Apologise lady
JF-Expert Member
- Sep 16, 2013
- 5,979
- 3,097
Ni nini mbaya wamefanya watu wa kenya???
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
kuna ticha 1 wa kenya alikuwa anafundisha wingi na umoja ilikuwa ni balaa tupu.
wingi wa KISU anakwambia MIBISU.. sasa iko ni kiswahil cha wapi.
Kama hicho wanachoongea ni kiswahili chao, basi huko ndio tunaita kuharibu kiswahili. Huwezi kuweka makosa ya namma hiyo kwenye mitihani eti kisa ni kiswahili cha kikwako..Unajiumiza bure, kile ni kiswahili chao na hicho unachokisifia ni kiswahili chako. Lugha zote ziko hivyo hivyo, hutofautiana kwa kutegemea eneo, nchi hadi bara. Kiingereza cha London hakifanani na cha New York na hata vitabu wanavyovitumia kama dictionary ni tofauti. Kiingereza cha Afrika Kusini hakifanani kabisa na cha Nigeria na hivyo hivyo kiingereza cha Kenya hakifanani na cha New Zealand na kote huko Kiingereza ndiyo lugha kuu ya taifa. Kiswahili nacho kinatofautiana - cha Zaire hakifanani na cha Uganda na cha Zanzibar hakifanani na cha Mwanza, sasa kwa nini useme cha Kenya ni kibovu na huku wanaelewana wazungumzaji. Nimeshuhudia wakitucheka kwa kuongea Kiswahili kibovu hasa tunaposema maiti huyu badala ya maiti hii, au ng'ombe huyu badala ya ng'ombe hii - sasa hapo !