Wako ni waina gani?

Pdidy

JF-Expert Member
Nov 22, 2007
50,956
22,136
[h=3]Wako ni wa aina gani?[/h]

Mara nyingi kuna usemi kwamba kwa mwanaume kawaida ana kitu kimoja tu ambacho kinaweza kumfanya apate hamu ya kufanya mapenzi nacho ni “kitu chochote”.
Najua hujanielewa ila Ukweli ni kwamba mwanaume ni tofauti sana na mwanamke linapokuja suala la kusisimka kimapenzi kwani mwanaume anaweza kusisimka (stimulated) hata pale tu mwanamke au mke wake akiwa nusu uchi, au uchi au hata kile kitendo cha kuvua nguo au akiwa amevaa kivazi chochote kinachoshawishi, wanawake hawapo hivyo.
Wanawake kila mmoja ni tofauti hata huyo mmoja (mke wako) yupo tofauti kila siku katika mwezi mmoja, mwaka na miaka.
Mwanaume unahitaji kuwa mbunifu kufahamu namna upepo wa hamu ya mapenzi unavyovuma kwa mke wako, kwani ukilemaa unaweza kuchanganya mambo na kupitwa na wakati.
Unahitaji kujifunza nini kinaweza au kwa sasa kunamsisimua mke wako kuwa tayari kukupa nafasi ya kufurahia tendo la ndoa.
Inawezekana mkeo ni aina ya wanawake ambao husisimka na kuwa tayari kimapenzi kwa kuguswa, kumbatiwa, shikwashikwa (caresses) yaani TOUCH GIRL!
Au Inawezekana mke wako ni aina ya wanawake ambao ukitaka apate hamu ya kuwa na wewe ni sharti uongee, umsifu, umtie moyo, uchonge sana maneno matamu yaani TELL ME GIRL.
Inawezekana yeye ni wale wa kuwashirikisha siri, au malengo au jambo lolote unafanya au waza ndipo afunguke kimapenzi yaani SHARE WITH ME GIRL.
Inawezekana mke wako ni walewale usipofanya kazi naye, usipomsaidia vikazi vidogo vidogo pale nyumbani, kupika chakula, kufunga net nk hawezi kujibu kimapenzi yaani DOING GIRL.
Inawezekana ni aina ya mwanamke ambaye ukitaka ufurahie mwili wake na moyo wake chumbani lazima mfanye maombi, au soma Neno (Biblia), au fanya ibada au ongea mambo ya kiroho yaaani SPIRITUAL GIRL.
nk
Je, wewe mwanaume unayesoma hapa unajua mke wako ni aina gani
 
Back
Top Bottom