Walemavu wataka Masha ajiuzulu

macho_mdiliko

JF-Expert Member
Mar 10, 2008
21,766
39,536
WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Bw. Lawrence Masha ametakiwa kujiuzulu kutokana na kauli anayodaiwa kuitoa hivi karibuni juu ya mauaji ya albino alipohojiwa na Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) kuwa mauaji ya albino ni kitu kidogo.

Wakizungumza jijini jana katika mdahalo wa watu wenye ulemavu, washiriki wa mdahalo huo walisema kutokana na kauli hiyo albino pamoja na walemavu wote nchini walitangaza kutokuwa na imani naye na kumtaka awapishe wengine.

Wadau hao pia walisikitishwa na jinsi Serikali inavyoshindwa kuwalinda albino huku wanyama walioko katika mbuga mbalimbali wakipatiwa ulinzi wa kutosha.

"Vifaru na wanyama huko porini wanalindwa na helkopta ili wasizidi kuuawa, lakini albino wameshindwa kuwekewa walinzi na huku kila siku vifo vyao vinaripotiwa, hii inaonesha wazi kuwa suala la mauaji ya albino halishughulikiwi ipasavyo na mwenye dhamana ya kuhakikisha usalama wao ni Waziri wa Mambo ya Ndani, sasa leo hii anasema mauaji hayo ni kitu kidogo, jamii imueleweje?" walihoji.

Mtaalamu wa ushauri wa Jamii ya Albino Tanzania (TAS), Bw. Kondo Seif alisema kuwa ni lazima watahakikisha kuwa Bw. Masha anawajibishwa kwa kauli yake hiyo na kuahidi kuwa 'asipokufa' na waziri huyo basi atauawa na wauaji na kumtaka Rais Jakaya Kikwete amwajibishe waziri wake huyo haraka.

Aliongeza kuwa mpaka sasa hakuna takwimu sahihi za mauaji ya albino, ambapo kwa makadirio ni 32 tu ndio wanaotambulika kuuawa kinyama, lakini idadi hiyo ni ndogo sana kutokana na idadi kubwa ya albino wanaouawa kutotolewa taarifa iwe kwa makusudi au kwa bahati mbaya.

"Tulisikia kauli ya Mheshimiwa Rais Kikwete katika kilele cha maadhimisho ya kulaani mauaji ya albino kuwa ni lazima atasambaratisha mtandao wa wauaji kama dola lilivyofanikiwa kusambaratisha mtandao wa majambazi nchini.

"Kauli hii ilileta faraja kwa albino, lakini kwa bahati mbaya kuanzia siku ile hadi leo, albino kadhaa wamepoteza maisha yao na wengine kuongezewa kiwango cha ulemavu kwa kunyofolewa viungo vyao, jamii ya albino imepungukiwa imani kwa viongozi wao na vyombo vya dola kwa ujumla," alidai Bw. Seif.

Akizungumza kwa upande wa walemavu wote nchini, Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Walemavu la DOLASED, Bw. Gideon Mandesi alisema kuwa rasilimali fedha ni muhimu kuwepo ili kuhakikisha mchakato wa utekelezaji wa sera unafanikiwa na ubora wa maisha ya kila mtu mwenye ulemavu unapatikana Tanzania.

Hata hivyo alipotakiwa kufafanua juu ya kauli hiyo Waziri Masha alikanusha kusema hivyo badala yake alifafanua kuwa alieleza Serikali kusikitishwa na mauaji hao na kulaumu tu kuwa vyombo vya habari vimekuwa vikilikuza suala hilo.

"Sijawahi kuzungumza kitu kama hicho, isipokuwa nilisema kuwa serikali inasikitishwa sana na mauaji hayo na tunafanya juhudi kukomesha, ila baadhi ya waandishi wa habari wanataka kukuza mpaka suala hili kuonekana kuwa ni watanzania wote ndio wanaohusika kitu ambacho si kweli," alisema Bw. Masha.

Kutoka Majira
Majira
 
Sasa itabidi tupate nukuu ya hiyo habari yake maana anabisha kuwa hajasema hivyo.
 
Sasa itabidi tupate nukuu ya hiyo habari yake maana anabisha kuwa hajasema hivyo.

Tumewazoea hawa viongozi uchwara kila mara wakibofoa hukimbilia kusema wamenukuliwa vibaya, ebu kumbuka ya Ngombare Mwiru alivo ruka kimanga!

Si dhani kama hawa Albino ama waandishi wa BBC wali mnukuu vibaya, tena uzuri wa BBC huwa imerekodiwa, mweye kuweza pata ni ya tarehe gani aweke hapa ili itafutwe kwenye archive imawagwe hapa! Na ikibidi hao viongozi waitumie kama ushahidi halisi kumtaka awajibishwe!
 
Sasa itabidi tupate nukuu ya hiyo habari yake maana anabisha kuwa hajasema hivyo.

Siyo nukuu tu, walete video tuone na kusikia wenyewe. Ila kwa tabia ya viongozi wetu ya kutaka kukanusha kila kitu, siwezi kushangaa majibu ya Masha. Kwani mmesahau Mzee BWM alivyokanusha matamshi yake baada ya kusema kuwa ilani ya uchanguzi ya CCM 1995-2000 haitekelezeki??
 
Whether huyu Mheshimiwa ametamka hivyo au la lakini kwa suala la mauaji ya Albino binafsi naona Serikali haijalichukuilia hili jambo kwa uzito unaotakiwa. Iweje mauaji yanaendelea, hakuna watu wanaokamatwa kuhusiana na uovu huu na Serikali haitoi tamko lolote la kuhakikisha kuwa mtandao wa wauaji hawa unatokomezwa?. Katika hili jambo la kuwaua Albino kwa imani za kishenzi, nashauri Mh. Rais aweke msimamo uliowazi kuwa Viongozi wa maeneo amabayo mauaji haya yametokea ama yatatokea (Wakuu wa Wilaya/Mikoa, Wakuu wa Polisi pamoja na Waziri wa Mambo ya Ndani) wawe responsible. Pale wanaposhindwa kuthibiti uovu huu wawajibishwe mara moja bila kusubiri ngonjera nyingi kutoka kwao. Naamini hawa wauaji wanajulikana, waganga na wafanyabiashara wanaochochea uovu huu wanajulikana. Kwa nini hawakamatwi na kupelekwa kwenye vyombo vya sheria? Au nao wataitikisa Nchi kama wakikamatwa, au tuamini kuwa kuna viongozi wakubwa Serikalini wanashiriki katika uovu huu. Iweje mtoto mdogo anavamiwa kijijini mchana kweupe na kukatwa mikono na miguu halafu viongozi husika wanaishia kuwakamata watoto waliokuwa wameongozana na aliyeuawa kwa uchunguzi pasipo kuwakamata wauaji wenyewe?. Naomba Rais uwe tough katika hili, kama mengine yanashindikana hili nalo lisikushinde, ni aibu kwako na Watanzania wote.
 
Hata hivyo alipotakiwa kufafanua juu ya kauli hiyo Waziri Masha alikanusha kusema hivyo badala yake alifafanua kuwa alieleza Serikali kusikitishwa na mauaji hao na kulaumu tu kuwa vyombo vya habari vimekuwa vikilikuza suala hilo.

"Sijawahi kuzungumza kitu kama hicho, isipokuwa nilisema kuwa serikali inasikitishwa sana na mauaji hayo na tunafanya juhudi kukomesha, ila baadhi ya waandishi wa habari wanataka kukuza mpaka suala hili kuonekana kuwa ni watanzania wote ndio wanaohusika kitu ambacho si kweli," alisema Bw. Masha.
 
inasikitisha sana kama hii ndio kauli ya waziri mwenye dhamana na usalama wetu!!!!!
 
Hawezi kujiuzulu huyu anasiri nyingi za ufisadi uliochangia CCm 2005!! huo uwaziri ndio zawadi yake.
 
Mambo ya huyu Masha huwa hayanishangazi tena. Nahifadhi nguvu za kushagaa ya kushangalika. Hata kama alisema au hakusema suala liko wazi albino bado wanauawa, na hii ni aibu sana kwa mataifa mengine. Tunashindwa kujielezaTanzania ni nchi ya karne gani karne hii
 
"Sijawahi kuzungumza kitu kama hicho, isipokuwa nilisema kuwa serikali inasikitishwa sana na mauaji hayo na tunafanya juhudi kukomesha, ila baadhi ya waandishi wa habari wanataka kukuza mpaka suala hili kuonekana kuwa ni watanzania wote ndio wanaohusika kitu ambacho si kweli," alisema Bw. Masha.


I think this is where he went wrong! Kama anaamini mauaji ya albino ni suala kubwa, kwa nini anadhani waandishi wanalikuza? Ki mantiki Mh Masha anasema 'linakuzwa' kwa sababu yeye anamini ni suala dogo na hapo ndipo ugomvi na maalbino nadhani ulipoanzia. Kama ana busara anatakiwa awaombe radhi na serikali kwa dhati kabisa ishughulikie kadhia hii inayoitia aibu Tanzania na watanzania badala ya kulalamika kwamba linakuzwa na waandishi!
 
"Sijawahi kuzungumza kitu kama hicho, isipokuwa nilisema kuwa serikali inasikitishwa sana na mauaji hayo na tunafanya juhudi kukomesha, ila baadhi ya waandishi wa habari wanataka kukuza mpaka suala hili kuonekana kuwa ni watanzania wote ndio wanaohusika kitu ambacho si kweli," alisema Bw. Masha.


I think this is where he went wrong! Kama anaamini mauaji ya albino ni suala kubwa, kwa nini anadhani waandishi wanalikuza? Ki mantiki Mh Masha anasema 'linakuzwa' kwa sababu yeye anamini ni suala dogo na hapo ndipo ugomvi na maalbino nadhani ulipoanzia. Kama ana busara anatakiwa awaombe radhi na serikali kwa dhati kabisa ishughulikie kadhia hii inayoitia aibu Tanzania na watanzania badala ya kulalamika kwamba linakuzwa na waandishi!
Your logic is flawed.. Waandishi wa habazi wanataka kukuza kitu ambacho hajasema.. period!....
 
Mwenyewe amesema hakusema, na record ziko clear na waandishi wetu na inategemea hili gazeti ni la kiongozi gani, that is how low taifa letu limefikia sasa!
 
MAUAJI ya albino yanaendelea kutikisa, na safari hii kwa kutumia silaha kali, licha ya serikali kuanza operesheni maalum ya kupambana na uovu huo baada ya mlemavu wa ngozi anayefahamika kama Ezekiel John, 47, kuuawa kwa risasi na watu wasiojulikana ambao walitoweka na mkono wake wa kulia.


Mlemavu huyo wa ngozi aliuawa wakati akiwa nyumbani kwake.


Kamanda wa polisi mkoani Kigoma, Abdihaki Rashid alisema katika taarifa yake jana kuwa watu hao walivamia nyumbani kwa marehemu na kumpiga risasi mgongoni, na baadaye kumkata mkono ambao walitoweka nao.


“Tukio hilo lilitokea juzi, katika Kijiji cha Muyama wilayani Kasulu na askari waliokwenda kufanya uchunguzi wa awali katika eneo la tukio hawajarudi, hivyo watakaporejea tutatoa taarifa za kina zaidi,” inasema sehemu ya taarifa hiyo.


Mauaji ya albino yametapakaa katika mikoa ya Kanda ya Ziwa yakihusishwa na imani za kishirikina na tayari watu wengi wenye ulemavu wa ngozi wameshauawa kikatili na watu wasiojulikana ambao hukata viungo vya albino na kutoweka navyo.


Serikali imepeleka askari wa kikosi maalum cha kupambana na ukatili huo, lakini taarifa za kuuawa kwa albino zinaendelea kumiminika, huku polisi wanne wakiripotiwa kuwekwa ndani kwa tuhuma za kuwaachia wauaji wa albino baada ya kuhongwa fedha.


Mwanzoni mwa wiki hii watu waliokuwa wamejifunika sura zao walimvamia mwanafunzi wa darasa la tatu mwenye ulemavu huo, Mateso Dunia, 13 na kumuua kikatili.


Mtoto huyo wa darasa la tatu alikuwa mkazi wa Kijiji cha Gunihuna kilicho katika Kata ya Iponya wilayani Bukombe. Hilo lilikuwa tukio la pili wilayani humo kwa mtoto albino kuuawa tangu mauaji hayo ya kikatili yanayohusishwa na imani za uchawi yaanze Kanda ya Ziwa.


Tukio hilo lilitokea siku chache baada ya jeshi hilo kuwakamata polisi wanne ambao wanatuhumiwa kupokea rushwa kutoka kwa wauaji wa albino na kuwaachia huru.


Mwanafunzi huyo albino aliuawa juzi majira ya saa 6:00 wakati akiwa anarudi nyumbani na wenzake. Walikuwa wakitoka kuangalia video.


Hata hivyo baadaye miguu miwili ya albino ilikamatwa kwa mganga wa jadi ambaye alikimbia kabla polisi hawajamfikia.



Katika hatua nyingine taarifa hiyo ilisema kwamba, katika Kijiji cha Munyange, Polisi wakiwa katika doria ya kawaida, waliwakurupusha watu waliodhaniwa kuwa ni majambazi na kukimbia.


Taarifa hiyo ilifafanua kwamba watu hao wakiwa katika harakati za kukimbia, walidondosha mabomu mawili ya kutupa kwa mkono.

Mwananchi Read News

WAKATI HAYA YAKITOKEA ... WAZIRI ANAYEHUSIKA NA DHAMANA YA KUWALINDA MAALBINO NA WAKALA MKUBWA WA MAFISADI YUKO BUSSY KUPANGA MIKAKATI YA KUMWONGEZEA R. MENGI KODI ILI AFISILIKE....
 
Back
Top Bottom