don-oba
JF-Expert Member
- Dec 8, 2011
- 1,387
- 677
"Galanos school penda watoto....twakupenda twakusifu!.." mnaukumbuka huo wimbo?, Headmaster alikua T. Z. KINALA, namkumbuka sana mwl wa michezo Msocha. Tulikuwa tukitoroka tunaenda disco Club Lacasachika, siku moja walipitisha bed check usk tukakutwa hatupo. Suspension miezi miwili ndo ilikua adhabu kali. Special diet kwa wale wagonjwa tulikua tukivizia sicksheet za uongo tupate mbogamboga. J'4 na j'moc watu walikua wanajaa dinning hall kwasababu ya nyama na ubwabwa. Miogo 'chipc dume' ilikua zetu pale mwisho wa rami kwa ma K. J-DRONE na SOKORO hizo chata zilipigwa hadi kwenye kiti cha headmaster. Daladala zetu za Nguvumali, majani mapana- mjini zilikua full muziki. Patner wetu walikua TANGA tech na St Christina. Mkonge, Chai na pamba dom zilikua poa. Hebu tukumbushane mambo mengine wadau.