Wakulima wanapata posho gani?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,476
39,995
Baada ya kikundi cha watu wachache kujitengenezea mfumo wa posho kama mastahili ya kujikimu watu pekee ambao hawapokei posho japo ndio wanafanya kazi kubwa zaidi ni wakulima.

a. Mkulima anapolima mazao na kuyahifadhi anapata posho gani ya kufanya kazi yake kama mkulima? - farming allowance? alipwe na nani?

b. Mkulima anapopata upungufu wa mazao kutokana na hali mbaya ya hewa, soko n.k anapewa posho gani ya kujikimu kwa siku? Ili kumsaidia kumudu gharama za maisha? au hizi gharama za maisha zinawagusa watu wenye ajira rasmi tu?

c. Mkulima analeta mahindi, ndizi, nafaka nyingine, matunda hadi kwenye masoko makubwa say Kariako, Tandale n.k au Ngamiani pale Tanga je anapoouza mazao hayo analipwa posho ya kusafirisha (transportation allowance); je anaweza kudai "transportation allowance" au yeye anabeba gharama ya kusafirisha na kuiingiza kwenye bei ya vitu anavyouza? Vipi allowance ya vikao vya majadiliano ya bei (negotiation allowance) kwa muda anaotumia kufanya dili na wanunuzi?

d. Mkulima wetu huyu ambaye tunaambiwa ndiye anayeshikilia nchi kwa jasho lake anapotumia usafiri wake kuleta mazao kutoka shambani hadi sokoni au kwenye sehemu ya mauzo analipwa posho ya mafuta (gas allowance)? Au hatujali mazao hayo yanafikishwaje sokoni?

e. Hakuna kazi ngumu kama ukulima hasa ukulima wetu ambao bado unategemea sana jembe la mkono. Maandalizi ya shamba, kulima, kulinda mazao na hata kuja kuvuna ni kweli ni kazi ya "jasho" la mtu literally. Lakini mbona wanapoenda kuuza hasa wanapoiuzia serikali kwanini pamoja na kununua mazao serikali haiwalipi hardship allowance? Au wao hawastahili?

Ninachouliza hasa ni kuwa kwanini ni watumishi walioajiriwa katika sekta rasmi tu ndio wanalipwa hizi allowance ambazo hawataki kuziachia? Wakulima wetu mbona hata ruzuku hawapati (wenyewe wanapewa vocha! siyo fedha!). Kwanini hatuwapi ruzuku wakulima - ya fedha au allowance kusaidia kumudu maisha yao kama tunavyowapa watumishi wa umma na hata wengine wa sekta binafsi ambao tunaambiwa ati maisha ni magumu kweli kwao? Hivi wakulima wa Tanzania wanapata maisha mazuri kuliko ya watu wengine?

Jamani vipi kuhusu wanakijiji wenzangu wakulima? Tunawapa ahueni ipi katika mapato yao? au ndio yale yale "tutaboresha soko la mazao yetu ili wakulima wapate bei bora za mazao?".. Really? Au ni kwa sababu wao hawana uwezo wa kuiba waziwazi kama hawa wengine?
 
Ndio maana vijana wengi sana wanachukia kilimo....Unapata pesa baada ya kumenyeka kwa mwaka mzima na wakati mwingine mvua zinakufanyia mtima nyongo unaambulia patupu. Ila ukiwa machinga au mfanyakazi ....una uhakika wa kuiona msimbazi wakati wowote!!

Ila kwa mwendo huu wa kuwanyonya wakulima, ipo siku wote watagombea ubunge....Naamini hapo ndipo kila mtu atakapolijua jiji na joto lake!!
 
Tatizo haiko kwenye Katiba na Kanuni za Watawala.....what a shame reasoning!!!

Ndio maana kila jibwa lililochoka ku-fight kwa kanuni halisi linakimbilia kugombea ubunge
 
Kinachoniudhi mimi ni kuwa kuna kakikundi cha watu ambacho kanaamini kuwa kanastahili zaidi kwenye hii keki ya taifa kwa sababu tu kenyewe ndio kamepewa visu na uma kuikata keki hiyo.
 
Kwa Tanzania kuwa mkulima ni aina ya adhabu na kazi ya dhalili!
Hata tenda kubwa za kusupply pembejeo za Kilimo wanapewa watu walioko pale mtaa wa Azikiwe!
Posho?....ya nini kwa mshamba?
 
Kinachoniudhi mimi ni kuwa kuna kakikundi cha watu ambacho kanaamini kuwa kanastahili zaidi kwenye hii keki ya taifa kwa sababu tu kenyewe ndio kamepewa visu na uma kuikata keki hiyo.

Unajua Mwanakijji kama hawa watu wangekuwa wanajali basi wangefanya hivi

Kwenye viti maalum vya ubunge kungewa na nafasi moja au mbili ya wakulima bora kila mkoa au wilaya. kama kuna nafasi maalum za wanawake na walemavu nadhani si vibaya wakulima ambao ni disdavantage but important group ingekuwa na muwakilishi japo mmoja kila mkoa.

Kila mwaka kutokna a na uzalishaji wa mazao au mifugo basi mkulima fulani agekuwa anachaguliwa kuwailisha kila mkoa kwenye bunge la kila mwaka. Nao waonje posho . teh teh teh .
 
Mfano wabunge, ndio wenye jukumu la kutunga sheria.
Sasa wanapotunga sheria ya kujilipa posho ya kikao, hii sio ndio inayoitwa "the conflict of interest"?
Swali, ni nani atakuwa mtatuzi wa hii conflict?
I'm just cooking my brain ............!
 
wauza kahawa walikuwa wanapewa kitu kinaitwa mabaki..sema kahawa ishakufa

Naomba nitoe maelezo tofauti kwa ufahamu wangu..... BAKI haikuwa posho hata chembe. Ilikuwa ni malipo halali kutokana na price flactuations kwenye soko la dunia. Ni hivi, wakulima wa kahawa (wooote) walikuwa wanauza kahawa yao kwenye vyama vya ushirika i.e KNCU. Sasa KNCU ananunua kwa bei ya wakati huo (current price) lakini wakati wa mauzo bei inabadilika kwenye soko la dunia na kuwa juu hivyo anapata faida zaidi ya initial projections. Ni kutoka kwenye hiyo nyongeza ya faida ndiyo BAKI inalipwa na ndio maana BAKI ilikuwa ina-flactuate mwaka hadi mwaka hata kama kiasi cha kahawa ulichouza kinalingana. Kumbuka kahawa iko kama oil. price kwenye soko la dunia inabadilika kila mara. Hata hivyo hii concept na implementation ya BAKI naweza kusema iliwezekana tu kwa sababu ya uaminifu/ethics za watawala wetu kipindi hicho. Sasa hivi kahawa ikinunuliwa ni kimoja!
 
Naomba nitoe maelezo tofauti kwa ufahamu wangu..... BAKI haikuwa posho hata chembe. Ilikuwa ni malipo halali kutokana na price flactuations kwenye soko la dunia. Ni hivi, wakulima wa kahawa (wooote) walikuwa wanauza kahawa yao kwenye vyama vya ushirika i.e KNCU. Sasa KNCU ananunua kwa bei ya wakati huo (current price) lakini wakati wa mauzo bei inabadilika kwenye soko la dunia na kuwa juu hivyo anapata faida zaidi ya initial projections. Ni kutoka kwenye hiyo nyongeza ya faida ndiyo BAKI inalipwa na ndio maana BAKI ilikuwa ina-flactuate mwaka hadi mwaka hata kama kiasi cha kahawa ulichouza kinalingana. Kumbuka kahawa iko kama oil. price kwenye soko la dunia inabadilika kila mara. Hata hivyo hii concept na implementation ya BAKI naweza kusema iliwezekana tu kwa sababu ya uaminifu/ethics za watawala wetu kipindi hicho. Sasa hivi kahawa ikinunuliwa ni kimoja!

Kwakweli umelitolea ufafanuzi mruri na ambao ndio ukweli wenyewe. na jingine la kuwa ilikuwa iknawezekana kwa sababu ya uaminifu wa wakati huo nalo ni ukweli mwingine uliotukuka. na kwa sasa wanafanya hivo baada ya kuwa wameishajihakikishia kuwa wameua kila kilichokuwa kinasimamia haki ya mkulima iwe ni vyama vya ushirika hata kama vipo si kwa manufaa ya mkulima tena, miiko ya uongozi ndio hiyo waliizikia zanzibar na hata wale waliokuwa wanaiamini na kuisimamia waliisha wazika wote sasa ni utawala ndio umeshika hatamu hakuna uongozi wala utumishi wa umma ni UTAWALA MTINDO MMOJA
 
hata mimi utingo nawasaidia wakulima na wachoma mikaa kuuingiza mjini wengine nawafungia juu ya malori kwa TOZO dogo sana, sihitaji posho, nahitaji ruzuku!
 
Hata km nina ajira rasmi siwezi kushabikia uroho huu na ulafi uliobarikiwa kwa kupewa jina la kiungwana...maana kwa kufanya hivyo nitakua nimemsaliti mama yangu aliyebinafsisha nguvu zake za mwili bila posho kwa kukakamata jembe sawasawa hadi leo hii walao najua nini tofauti ya ujira na posho...ni broilers pekee wanaoweza ku support hizi 'what so ever allowance' lakini kwa sisi watoto wa kienyeji si jambo la kusherehekea hata kidogo!
 
Swali zuri bwana Mwanakijiji. Ni wapi hayo uliyoauliza yanafanyika? Tupe uzoefu maana wewe mwenzetu exposure yako ni kubwa sana!
 
Mwanakijiji,

Wenzako watakwambia kwenye Income tax Act (na pia VAT) kuna allowances, sijui wanayaita capital goods au stuffs like that kwenye pembejeo na kilimo. Swali langu ni hili, hivi hawa watunga sheria zetu kwelu wanaamini mzee wangu wa huko Ikungulyabashashi anaweza kufunua "schedule" ya Income tax Act kuona hizo allowances?

Pili utatofautiana sana na hao "wakulima". Wenzako wakiongelea wakulima ni makampuni, au kwa lugha yao "wawekezaji". All of sudden it comes to one certaion thing, makampuni ya madini (wawekezaji) ndio wafaidika wakubwa kwa sera za nchi hii, wakulima (makampuni & wawekezaji) ndo wafaidika wakubwa, wachimba madini wadogo ni wezi na/au wavamizi so wanachostahili ni kufukuzwa tu, "wakulima" wetu wengine hawajui hata kuna hizo allowance, wanachojua ni mbolea, bei bora, mvua ipo au haipo basi.

Conclusion: Nchi hii usipokuwa mmoja wa waheshimia kujilipa posho, au kampuni ya madini/ukulima au kufanya kazi katuika maeneo hayo, nakuhakikishia you're guarantee to live on hell. Tazama wamachinga, hao wakulima, walimu, etc na uniambie
 
Baada ya kikundi cha watu wachache kujitengenezea mfumo wa posho kama mastahili ya kujikimu watu pekee ambao hawapokei posho japo ndio wanafanya kazi kubwa zaidi ni wakulima.

a. Mkulima anapolima mazao na kuyahifadhi anapata posho gani ya kufanya kazi yake kama mkulima? - farming allowance? alipwe na nani?

b. Mkulima anapopata upungufu wa mazao kutokana na hali mbaya ya hewa, soko n.k anapewa posho gani ya kujikimu kwa siku? Ili kumsaidia kumudu gharama za maisha? au hizi gharama za maisha zinawagusa watu wenye ajira rasmi tu?

c. Mkulima analeta mahindi, ndizi, nafaka nyingine, matunda hadi kwenye masoko makubwa say Kariako, Tandale n.k au Ngamiani pale Tanga je anapoouza mazao hayo analipwa posho ya kusafirisha (transportation allowance); je anaweza kudai "transportation allowance" au yeye anabeba gharama ya kusafirisha na kuiingiza kwenye bei ya vitu anavyouza? Vipi allowance ya vikao vya majadiliano ya bei (negotiation allowance) kwa muda anaotumia kufanya dili na wanunuzi?

d. Mkulima wetu huyu ambaye tunaambiwa ndiye anayeshikilia nchi kwa jasho lake anapotumia usafiri wake kuleta mazao kutoka shambani hadi sokoni au kwenye sehemu ya mauzo analipwa posho ya mafuta (gas allowance)? Au hatujali mazao hayo yanafikishwaje sokoni?

e. Hakuna kazi ngumu kama ukulima hasa ukulima wetu ambao bado unategemea sana jembe la mkono. Maandalizi ya shamba, kulima, kulinda mazao na hata kuja kuvuna ni kweli ni kazi ya "jasho" la mtu literally. Lakini mbona wanapoenda kuuza hasa wanapoiuzia serikali kwanini pamoja na kununua mazao serikali haiwalipi hardship allowance? Au wao hawastahili?

Ninachouliza hasa ni kuwa kwanini ni watumishi walioajiriwa katika sekta rasmi tu ndio wanalipwa hizi allowance ambazo hawataki kuziachia? Wakulima wetu mbona hata ruzuku hawapati (wenyewe wanapewa vocha! siyo fedha!). Kwanini hatuwapi ruzuku wakulima - ya fedha au allowance kusaidia kumudu maisha yao kama tunavyowapa watumishi wa umma na hata wengine wa sekta binafsi ambao tunaambiwa ati maisha ni magumu kweli kwao? Hivi wakulima wa Tanzania wanapata maisha mazuri kuliko ya watu wengine?

Jamani vipi kuhusu wanakijiji wenzangu wakulima? Tunawapa ahueni ipi katika mapato yao? au ndio yale yale "tutaboresha soko la mazao yetu ili wakulima wapate bei bora za mazao?".. Really? Au ni kwa sababu wao hawana uwezo wa kuiba waziwazi kama hawa wengine?

Labda kulingana na vyama vya ushirika husika,kule kwetu Nanyumbu kwa mwaka jana wakulima walilipwa korosho kwa awamu tatu. yaani kwanza walilipwa malipo yao halisi.korosho zilipouzwa nje ile faida (ziada) ilipelekwa kwa wakulima wakalipwa kwa mara ya pili, chama tena kikatoa posho (malipo ya tatu) kwa wakulima. Mwaka huu mkuu wetu wa wilaya ya Nanyumbu aliongoza wakulima katika kilimo cha choroko,tena kwa vitendo, yaani yeye mwenyewe alilima takriban hekari 8 za choroko na kwa hakika alipigana kufa na kupona kufuatilia masoko ya choroko, ambapo mafanikio yameonekana kwani kilo moja ya choroko mwaka huu imeuzwa kwa shilingi 1500/= cash. japo baadae bei ilipungua kutokana na quality kupungua katika miezi ya mwisho mwa msimu wa mvua.hapo utasema serikali haiwajali wakulima? Big up Dada yetu Fatma. Nanyumbu oyeeeeeee!
 
Baada ya kikundi cha watu wachache kujitengenezea mfumo wa posho kama mastahili ya kujikimu watu pekee ambao hawapokei posho japo ndio wanafanya kazi kubwa zaidi ni wakulima.

a. Mkulima anapolima mazao na kuyahifadhi anapata posho gani ya kufanya kazi yake kama mkulima? - farming allowance? alipwe na nani?

b. Mkulima anapopata upungufu wa mazao kutokana na hali mbaya ya hewa, soko n.k anapewa posho gani ya kujikimu kwa siku? Ili kumsaidia kumudu gharama za maisha? au hizi gharama za maisha zinawagusa watu wenye ajira rasmi tu?

c. Mkulima analeta mahindi, ndizi, nafaka nyingine, matunda hadi kwenye masoko makubwa say Kariako, Tandale n.k au Ngamiani pale Tanga je anapoouza mazao hayo analipwa posho ya kusafirisha (transportation allowance); je anaweza kudai "transportation allowance" au yeye anabeba gharama ya kusafirisha na kuiingiza kwenye bei ya vitu anavyouza? Vipi allowance ya vikao vya majadiliano ya bei (negotiation allowance) kwa muda anaotumia kufanya dili na wanunuzi?

d. Mkulima wetu huyu ambaye tunaambiwa ndiye anayeshikilia nchi kwa jasho lake anapotumia usafiri wake kuleta mazao kutoka shambani hadi sokoni au kwenye sehemu ya mauzo analipwa posho ya mafuta (gas allowance)? Au hatujali mazao hayo yanafikishwaje sokoni?

e. Hakuna kazi ngumu kama ukulima hasa ukulima wetu ambao bado unategemea sana jembe la mkono. Maandalizi ya shamba, kulima, kulinda mazao na hata kuja kuvuna ni kweli ni kazi ya "jasho" la mtu literally. Lakini mbona wanapoenda kuuza hasa wanapoiuzia serikali kwanini pamoja na kununua mazao serikali haiwalipi hardship allowance? Au wao hawastahili?

Ninachouliza hasa ni kuwa kwanini ni watumishi walioajiriwa katika sekta rasmi tu ndio wanalipwa hizi allowance ambazo hawataki kuziachia? Wakulima wetu mbona hata ruzuku hawapati (wenyewe wanapewa vocha! siyo fedha!). Kwanini hatuwapi ruzuku wakulima - ya fedha au allowance kusaidia kumudu maisha yao kama tunavyowapa watumishi wa umma na hata wengine wa sekta binafsi ambao tunaambiwa ati maisha ni magumu kweli kwao? Hivi wakulima wa Tanzania wanapata maisha mazuri kuliko ya watu wengine?

Jamani vipi kuhusu wanakijiji wenzangu wakulima? Tunawapa ahueni ipi katika mapato yao? au ndio yale yale "tutaboresha soko la mazao yetu ili wakulima wapate bei bora za mazao?".. Really? Au ni kwa sababu wao hawana uwezo wa kuiba waziwazi kama hawa wengine?


MM,

Sikio la kufa halisikii dawa. Hawa wabunge wa CCM wameamua kufunga masikio na kuangalia maslahi yao binafsi. Ukiwauliza uhalali wa hizo posho unaweza kuvunjika mbavu kuna anatokea kisiwa cha kule kusini nilimuuliza je wavua samaki nao mnawakatia kidogo hizo posho akanijibu lazima ati!!! nikasema kweli wameenda kutetea maslahi yao binafsi. Hao ndio watunga sheria wetu.

Isipokuwa usiwe na wasiwasi mkuu waangalie tu Ugiriki wanavyoteseka hadi wale wabunge waliokuwa wakitetea posho bungeni sasa hivi wanapiga kura wapunguziwe mishahara yao. Kufilisika sio mchezo!!!!! Tanzania muda ukiwadia utajionea mwenyewe.
 
Back
Top Bottom