Peter Fabian
Member
- Jul 18, 2011
- 73
- 7
Huu ndio mguso wa fikra zangu kwa leo!kiukweli ni chama pekee ambacho kwa sasa kimeonyesha kupendwa na wananchi wengi hasa hasa vijana na hii ni kwa sababu ya ujasiri na uwazi wa viongozi wake ambao waliamua kuyatoa maisha yao kwa ajili yawatanzania,walizika wazi kashfa zote nzito walizofanikiwa kuzijua kwa hoja zenye msingi imara,wasiwasi wangu ni juu ya kushuka kwa umaarufu wa chama hicho,ndiyo chama hichi cha vidole viwili,umaarufu wake si mkubwa sana kwa sasa kulinganisha na kipindi kile alichokuwepo Dr.Claa ndani ya mjengo,pia moto wao ndani ya bunge si mkali sana kama zamani walivyokuwa wachache,pia hata nafasi aliyo nayo Mboy kama kiongozi wa upande wa pili hajaweza kuitendea haki na furungu baina yao na kupigana pia kunanipa mashaka kuwa kwasasa ndani ya chama cha vidole viwili wameingia mamluki ambao mi wananipa ujasiri wakusema kinaweza kisifike 2015 ingawa ndio chama kilichobeba matumaini ya watanzania wengi katika nyanja zote,jamani ukitaka inzi wasikufuate sharti utupe mzoga,mnahaja ya kujitanzama marambili mkitaka kufika 2015 kwa amani kama ilivyokuwa 2010