakini tumeyasikia yale yaliyo nyuma ya pazia hata kama ni kwa kiasi kidogo.
Jamani let us be fair ni viongozi wangapi waliopo madarakani ambao hawapigi videal ama madeal ya hapa na pale kwa hakika viongozi wote kila mmoja kwa nafasi yake anajaribu kupiga deal kulingana na urefu wa kamba yake.Hivyo basi nikirudi kwenye hii mada mimi pia bado sijashawishiwa kuamini kuwa huyu bwana EL ni mwizi hivyo inavyoelezwa ni kweli ni mfanyabiashara na mwanasiasa pengine kama ilivyo kwa mtendaji wa kata/mbunge/diwani akiwa anafanya pia biashara ya mazao mfano ni mkulima ama mfugaji na akauza mazao ama mifugo yake.
EL amekanusha na kusema JK anafahamu na huyuhuyu raisi alishasema mfano kuwa hawajui DOWANS sasa nani mkweli na nani muongo ina maana EL anaweza kumsingizia JK ilhali waha ni marafiki?haiwezekani!!

huyu jamaa kweli alisetiwa na waliomseti ndo hao wamepewa madaraka ya ukuu wa mikoa na uwaziri kama ni kweli ni wazalendo na walikuwa wanamaanisha ku expose yote mabaya waliyoyaona kuhusu sekta ya umeme ina maana walishindwa kung'amua kuhusu uhusika wa ''JK'' kwenye mkataba wa IPTL? then wakasema eti " kuna taarifa nyingine ambayo hatuisema kama tungeisema mambo yangekuwa mabaya" walikaa kimya kwa faida ya nani?kwa nini wasisema na wahusika wote either wakaomba msamaha ama kujiuzuru!! walikaa kimya na matokeo yake badala ya kuendelea kupambana eti Mh S.6 akastopisha ule mjadala na wala mkakati wa kutekelezaaazimio yaliyo kubaliwa ukafa natural death alafu wanadai eti ni wapambanaji kwa ajili ya nani? walipata feed back kutoka kwa wananchi kuwa wameridhishwa!??? na hatua ? jibi ni hapana!!! huu ulukuwa ni mkakati wao na kweli walifanikiwa baada ya jamaa kujiuzulu hawakuwa na agenda nyingine!!!


HIS PAST IS OVER.......AND WHEN GOD SAYS NO ONE WILL SAY NO AND NOTHING WILL COME BETWEENN!!! HAKUNA USHAHIDI WA KUMTIA HATIANI! kama ni kimemo wangapi wameandika vimemo!!!!!!!!


NINI CHA KUFANYA;

1. Ni ku review miiko ya uongozi

2. Kuinsist uwajibikaji

3. labda kutenganisha biashara na siasa kukwepa conflict of interest
 
Kuna kitu hapa mimi sijakielewa naomba mtoa thread hii unisaidie. Unaposema "walevi wanaomtuhumu......hawakuumizi kichwa" kuna uhusiano gani kati yako na Lowassa?

Yawezekana usielewe swali langu, lkn nachojiuliza ni ktk mazingira yepi mtu uumwe kichwa kwa jambo la kisiasa linalomhusu mtu mwingine! Kwa mfano, sasa hivi mimi niseme kuwa shutuma zinazomkabili fulani zinaninyima usingizi, zininyime usingizi kwa vipi ikiwa mimi si mhusika? Hebu nieleweshe unahusianaje na Lowassa mpk mambo yake yakuumize au yasikuumize kichwa?
 
Kuna kitu hapa mimi sijakielewa naomba mtoa thread hii unisaidie. Unaposema "walevi wanaomtuhumu......hawakuumizi kichwa" kuna uhusiano gani kati yako na Lowassa?

Yawezekana usielewe swali langu, lkn nachojiuliza ni ktk mazingira yepi mtu uumwe kichwa kwa jambo la kisiasa linalomhusu mtu mwingine! Kwa mfano, sasa hivi mimi niseme kuwa shutuma zinazomkabili fulani zinaninyima usingizi, zininyime usingizi kwa vipi ikiwa mimi si mhusika? Hebu nieleweshe unahusianaje na Lowassa mpk mambo yake yakuumize au yasikuumize kichwa?

Wewe unawashwa? Unahitaji kukunwa. Mimi ni shabiki kama wewe ulivyo shabiki wa lile jeshi la bandia.
 
Kwanini tugombane kwa uraisi wa 2015 leo hii ,ni kwa sababu nchi haina raisi,au ni kwa sababu tuna uhakika tutakuwapo ?

Hii inanikumbusha habari ya familia moja iliyofikiria kufuga bata,katika mpango wao huo waliishia kutofuga baada ya kushindana nani atasafisha banda
.

Tunakoelekea ndio huko tusipoangalia, kwani inawezekana kuna watu wasipokuwa maraisi nchi itakufa.
 
Kwanini tugombane kwa uraisi wa 2015 leo hii ,ni kwa sababu nchi haina raisi,au ni kwa sababu tuna uhakika tutakuwapo ?

Hii inanikumbusha habari ya familia moja iliyofikiria kufuga bata,katika mpango wao huo waliishia kutofuga baada ya kushindana nani atasafisha banda
.

Tunakoelekea ndio huko tusipoangalia, kwani inawezekana kuna watu wasipokuwa maraisi nchi itakufa.

Tunajadili katika hali ya kawaida, lakini kuna watu hawaelewi maana yamajadiliano. Haya ni mambo ya kawaida kuzungumza.
 
guys are you still thinking about EL??

Worry not for EL, worry much for CCM.......

read my signature please!!
 
Tunajadili katika hali ya kawaida, lakini kuna watu hawaelewi maana yamajadiliano. Haya ni mambo ya kawaida kuzungumza.
Wewe na Lowasa mnaijua 'ghaibu' ! Hivyo tumwachie Mungu tuone kama aliwaachia kazi yake mkaimu !
 
Back
Top Bottom