QUALITY
JF-Expert Member
- Sep 27, 2010
- 853
- 115
Ndugu zangu, mimi ni mgeni katika forum hii lakini kuna jambo moja nimelikumbuka ambalo huu ndio wakati wake muafaka. kuna walaka wa maaskofu waliouzindua mwaka huu ambapo baadaye waislamu nao walizindua walaka wao. sasa nyalaka hizi zililenga kuwafikishia ujumbe wapiga kura ili wasidanganyike mwaka 2010. sasa ziko wapi? Huu ndio wakati muafaka kuzieleza hadharani ili wananchi wafanye maamuzi sahihi.
wafuatao wanawajibu wa kujitokeza hadharani na kuueleza umma wa watanzania kuhusu nyaraka hizo ili watanzania waelewe namna ya kuchagua viongozi bora. Hongera kwa Kabobe kwa kuonesha njia hapo jana. Big Up!
watu hao ni pamopja na
1. Shekhe mkuu wa Tanzania
2. Mkuu wa Bakwata
3. Askofu mkuu Pengo
4. Askogu Gamanywa
5. Maaskofu wote tanzania ambao ni members wa Christian Council of Tanzania (CCT), Christian Social Service Committee (CSSC), Baraza la maskofu katoriki tanzania (TEC) n.k
Tukumbuke viongozi wa dini na madhehebu wanaongoza watu ambao maisha yao yanaathiriwa na maamuzi ya wana siasa. Viongozi hawa wasipoeleza ukweli watakuwa wanafiki. kwa sababu wananchi wataingia kuchagua chama badala ya mtu mwenye uwezo wa kuongoza ambaye ameonesha mfano wa namna ya kutetea maslahi ya Taifa. Hebu amkeni na kufungua vunywa vyenu na kuwajuza watanzania kuhusu ubaya na uzuri wa utawala unaomaliza muda wake. Huu si wakati wa kuendelea kuwaacha waumini gizani huku wengi wenu (viongozi wa dini na madhehebu) mkinung'unikia chini chini.
Kwa wanaoweza pia wekeni link ya kupata nyaraka hizo katika net ili wengine tuzisome pia.
wafuatao wanawajibu wa kujitokeza hadharani na kuueleza umma wa watanzania kuhusu nyaraka hizo ili watanzania waelewe namna ya kuchagua viongozi bora. Hongera kwa Kabobe kwa kuonesha njia hapo jana. Big Up!
watu hao ni pamopja na
1. Shekhe mkuu wa Tanzania
2. Mkuu wa Bakwata
3. Askofu mkuu Pengo
4. Askogu Gamanywa
5. Maaskofu wote tanzania ambao ni members wa Christian Council of Tanzania (CCT), Christian Social Service Committee (CSSC), Baraza la maskofu katoriki tanzania (TEC) n.k
Tukumbuke viongozi wa dini na madhehebu wanaongoza watu ambao maisha yao yanaathiriwa na maamuzi ya wana siasa. Viongozi hawa wasipoeleza ukweli watakuwa wanafiki. kwa sababu wananchi wataingia kuchagua chama badala ya mtu mwenye uwezo wa kuongoza ambaye ameonesha mfano wa namna ya kutetea maslahi ya Taifa. Hebu amkeni na kufungua vunywa vyenu na kuwajuza watanzania kuhusu ubaya na uzuri wa utawala unaomaliza muda wake. Huu si wakati wa kuendelea kuwaacha waumini gizani huku wengi wenu (viongozi wa dini na madhehebu) mkinung'unikia chini chini.
Kwa wanaoweza pia wekeni link ya kupata nyaraka hizo katika net ili wengine tuzisome pia.