Wakazi dar na changamoto ya mafuriko!!!!

Aug 10, 2011
81
9
Nasikitika sana na hali ya mafuriko yanayotokea katika jiji la Dar,hii si mara ya kwanza au ya pili hali hii kutokea lakini baada ya mafuriko wananchi husahau na kuendelea na shughuli zao kama hakuna kitu kilichotokea. Ajabu na la kushangaza zaidi baada ya muda viongozi wa serikali na chama huja na kuongea blabla basi mambo yanaisha. Najiuliza kwanini wakazi wa Dar hawaombi suala la miundombinu ya jiji katika kupeleka maji machafu na maji ya mvua? wameridhika na hali hii? jiji linaendesha miradi mingi tu ya maghorofa makubwa na marefu mbona hakuna hata mwananchi anayelalamika kuhusu miundombinu ya maji? Je Dar wakazi wake wamezoea kuishi na uchafu au harufu mbaya kila kona huku wakiwaangalia watawala wetu na viongozi waliowapa dhamana wakiwa kwenye magari ya viyoyozi raha mstarehe? Dar nani kawaloga?
 
Mkuu bas bas mana mi nkifikiriaga nataman kulia,yani maafisa mipango miji cjui kaz yao nin?Au ndo walewale wakata utepe kama....!?
 
Naunga mkono hoja. Mstahiki meya, mkuu wa mkoa, wizara ya miundombinu na mabwanyenye TANROADS wanafanya kazi gani. Je tunapimaje utendaji wao wa kazi kama haya yako chini yao na wameshindwa kutenda kila kitu wanasingizia ukosefu wa fedha mbona maghorofa yao na maguest house wanayomiliki hawasemi bajeti ni ndogo. Ni kwanini barabara zinajaa maji, lami inavimba mashimo makubwa ni nani awajibike?
 
Back
Top Bottom