Invisible
Robot
- Feb 11, 2006
- 9,075
- 7,878
Rushwa ndani ya bandari ya Dar es Salaam si jambo jipya. Bali kwa upande mwingine, jipya linakuja pale inapogundulika kuwa kuna urasimu ndani ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Pengine Mamlaka ya Mapato Tanzania inaweza kutaka kujibu ripoti kadhaa zilizotolewa kuhusiana na rushwa iliyokithiri katika uchukuzi wa kodi pale bandari ya Dar es Salaam.
Tangu mwezi Aprili, wakaguzi wa ndani wamekuwa wakikagua kesi mbali mbali zinazowahusu maafisa wa juu wanaosemekana kushirikiana na makabwela na wanaokwepa kulipa kodi. Ripoti hii imewasilishwa kwa mwenyekiti wa bodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania, Marceline Chijoriga.
Mwanzoni mwa mwezi Julai, Chijoriga alikiri kuwa moja kati ya watu waliotiliwa mashaka ni pamoja na Kamishna wa Ushuru na Forodha, Generosi Bateyunga, na kwa sasa amehamishwa kwenye majukumu mengine wakati yeye pamoja na maafisa wengine bado wapo kwenye uchunguzi zaidi.
Kwa mujibu wa Chijoriga, ripoti ya ukaguzi imewanyoshea vidole baadhi ya makamishna na makaimu ambao watawajibishwa na bodi. Pia imetoa shaka kuhusu maafisa wa chini abao wanahusika na menejimenti ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Bateyunga amepewa wiki mbili za kujibu mashtaka dhidi yake kama yanavyosemekana kwenye ripoti ya ukaguzi. Lakini, katika wale ambao wameshutumiwa kwenye ripotii hiyo, hakuna ambaye amesimamishwa kimajukumu, jambo ambalo linaweza kusababisha kupotea kwa baadhi ya nyaraka ambazo zinaweza kutumika kama ushahidi dhidi yao.
Tutawaletea zaidi kadiri habari zitakavyotufikia...
Pengine Mamlaka ya Mapato Tanzania inaweza kutaka kujibu ripoti kadhaa zilizotolewa kuhusiana na rushwa iliyokithiri katika uchukuzi wa kodi pale bandari ya Dar es Salaam.
Tangu mwezi Aprili, wakaguzi wa ndani wamekuwa wakikagua kesi mbali mbali zinazowahusu maafisa wa juu wanaosemekana kushirikiana na makabwela na wanaokwepa kulipa kodi. Ripoti hii imewasilishwa kwa mwenyekiti wa bodi ya Mamlaka ya Mapato Tanzania, Marceline Chijoriga.
Mwanzoni mwa mwezi Julai, Chijoriga alikiri kuwa moja kati ya watu waliotiliwa mashaka ni pamoja na Kamishna wa Ushuru na Forodha, Generosi Bateyunga, na kwa sasa amehamishwa kwenye majukumu mengine wakati yeye pamoja na maafisa wengine bado wapo kwenye uchunguzi zaidi.
Kwa mujibu wa Chijoriga, ripoti ya ukaguzi imewanyoshea vidole baadhi ya makamishna na makaimu ambao watawajibishwa na bodi. Pia imetoa shaka kuhusu maafisa wa chini abao wanahusika na menejimenti ya Mamlaka ya Mapato Tanzania.
Bateyunga amepewa wiki mbili za kujibu mashtaka dhidi yake kama yanavyosemekana kwenye ripoti ya ukaguzi. Lakini, katika wale ambao wameshutumiwa kwenye ripotii hiyo, hakuna ambaye amesimamishwa kimajukumu, jambo ambalo linaweza kusababisha kupotea kwa baadhi ya nyaraka ambazo zinaweza kutumika kama ushahidi dhidi yao.
Tutawaletea zaidi kadiri habari zitakavyotufikia...