Wakazi wa Dar Es Salaam wanakwamisha Mageuzi Tanzania.

JACADUOGO2.

JF-Expert Member
Dec 13, 2010
930
217
Ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa Tanzania kwani Dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela?

Wakazi wa Dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya UDAKU kama mambo ya Kanumba, Lulu, Wema, Diamond, Johari, Jokate. UBITOZI NA USHAROBARO kwa kwenda mbele.

Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama Dar, wakazi wa Dar badilikeni.....!!!!
 
Vijiwe (hasa vya Bao na Kahawa) vilivyo pandikizwa na MAGAMBA ndivyo chanzo cha watu kutokuwa ma mzuka huo.. wengi wapo Humu JF mabingwa wa kulalama lakini ikitokea tuingie front ,utasikia NIKO BIZE BANA.......
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa Tanzania kwani Dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela? Wakazi wa Dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya UDAKU kama mambo ya Kanumba, Lulu, Wema, Diamond, Johari, Jokate. UBITOZI NA USHAROBARO kwa kwenda mbele.
Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama Dar, wakazi wa Dar badilikeni.....!!!!

Umekosea sana ndugu. vyama vingi vya siasa chimbuko lake Dar es Salaam. Dar ndiyo chimbulo la mageuzi Tanzania. Mkutano wa kwanza wa mageuzi ulifanyika Motel Agip Dar es Salaam, siyo Arusha. Mtei, Mareale, Makani na timu yake walianzisha chadema Kisutu Dar es Salaam.

Magazeti kama Shaba, Watu, Family Mirror, Majira ndiyo vyombo vya habari vya mwanzo kutoa elimu ya uraia kuhamasisha watu kufikiri kimageuzigeuzi ndipo wewe ukapata elimu inayokupa werevu katika siasa.

Hawa watu wote wanakaa Dar es Salaam. Dar es Salaam ndiyo msingi wa mageuzi Tanzania. Kwa sasa ni kama baba ambaye kajichokea kwa mahangaiko ya muda mrefu na umri kwenda sana, wanae wameshakuwa wakubwa ndio wanahangaika sasa huko pembezoni kumsaidia baba.

Nina hakika baba huyu akiitazama Arusha leo, na Mwanza, na Mbeya, Tandahimba, na Songea, Iringa mjini nasikia eti hata Dodoma? moyo wake unapata faraja! Ipe Dar es Salaam sifa inayostahili.

Ni kweli vijana wana nguvu sana sasa. Lakini halikuanza jana Arusha, mkuu!
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa Tanzania kwani Dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela? Wakazi wa Dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya UDAKU kama mambo ya Kanumba, Lulu, Wema, Diamond, Johari, Jokate. UBITOZI NA USHAROBARO kwa kwenda mbele.
Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama Dar, wakazi wa Dar badilikeni.....!!!!

Mkuu wakazi wa dar wameathiriwa sana na nyoto kiasi kwamba hata uwezo wa kufikiri unakuwa mdogo
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa Tanzania kwani Dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela? Wakazi wa Dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya UDAKU kama mambo ya Kanumba, Lulu, Wema, Diamond, Johari, Jokate. UBITOZI NA USHAROBARO kwa kwenda mbele.
Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama Dar, wakazi wa Dar badilikeni.....!!!!

Nadhani umri wako ni mdogo siwezi kukulaumu hivi unajua kuwa Dar ndio kila kitu ndio chimbuko la siasa za mageuzi Tanzania wewe unadhani siasa zimeanza baada ya Lema kushinda Arusha...fuatilia mdogo wangu historia ya Dar es Salaam.
 
siamini kihivyo kwa sababu;
  • Dar ilitoa wabunge watatu ie MNYIKA,(kijana) MDEE(kijana Mwanamke) na MPENDAZOE (awali alikuwa Kishapu via CCM - Ingawa alichakachuliwa)
  • M4C haijapita Dar hata tuka evaluate mwitikio wao
  • etc
 
Wakazi wa Dar wanaelewa vizuri kuwa wanasiasa ni sawa na wafanyabiashara tu, wote wanatafuta pesa, umaarufu na sifa. Tofauti ni kuwa mfanyabiashara anauza bidhaa na huduma, mwanasiasa anauza maneno, ahadi na uongo.

Tumekataa kuwa wateja wa wanasiasa. Tofauti ya CCM, Chadema, CUF, TLP, UDP n.k ni sawa na tofauti ya biashara ya mafuta, vifaa vya ujenzi, duka la mapambo, saloon n.k Chapa kazi, hakuna mwanasiasa atakaekuletea maendeleo kwa hapa kwetu. Ndio ajira zao hao
 
ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la dar es salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa tanzania kwani dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela? Wakazi wa dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya udaku kama mambo ya kanumba, lulu, wema, diamond, johari, jokate. Ubitozi na usharobaro kwa kwenda mbele.
Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama dar, wakazi wa dar badilikeni.....!!!!

mageuzi ya kweli hutoka moyoni mkuu na wala si suala la kuiga. Dar es salaam ina watu toka sehemu tofauti nchini na matatizo yao yaonekana kutowaingia mioyoni mwao kama sehemu nyingine zenye watu wenye uchungu na maeneo yao kama vile arusha/arumeru na matatizo ya ardhi/maji kanda ya ziwa na uamko halisi wa kutaka maendeleo yaliyo sawa na kanda zilizoendelea zaidi yake nk.
 
Nadhani umri wako ni mdogo siwezi kukulaumu hivi unajua kuwa Dar ndio kila kitu ndio chimbuko la siasa za mageuzi Tanzania wewe unadhani siasa zimeanza baada ya Lema kushinda Arusha...fuatilia mdogo wangu historia ya Dar es Salaam.
leo umefunguka big up
 
Safi sana Dar muendelee hivyo hivyo kupinga hao wavunja amani wa nchi, endeleeni kuchagua chama makini(CCM).
.
"WASIOSOMA NI CHAKULA CHA WASOMI".
 
ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la dar es salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa tanzania kwani dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela? Wakazi wa dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya udaku kama mambo ya kanumba, lulu, wema, diamond, johari, jokate. Ubitozi na usharobaro kwa kwenda mbele.
Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama dar, wakazi wa dar badilikeni.....!!!!

Natumai pia naamini hauko sahihi, mwamko wa mageuzi ni mkubwa sana dar, mfano kiduchu ni ofisini kwangu tuko kama 300 ivi ccm ni km 2% ya wote tatizo naloliona dar hatulindi kura zetu.

Majuzi umefanyika uchaguzi wa udiwani vijibweni hatukulinda kura zetu ccm wakaweza kuzichakachua (pia watu toka temeke walikuja na kuipiga kura ccm) ivo mgombea wetu wa chadema akashindwa lkn ukweli ndo alokuwa ameongoza ata ccm wanalijua ilo na kulikubali kwani kampeni zao ccm zilidolola sana yani hawakuungwa mkono kabisa.

Ata wakati wa ubunge mama komu wa cdm alishindwa kwa margin ndogo wakati vituo vingi tu hakukuwa na mawakala wa cdm hii ni wazi kama kawaida yao ccm walifanya kweli.

Hayo ni machache tu.

My take: Viongozi wa chadema dar waache tabia za kuonekana wakati wa kampeni tu, wajipange wazunguke kila kona hasa mda huu wa m4c waamasishe kuwa wanachama hai pia jinsi ya kuzilinda kura zao nakuhakikishia mabadiliko makubwa na ya ajabu yatatokea dar asa
 
You're absolutely right. Dar people are obsessed with nonsense issues like the likes of Kanumba and many more. They keep busy in the name of searching for money and yet they're poor.

They don't sit down and dig deep to know the sourse of their poverty. Up country people have known that and now they are eager for change. Once freedom comes then I think the capital city must be shifted to any of the serious region from these LAZY Dar dwellers.
 
Nadhani umri wako ni mdogo siwezi kukulaumu hivi unajua kuwa Dar ndio kila kitu ndio chimbuko la siasa za mageuzi Tanzania wewe unadhani siasa zimeanza baada ya Lema kushinda Arusha...fuatilia mdogo wangu historia ya Dar es Salaam.
Kuanzisha vita si issue ! issue ni kupigana vita hadi ushinde! Dar mageuzi yameanzia huko fine mbona hamkuyaendeleza??mmekaa tu kimya mambo ya hovyo hovyo yanafanyika hajuwahi kusikia hata mkitishia kwenda ikulu ambayo mpo nayo huko! wanaharakati juzi wakati wa mgomo wa madaktari waliandamana hamuwaunga mkono! amkeni acheni kulala!!
 
Haa haaa haaaa! Dar es Salaam watu hawana akili za kushikiwa mwambie aje halafu aitishe mkutano ndio atajua labda aende Kimara..

wewe ni debe tupu hujui siasa afadhali ujiunge na vikundi vya taarabu!!
 
Lema anatinga huko kuwaamsha waliolala
Dar Jimbo ambalo bado litaendelea kusumbuwa mabadiliko ni jimbo la Ilala lililojaa Wahindi na Waswahili kama Faiza Foxy na jimbo la Kinondoni lililojaa makahaba, mafuska, mateja, wezi, Matapeli, Wasanii na kila aina ya machukizo machoni pa Mungu.

Jimbo la Kinondoni wengi wao hawaoni hata umuhimu wa kuwepo Serikali na ingewezekana kwa amri yao basi Rais wa Ngwasuma ndiyo huyo huyo angekuwa Rais wa Nchi.

Majimbo yaliyobaki kama Kawe na Ubungo hapa somo linaeleweka vyema, Temeke na Kigamboni, wakazi wake wengi ni wandengereko na wamatumbi, Uislamu na uswahili ni sehemu ya advatage ya kushinda jimbo hili.

Ukonga na Segerea ni majimbo ambayo yapo kibla ni Chadema tu inayopaswa kujenga mtandao imara ili kuyachukuwa majimbo haya mawili, hakuna tatizo lolote kwenye haya majimbo.
 
You're absolutely right. Dar people are obsessed with nonsense issues like the likes of Kanumba and many more. They keep busy in the name of searching for money and yet they're poor. They don't sit down and dig deep to know the sourse of their poverty. Up country people have known that and now they are eager for change. Once freedom comes then I think the capital city must be shifted to any of the serious region from these LAZY Dar dwellers.
You are absolutely right!
 
siamini kihivyo kwa sababu;
  • Dar ilitoa wabunge watatu ie MNYIKA,(kijana) MDEE(kijana Mwanamke) na MPENDAZOE (awali alikuwa Kishapu via CCM - Ingawa alichakachuliwa)
  • M4C haijapita Dar hata tuka evaluate mwitikio wao
  • etc

UKO SAHIHI SANA Duble Chris, HUO NDO UKWELI
 
Back
Top Bottom