Eeka Mangi
JF-Expert Member
- Jul 27, 2008
- 3,173
- 481
Jambo JF
Mimi bana naomba kwanza mniwie radhi. Najua ni maudhi kwenu ingawa pia kwa wengine inaweza kuwa baraka maana nimewaletea wenza wenu!
Miaka ya ujana wangu nilikuwa si haba jamani. Kama ni enzi hizi wallah nshafungwa!
Nikiwa kidato cha pili nilimpatia binti wa kidato cha kwanza ujauzito. Alifukuzwa shule na pia alijifungua katoto ka kike. Niliwahi kumwona mara moja tu! Then walipotea na mama yake. Sikujua waliko!
Nikiwa kidato cha nne house girl wetu naye likamkuta. Huyu alipata mtoto wa kiume! Akarudi kwao Singida!
Nikiwa namaliza kidato cha sita nikamwambukiza mwingine tena huyu alizaa mapacha. Naye tulipotezana sikujua aliko kwa kipindi kirefu.
Nikiwa pale Lang'ata Nairobi (Eti nilitakiwa niwe padri) nikapata binti mmoja naye hakudumu akaanza kutemea mate pembeni. Hakunivumilia akaja juu nikaachishwa chuo na kuozeshwa toto la Kwa Moi kipindi hicho.
Kwani kunguru mie nilidumu basi baada ya mtoto wa pili nikasepa nikarudi zangu Tanzania.
Nikapumzika kabisa na tangazo kubwa UKIPATA MIMBA URAFIKI WETU UMEKWISHA. So nimekaa hivyo kwa muda sasa.
Miaka 4 iliyopita nikaamua kuoa.
Huyu binti tuna mtoto mmoja naye ila anajua kuwa nina watoto 2 tu niliokuwa nao! Sikuwahi kumpa hadithi za hao wengine kwa kuhofia angeniona kiwembe sana.
Siku za karibuni nimeanza kupata salamu toka kwa watoto wale wa zamani wengine wakitamani kuniona tu. Kuna ambaye natarajia kuolewa siku za karibuni na anahitaji kumtambulisha mchumba wake kwa baba yake.
Naanzaje kumweleza mother house kuwa jeshi laja? Je ataelewa somo?
Najua wataalamu mpo humu! Sadia dugu!
Mimi bana naomba kwanza mniwie radhi. Najua ni maudhi kwenu ingawa pia kwa wengine inaweza kuwa baraka maana nimewaletea wenza wenu!
Miaka ya ujana wangu nilikuwa si haba jamani. Kama ni enzi hizi wallah nshafungwa!
Nikiwa kidato cha pili nilimpatia binti wa kidato cha kwanza ujauzito. Alifukuzwa shule na pia alijifungua katoto ka kike. Niliwahi kumwona mara moja tu! Then walipotea na mama yake. Sikujua waliko!
Nikiwa kidato cha nne house girl wetu naye likamkuta. Huyu alipata mtoto wa kiume! Akarudi kwao Singida!
Nikiwa namaliza kidato cha sita nikamwambukiza mwingine tena huyu alizaa mapacha. Naye tulipotezana sikujua aliko kwa kipindi kirefu.
Nikiwa pale Lang'ata Nairobi (Eti nilitakiwa niwe padri) nikapata binti mmoja naye hakudumu akaanza kutemea mate pembeni. Hakunivumilia akaja juu nikaachishwa chuo na kuozeshwa toto la Kwa Moi kipindi hicho.
Kwani kunguru mie nilidumu basi baada ya mtoto wa pili nikasepa nikarudi zangu Tanzania.
Nikapumzika kabisa na tangazo kubwa UKIPATA MIMBA URAFIKI WETU UMEKWISHA. So nimekaa hivyo kwa muda sasa.
Miaka 4 iliyopita nikaamua kuoa.
Huyu binti tuna mtoto mmoja naye ila anajua kuwa nina watoto 2 tu niliokuwa nao! Sikuwahi kumpa hadithi za hao wengine kwa kuhofia angeniona kiwembe sana.
Siku za karibuni nimeanza kupata salamu toka kwa watoto wale wa zamani wengine wakitamani kuniona tu. Kuna ambaye natarajia kuolewa siku za karibuni na anahitaji kumtambulisha mchumba wake kwa baba yake.
Naanzaje kumweleza mother house kuwa jeshi laja? Je ataelewa somo?
Najua wataalamu mpo humu! Sadia dugu!