Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Nawachukulia wanaomtuhumu mh EL kwa wizi na ufisadi kama wanaigiza COMEDY flani hivi....Siwezi kuamini bila kuona wala kushuhudia. Siwezi kushutumu na kutoa hukumu kwa maneno ya wahuni wa kwenye vijiwe vya wavuta bangi, wacheza kamari na walevi wa dawa za kulevya. Wale waropokao baada ya akili zao kushituliwa na nguvu ya ziada kutokana na moshi wa tumbaku haramu au maji ya nafaka iliyochacha. Siwezi kushikia bango maneno ya wacheza bao na waswahili kwenye vijiwe vya kahawa mitaani. Wala siwezi kuumiza kichwa kwa uzushi na uchafu wa makusudi........VUVUZELA wameshindwa kuthibisha na kuonyesha ushahidi wa uchafu wa Mh EL, Hivi ukimshitaki mwizi mahakami halafu hakimu akataka ulete ushahidi na kithibiti, wewe ukabaki kusema tu, mwizi huyu! Mwizi huyu! Mwizi huyu... Ama kwa hakika hakimu atakuona punguani!! Bado nasubiri jasiri, mwenye ushahidi wa kuniaminisha. Auweke hadharani