Wakili: DOWANS itadhoofisha nchi

Angalia wanasheria wa Tanzania walivyo. Huyu Fungamtama alikuwa akijidai kuzungumzia shauri hili kama raia wa kawaida aliyejua lolote kuhusu kesi hiyo. Akajifanya kutoa ushuri kuwa ni lazima serikali ilipe pesa hizo kwa sababu makosa yalifanywa na watu walioitetea TANESCO, leo hii ndiye anayepeleka nakala ya hukumu hiyo mahakamani kusajiliwa ili apate mshiko wake:

Kampuni ya Dowans leo imewasilisha rasmi maombi ya madai ya usajili wa TUZO katika Mahakama Kuu kanda ya Dar es Salaam na kusajiliwa kwa kupewa namba ya usajili nane ya mwaka huu.

Kampuni ya Dowans ilishinda kesi ya madai dhidi ya TANESCO katika Mahakama ya Kimataifa ya Usuluhishi wa Migogoro ya Kibiashara (ICC) na kuamuliwa TANESCO kumlipa Dowans Sh Bilioni 94.

Naibu msajili mwandamizi wa mahakama hiyo Mh. Salvatory Mwongole,ameiambia Globu ya Jamii kwamba maombi hayo yameifikia mahakama hiyo januari 25 mwaka huu na yamewasilishwa na wakili wa kampuni hiyo hapa nchini kutoka kampuni ya uwakili ya Kennedy Fungamtama.

Mh. Mwongole amesema maombi hayo yamekwishapangiwa jaji lakini kulingana na unyeti wa suala hilo jina la jaji linahifadhiwa kwa sababu ndio kwanza ameteuliwa kushughulikia maombi ya usajili huo na jalada halijamfikia.

Alisema maombi hayo ya usajili yameombwa na kampuni ya Dowans Holdings S.A na Dowans Tanzania dhidi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).

Kwa mujibu wa sheria TUZO hiyo haitasajiliwa hadi mahakama itoe nafasi kwa mdaiwa kuwasilisha pingamizi kupinga usajili wa Tuzo hiyo kama anaona haifai kusajiliwa, na kama hana pingamizi itasajiliwa kama imekidhi sheria na mdaiwa kulazimika kulipa fedha hizo.

Wadau wengine pia wana nafasi ya kuwasilisha maombi yao kama wanadhani usajili wa TUZO hiyo haustahili nayo pia yatapokelewa, Mahakama ikishasikiliza kama kuna mapingamizi itatoa maamuzi kama ni kuisajili au la.
 
Fungamtama ana maslahi binafsi katika kesi hii wakati Sitta anatetea maslahi ya watanzania wote! Watu kama Fungamtama hawatakiwi kwenye jamii kabisa. ICC haiwezi kupuuza kuhusu mmiliki wa Dowans hizo ni propaganda za Fungamtama tu! Pamoja na kwamba company ni legal person lazima wamiliki wake wajulikane pia! Issue iliyopo hapa ni kwanini Dowans iwe na uhalali wa ku-contract wakati ilii-rith Company hewa ya Richmond? Kama kamati ya bunge iliona Richmond ni company hewa, inawezekanaje Dowans iwe halali? Zote Richmond na Dowans ni company hewa!! Wabaya wetu wakubwa ni akina Fungamtama wanaoweka maslahi yao binafsi mbele na inabidi washughulikie!
 
Mimi ninapendekeza, hata kabla ya kuwatafuta wamiliki wa Dowans, kwanza tuambiwe washiriki wote kwa upande wa serikali na tanesco walio ridhia madudu yote haya yaliyo tokea. tujue majina yao na walishiriki vipi ! tuwafunge kwanza hawa na kuwafilisi mali zao zote na kisha tumjue mmiliki wa hiyo Dowans, manake hawa tutakao wafilisi na kuwafunga lazima watakuwa wanamjua mmiliki. haiwezekani nchi iingie kwenye utata wa kiasi hiki na kusiwe muwajibikaji wa kuadhibiwa !! au wahusika walio liingiza taifa hili kwenye utata huu nao hawajulikani?
 
Back
Top Bottom