Lunyungu
JF-Expert Member
- Aug 7, 2006
- 8,873
- 1,894
Mwananchi
Mon 30 Jan 12:47AM
Hamad Rashid atikisa Pemba
BOOKMARK THIS PAGE
Hamad Rashid atikisa Pemba Send to a friend
Monday, 30 January 2012 11:40
0digg
Aziza Masoud, Pemba
MBUNGE wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed ambaye alitangazwa kuvuliwa
uanachama na chama chake, jana alipokewa kwa mbwembwe na kuimarishiwa
ulinzi alipowasili Pemba. Msafara wake uliongozwa na magari manne ya
polisi yakiwa na ving'ora na askari takriban 30.
Hamad amefungua kesi Mahakama Kuu akipinga uamuzi wa chama chake
kumvua uanachama huku akiitaka iwatie hatiani viongozi wakuu wa chama
hicho akiwemo Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharrif Hamad
kwa tuhuma za kukiuka amri ya Mahakama.
Jana, Hamad aliwasili Uwanja wa Ndege wa Chake Chake, Pemba saa 5:45.
Baada ya kushuka katika Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL),
alipokewa na mamia ya mashabiki wake waliokuwa wakiimba:
Anamereta...,
Wengi wa mashabiki hao walikuwa wamevaa fulana nyeusi zilizoandikwa
Anti Virus na mara baada ya kuteremka katika ndege hiyo, alitumia
takriban dakika 20 kusubiri kutoka nje ya uwanja katika kile
kilichoelezwa na uongozi wa uwanja huo kuwa ni kuandaa mazingira ya
usalama kutokana na umati mkubwa wa watu uliokuwa umekwenda kumlaki.
Mbali na ulinzi huo wa polisi, mapokezi hayo yalikuwa na zaidi ya
pikipiki 85, magari 30 na umati wa watu. Hata hivyo, katika hali
isiyokuwa ya kawaida wananchi hao waliimba nyimbo mbalimbali bila
kukitaja CUF kama ilivyozoeleka.
Nyimbo zilizokuwa zikiimbwa katika mkusanyiko huo zilikuwa ni za sifa
kwa mbunge huyo... Hamad anameremeta... tumpambe maua... Hamad ni
nuru ya Wawi... hao vibua macho wanataka kushindana na Hamad hawawezi
haoooo na mwingine ukisema Maalim Seif, Serikali ya mseto haikufanya
kitu, tunataka mabadiliko.
Ilipotimu saa 6:15, msafara wake ulielekea hadi katika Uwanja wa soka
wa Ditia, ulioko katika Jimbo hilo la Wawi ambako Hamad alihutubia.
Hata hivyo, tofauti na ilivyokuwa siku za awali, hakuna bendera ya CUF
iliyokuwa ikipepea mbali na ile ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Akizungumza katika mkutano huo, Hamad alisema alishaambiwa na baba
yake kwamba atapambana na ugumu katika maisha ya kisiasa kwa kuwa
anasimamia haki na ukweli.
Marehemu baba yangu aliniambia katika siasa yatakukuta mambo manne
ambayo ni kufukuzwa katika chama, fitina na mwenzangu aliyeshika
mpini, kuwekwa ndani na kupigwa risasi katika hayo yote yameshanitokea
kasoro moja la kupigwa risasi, alisema Hamad.
Alisema Maalim Seif akisema ndiye chanzo cha migogoro yote ndani ya
chama hicho: Namuheshimu sana Maalim lakini uvumilivu umenishinda
dhambi tuliyoifanya kubwa wanachama wa CUF ni kumfanya Maalim Seif
kama malaika hana dhambi na hakosei kitu chochote na harekebishwi na
wanachama wengine.
Kama yeye ni hodari wa kutoa taarifa, aje atoe sababu ya kuweka
mageti ya kuzuia kuingia karafuu katika barabara zote wakati aliahidi
katika kampeni kwamba biashara ya zao la karafuu itakuwa huru.
Anashindwa kupita kwenye njia zake alizoziahidi, anatumia nafasi yake
kuharibu chama na kupandikiza chuki kwa watu.
Mmoja wa wakazi wa Wawi, Khamis Baharani alisema wakazi wengi wa jimbo
hilo wamestushwa na kufadhaishwa na uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la
CUF wa kuwafukuza wanachama watatu na wengine wanane kupewa karipio
bila wao kushirikishwa.
Baharani alisema Hamad ni mbunge wao na kwamba wanaamini amefanya
mambo mengi ya maendeleo na mazuri katika utumishi wake jimbo ni kwao
hivyo ingekuwa vyema wakashirikishwa katika hatua hiyo kubwa
iliyochukuliwa dhidi yake.
Mon 30 Jan 12:47AM
Hamad Rashid atikisa Pemba
BOOKMARK THIS PAGE
Hamad Rashid atikisa Pemba Send to a friend
Monday, 30 January 2012 11:40
0digg
Aziza Masoud, Pemba
MBUNGE wa Wawi (CUF), Hamad Rashid Mohamed ambaye alitangazwa kuvuliwa
uanachama na chama chake, jana alipokewa kwa mbwembwe na kuimarishiwa
ulinzi alipowasili Pemba. Msafara wake uliongozwa na magari manne ya
polisi yakiwa na ving'ora na askari takriban 30.
Hamad amefungua kesi Mahakama Kuu akipinga uamuzi wa chama chake
kumvua uanachama huku akiitaka iwatie hatiani viongozi wakuu wa chama
hicho akiwemo Makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar, Seif Sharrif Hamad
kwa tuhuma za kukiuka amri ya Mahakama.
Jana, Hamad aliwasili Uwanja wa Ndege wa Chake Chake, Pemba saa 5:45.
Baada ya kushuka katika Ndege ya Shirika la Ndege Tanzania (ATCL),
alipokewa na mamia ya mashabiki wake waliokuwa wakiimba:
Anamereta...,
Wengi wa mashabiki hao walikuwa wamevaa fulana nyeusi zilizoandikwa
Anti Virus na mara baada ya kuteremka katika ndege hiyo, alitumia
takriban dakika 20 kusubiri kutoka nje ya uwanja katika kile
kilichoelezwa na uongozi wa uwanja huo kuwa ni kuandaa mazingira ya
usalama kutokana na umati mkubwa wa watu uliokuwa umekwenda kumlaki.
Mbali na ulinzi huo wa polisi, mapokezi hayo yalikuwa na zaidi ya
pikipiki 85, magari 30 na umati wa watu. Hata hivyo, katika hali
isiyokuwa ya kawaida wananchi hao waliimba nyimbo mbalimbali bila
kukitaja CUF kama ilivyozoeleka.
Nyimbo zilizokuwa zikiimbwa katika mkusanyiko huo zilikuwa ni za sifa
kwa mbunge huyo... Hamad anameremeta... tumpambe maua... Hamad ni
nuru ya Wawi... hao vibua macho wanataka kushindana na Hamad hawawezi
haoooo na mwingine ukisema Maalim Seif, Serikali ya mseto haikufanya
kitu, tunataka mabadiliko.
Ilipotimu saa 6:15, msafara wake ulielekea hadi katika Uwanja wa soka
wa Ditia, ulioko katika Jimbo hilo la Wawi ambako Hamad alihutubia.
Hata hivyo, tofauti na ilivyokuwa siku za awali, hakuna bendera ya CUF
iliyokuwa ikipepea mbali na ile ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
Akizungumza katika mkutano huo, Hamad alisema alishaambiwa na baba
yake kwamba atapambana na ugumu katika maisha ya kisiasa kwa kuwa
anasimamia haki na ukweli.
Marehemu baba yangu aliniambia katika siasa yatakukuta mambo manne
ambayo ni kufukuzwa katika chama, fitina na mwenzangu aliyeshika
mpini, kuwekwa ndani na kupigwa risasi katika hayo yote yameshanitokea
kasoro moja la kupigwa risasi, alisema Hamad.
Alisema Maalim Seif akisema ndiye chanzo cha migogoro yote ndani ya
chama hicho: Namuheshimu sana Maalim lakini uvumilivu umenishinda
dhambi tuliyoifanya kubwa wanachama wa CUF ni kumfanya Maalim Seif
kama malaika hana dhambi na hakosei kitu chochote na harekebishwi na
wanachama wengine.
Kama yeye ni hodari wa kutoa taarifa, aje atoe sababu ya kuweka
mageti ya kuzuia kuingia karafuu katika barabara zote wakati aliahidi
katika kampeni kwamba biashara ya zao la karafuu itakuwa huru.
Anashindwa kupita kwenye njia zake alizoziahidi, anatumia nafasi yake
kuharibu chama na kupandikiza chuki kwa watu.
Mmoja wa wakazi wa Wawi, Khamis Baharani alisema wakazi wengi wa jimbo
hilo wamestushwa na kufadhaishwa na uamuzi wa Baraza Kuu la Uongozi la
CUF wa kuwafukuza wanachama watatu na wengine wanane kupewa karipio
bila wao kushirikishwa.
Baharani alisema Hamad ni mbunge wao na kwamba wanaamini amefanya
mambo mengi ya maendeleo na mazuri katika utumishi wake jimbo ni kwao
hivyo ingekuwa vyema wakashirikishwa katika hatua hiyo kubwa
iliyochukuliwa dhidi yake.