BIG X
JF-Expert Member
- Nov 4, 2011
- 777
- 212
Maandamano ni haki ya kila mtu duniani popote. Wanaposema kuna taarifa za kiitelinjisia kwamba kutakuwa na uvunjifu wa amani kwenye maandamano basi kazi ya polisi ni kupambana na hizo taarifa sio kuzuia maandamano. Kazi ya polisi itakuwa ni kuwatia nguvuni watu ambao watabainika kuvunja amani wakati maandamano yakiendelea. Kwahiyo kazi ya polisi ni kulinda Amani wakati wa maandamano sio kuzuia maandamano. Kuzuia maandamano hasa yanapokuwa na lengo maalum ni kuhatarisha Amani nchini, Na kuwafanya wananchi wapoteze imani kabisa na jeshi la polisi.
Huku ni kushindwa kazi kabisa kwa wakuu wa jeshi la polisi. kwa mtu yoyote mwenye akili atajua tu kazi inayofanywa na jeshi la polisi sasa sio kuleta amani tena ni kuvunja amani kwa sababu ya maslahi ya watu wachache nchini na sio kwa Taifa. kwa hili hamna budi viongozi wote wa jeshi la polisi mjiuzuru kabla hamjabeba dhambi zote za watanzania.
Huku ni kushindwa kazi kabisa kwa wakuu wa jeshi la polisi. kwa mtu yoyote mwenye akili atajua tu kazi inayofanywa na jeshi la polisi sasa sio kuleta amani tena ni kuvunja amani kwa sababu ya maslahi ya watu wachache nchini na sio kwa Taifa. kwa hili hamna budi viongozi wote wa jeshi la polisi mjiuzuru kabla hamjabeba dhambi zote za watanzania.