Wakumbuka nyimbo za zamani? Hebu sikia na hii.....

platozoom

JF-Expert Member
Jan 24, 2012
9,366
11,154
Mimi sio mzee lakini napenda nyimbo za zamani kupita maelezo kuanzia za akina Mbaraka mwishehe,Marijani,Cuban marimba wengineo utaongezea.Unajua kwa nini nimezikumbuka leo? kuna wimbo umepigwa nikakumbuka kisa cha kama miaka 15 iliyopita.

Kuna mlevi mmoja alikuwa almaarufu mtaani kwa rafiki yangu,kila akilewa hujiimbia nyimbo za zamani anapotoka ulevini halafu hupita anapoishi huyo rafiki yangu(alikuwa amepanga) mida ya saa 3 hadi 5 usiku na kuelekea kwake kwa sababu hapo ilikuwepo njia. Kila anapopita mabinti wa mwenye nyumba ambao umri wao ni zaidi ya miaka 25 na ambao hawana kazi yeyote wanayofanya humcheka huyo mlevi na kumkejeli wakiwa wamekaa barazani kwao (walikuwa hawajaolewa na mapepe fulani hivi).

Siku ya siku yule mlevi akautandika mtindi kama kawaida na kupita huku akiimba wimbo huu wa zamani.............

Msichana wa sura aah nzuri..... nini kimekufanya usiolewe
Elimu unayo ya kutosha lakini bado hujaolewa
Wadogo wa nyuma yako wameolewa wamekuachaa.. ukihangaika

Ooh baby.usionyeshe majivuno kwa vijana,ukionyesha majivuno kwa vijana utabaki ukihangaika
oooh miaka yaenda sana na sura inachujuka......................

***********************************************
Wale mabinti waliposikia anaimba hivyo hawakumkejeli na waliufyata kuanzia siku hiyo.

Nafikiri alikuwa Daudi Kabaka huyu.Sijui nawe unakumbuka nyimbo yeyote ya zamani au bendi inayokukumbusha matukio ya raha na karaha..........................!

[h=1]Daudi Kabaka - Msichana sura Nzuri[/h]
 
Last edited by a moderator:
Naona raia wamepiga kimya muda mrefu, ngoja thread isipotee. Si unajua tena kama hapa ni Chit-Chat, post mia kwa siku.
Huyo ni Daudi Kabaka yeah, wimbo wake unaitwa Msichana wa Sura if me is not mistaken, alikuwa anaimba Twist, nyimbo zake zengine ni pamoja na Bush Baby Twist, Mulofa Moja, Helule Helule, African Twist...
Mlevi alitisha that day, aliwachana ukweli wao hao macheche.
Nenda kule jukwaa la 'Maselebriti' kuna uzi unamzungumzia Franco Luambo Luanza Makiadi, Baba ya Rhumba, nadhani utaufurahia huo.
Nikija nitakuja na profile ndogo ya Newton Karish,
unamjua huyu?
 
mtafute mtu mmoja anitwa zomboko utafurahi na roho yako,mimi huwa namsikiliza kila alhamisi kuanzia saa nne usiku mpaka saa saba usiku Redio free africa ya mwanza 98.6 fm kuna jamaa anaitwa wambura mtani anaendesha kipindi kizuri sana ambapo zomboko ni mmoja wachangiaji,pia yupo mchangiaji mungine anaitwa John Jambele hawa jamaa wanatisha
 
mtafute mtu mmoja anitwa zomboko utafurahi na roho yako,mimi huwa namsikiliza kila alhamisi kuanzia saa nne usiku mpaka saa saba usiku Redio free africa ya mwanza 98.6 fm kuna jamaa anaitwa wambura mtani anaendesha kipindi kizuri sana ambapo zomboko ni mmoja wachangiaji,pia yupo mchangiaji mungine anaitwa John Jambele hawa jamaa wanatisha

leo umeskiza?
 
Naona raia wamepiga kimya muda mrefu, ngoja thread isipotee. Si unajua tena kama hapa ni Chit-Chat, post mia kwa siku.
Huyo ni Daudi Kabaka yeah, wimbo wake unaitwa Msichana wa Sura if me is not mistaken, alikuwa anaimba Twist, nyimbo zake zengine ni pamoja na Bush Baby Twist, Mulofa Moja, Helule Helule, African Twist...
Mlevi alitisha that day, aliwachana ukweli wao hao macheche.
Nenda kule jukwaa la 'Maselebriti' kuna uzi unamzungumzia Franco Luambo Luanza Makiadi, Baba ya Rhumba, nadhani utaufurahia huo.
Nikija nitakuja na profile ndogo ya Newton Karish,
unamjua huyu?

Mkuu hapo ni sawa au ni ki-jamaica hicho?
 
unauliza makofi polisi mzee

nitaanza kufuatilia hicho kipindi.
Kuna kile cha Regina Mwalekwa kipindi akiwa Radio One, kila Ijumaa kuanzia saa tatu asubuhi, remember?
That mathee was awesome bana, na ile voice yake basi daah?
She knew the music for sho!
 
... Wale mabinti waliposikia anaimba hivyo hawakumkejeli na waliufyata kuanzia siku hiyo.
Nadhani mwimbo una maudhui ya male chauvinists wanaotaka wanawake wajirahisishe ili wao wafaidi. Jamaa anasema msichana anaringa ndo maana haolewi, yeye alimtaka lakini msichana akamwambia hana kisomo. Well, si kosa kwa mwanamke kukataa kuolewa na mtu ambae hana kisomo. Ukilazimisha mnaweza kukosa connection and intellectual compatibility mkawa hamuelewani. Mi msichana akinambia hanitaki kwa sababu kanipita elimu kwa kweli nitashukuru kanambia mapema, nisije nikashindwa kumridhisha intellectually au kwenye kipato. Sidhani kama huko ni kuringa.
 
Naona raia wamepiga kimya muda mrefu, ngoja thread isipotee. Si unajua tena kama hapa ni Chit-Chat, post mia kwa siku.
Huyo ni Daudi Kabaka yeah, wimbo wake unaitwa Msichana wa Sura if me is not mistaken, alikuwa anaimba Twist, nyimbo zake zengine ni pamoja na Bush Baby Twist, Mulofa Moja, Helule Helule, African Twist...
Mlevi alitisha that day, aliwachana ukweli wao hao macheche.
Nenda kule jukwaa la 'Maselebriti' kuna uzi unamzungumzia Franco Luambo Luanza Makiadi, Baba ya Rhumba, nadhani utaufurahia huo.
Nikija nitakuja na profile ndogo ya Newton Karish,
unamjua huyu?

Yap african twist.safi sana ila nyimbo zilikuwa fupi sana dakika 2 hadi 3 umekwisha.Newton Karish simkumbuki labda unitajie wimbo mmoja hivi nijaribu kuvuta kumbukumbu
 
mtafute mtu mmoja anitwa zomboko utafurahi na roho yako,mimi huwa namsikiliza kila alhamisi kuanzia saa nne usiku mpaka saa saba usiku Redio free africa ya mwanza 98.6 fm kuna jamaa anaitwa wambura mtani anaendesha kipindi kizuri sana ambapo zomboko ni mmoja wachangiaji,pia yupo mchangiaji mungine anaitwa John Jambele hawa jamaa wanatisha

ZOMBOKO Huwa anakuwa Redio one pia siku ya jumatano mchmbuzi mzuri sana,unaweza kupata feelings kama ulikuwepo enzi hizo..huwa nikisikiliza hizo nyimbo rafiki yangu ananiita mzee
 
Nadhani mwimbo una maudhui ya male chauvinists wanaotaka wanawake wajirahisishe ili wao wafaidi. Jamaa anasema msichana anaringa ndo maana haolewi, yeye alimtaka lakini msichana akamwambia hana kisomo. Well, si kosa kwa mwanamke kukataa kuolewa na mtu ambae hana kisomo. Ukilazimisha mnaweza kukosa connection and intellectual compatibility mkawa hamuelewani. Mi msichana akinambia hanitaki kwa sababu kanipita elimu kwa kweli nitashukuru kanambia mapema, nisije nikashindwa kumridhisha intellectually au kwenye kipato. Sidhani kama huko ni kuringa.

Usisahau ni enzi zile ambapo kuolewa lilikuwa jambo kubwa na heshima sana...ukiusikiliza kwa makini ni kama jamaa anamponda kwa kujiamini sana pengine akijua msichana ana stress.anyway hata me nikikataliwa kwa sababu ya elimu yangu ndogo nitashukuru
 
kuna huu wimbo naupenda sijui kaimba nani

"Kweli sasa nimeamua kujibu barua za kinamama, kila ninapozisoma kuhusu mambo ya kuoana....nachoka nachokaaa mie
Kwani nioa pachanga......."
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom