Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
Nawatoleeni Salam wahusika wote na wakuu Wenzangu nataka kujuwa kuhusu huo Umeme wa Jua ( Solar Power) Je nikitaka kununuwa hapo kwetu haswa hapo Dares-Salaam ni Vifaa gani vilivyo bora vya kununuwa na kutumia huo Umeme wa Jua haswa kwa matumizi ya nyumbani ? Kwa Matumizi yote yanayohusu Nyumba kwa mfano mimi nina Friji,TV, Mashine ya kufulia nguo, Mashine ya kufagia Makapeti na Computer.Je nitahitaji ninunuwe vifaa gani vilivyokuwa imara na amabavyo vitaweza kunitosheleza kwa hayo matumizi yangu ya Umeme ? Na Kwa gharama zake itakuwa ni bei gani? nawaombeni majibu toka kwenu asanteni.