Wakati umefika wa CCM kugawanyika

Raia Fulani

JF-Expert Member
Mar 12, 2009
10,877
2,756
Kuna mambo mengi yanaendelea hapa nchini ambayo tunaweza kuyachambua na mengine kuonekana kwa wachache ambayo yote haya yanaumiza nafsi za watanzania wengi. Nikitaja madudu hapa sitamaliza ila wenzangu mnajua, tena zaidi kuliko mimi. Nimewahi kusema wakati flani kuwa mzalendo wa kweli ni yule mwenye sifa kuu mbili. kwanza uwezo wa kujibainisha, pili awe na dhamira iliyo hai. vingine ni mbembwe tu. sasa basi, haya yote yamefika hapa kwa uongozi 'imara' wa CCM. ndani ya chama kuna waadilifu wachache kama Sitta na kundi lake. Ili usemi wa baba wa Taifa utimie, LAZIMA hawa watu wajitoe ndani ya chama na kuangalia mistakabali wa taifa kwa mapana na uzalendo zaidi. kuendelea kubaki na kukubali kunyamazishwa huku ukijifanya unaumia ni unafiki tu! Mbona hawa viongozi wetu wanaogopa changamoto? Au siasa ndio ajira? Bila siasa mtu hawzi ishi? Bila CCM hakuna maisha? Obama alisema YES WE CAN! Na wao wanaweza kujiengua na kufanya mambo ya maana zaidi. Tunataka Tanzania mpya 2010 na kuendelea. Naomba kuwasilisha hoja!
 
kaka mi nakubaliana na wewe 100%
kila kitu kinamwisho, nahisi huu unaweza ukawa mwisho wa ccm.
 
hivi kipi,o cha uadilifu nini bwana mziwanda?

kipimo cha uadilifu bwana ni matendo yako mkuu. dhamira iliyo hai inayokusuta pale unapotenda kinyume. uwe na uwezo wa kuvaa hali ya mtu mwingine na kujiuliza itakuwaje kama nikiwa yeye? ukishajijibu maswali hayo kisahihi, basi huo ni uadilifu
 
SITTA hana lolote bado anahofuu kubwa ya maisha yake bila kuwa CCM..Ni unafiki usiokuwa na KIPIMOOOOO...
 
SITTA hana lolote bado anahofuu kubwa ya maisha yake bila kuwa CCM..Ni unafiki usiokuwa na KIPIMOOOOO...

thats y nikasema ni unafiki kuendelea kulamba miguu ya wakubwa kwa kuogopa changamoto
 
Akina Seif na wenzake waliachana na ufuasi wa Sultani CCM walipotakiwa kufanya hivyo na Mwalimu Nyerere ili kama wanapingana na maamuzi ya chama basi wapinge wakiwa nje ya CCM na hadi leo wapo nje ya CCM na mambo yao si mabaya tatizo kuna watu wanaiabudu CCM na kuona bila ya CCM hawana wa kuwapa riziki.

Watu kama hao huna la kuwambia wakaachana na CCM ,kwa wanavyoiabudu CCM hata wakiambiwa wavue watavua.
 
Kuanguka kwa ukomunisti uko Urusi(USSR) miaka ya 1990 na hatimaye kumeguka kwa nchi hiyo kulitoka na kile kitu kinaitwa "contradictions" katika mfumo wa kisoshalisti uliokuwa umetawala tangu mapinduzi ya 1919 (kama sikosei) chini ya Lenin. Utaona kwamba huu ni muda mrefu ni kama miaka 70 na ushee.

CCM ilianza kuwa na contradictions za ndani hasa pale ilipoamua kulitosa azimio la Arusha kule Zanzibar chini ya uongozi wa mzee Ruksa. Kwenye msafara wa Mamba pekee Kenge wakaanza kujipenyeza na matokeo yake ni tabaka kuanza ndani ya chama na hatimaye ndani ya nchi.

Contradictions hizo zilijitokeza zaidi katika mchakato wa urais ndani ya CCM 2005 ambapo kwa mara ya kwanza kulikuwa na ushindani mkubwa uliogubikwa na matumizi makubwa ya pesa, rushwa, ubaguzi wa rangi na hila mbali mbali. Mchakato ule wa ndani ya CCM uliacha ufa mkubwa. Kwa vile uongozi wa CCM haukujali kuziba "ufa" ule matokeo yake ukuta sasa unaanza kubomoka!

Kilichofanywa na NEC juzi ni "blunder" moja kubwa sana kama Bunge lilivyomfukuza Zitto Kabwe mwaka jana. Nafasi ya Usipika ni kubwa sana na Bunge ni moja ya muhimili wa dola. NEC haikumdhalilisha Sitta pekee lakini ndani ya mitima yao (deep down) wanajua wamewadhalilisha wabunge kwa ujumla kwa kisa ambacho kiiini chake hasa ( hata kama hili halisemwi) ni Richmond! Ndio maana NEC imeunda tume ya Rais Mstaafu Mwinyi kujaribu kuweka mambo sawa. Tusibiri tuone lakini CCM haiwezi kuwa kama zamani tena (CCM will never be the same).

Kwa nini nasema hivyo? Ni kwa sababu ya utandawazi hata wana CCM hususani wabunge wakizibwa midomo nje ya vikao hakuna siri tena kama tunavyoona kwenye JamiiForums. Wakifanya usiku, asubui mambo yanakuwa hadharani! Kwa hali hii hata kama CCM haitaki kutambua na kukubali kwamba inameguka taratibu lakini pole pole inaelekea uzeeni huku ikiandamwa na "magonjwa" lukuki (ufisadi, mahakama ya kadhi na IOC, waraka wa kanisa, mamlaka ya Zanzibar, Muafaka wa Zanzibar na sasa mvutano katika Bunge) na wote tunajua matokeo ya uzee: KIFO
 
SITTA hana lolote bado anahofuu kubwa ya maisha yake bila kuwa CCM..Ni unafiki usiokuwa na KIPIMOOOOO...

Mwingine huyu wa kambi ya ufisadi kaajiriwa ili kuwapaka wote wale ambao wanajaribu kupambana na mafsadi ndani ya chama na serikali. Wewe unafiki wako wa kuwapigia debe mafisadi huoni!!!
 
Haya yalitabiriwa na marehemu Kolimba (Mungu amrehemu) kipindi hicho. CCM ingekuwa macho ingezinduka na kufanya mambo yake kwa mtazamo mpya lakini wapi! Sio kwamba tunaichukia CCM bali yale yanayotendwa na wale walio chamani. Watu hamsini waadilifu ndani ya chama hicho hawawezi kutushawishi tukakipenda. Vuguvugu la kweli linahitajika hapa badala ya kung'ang'ania hii hali tete itakayotupeleka pabaya wakati fulani mbeleni. Tusidanganyike kuwa mataifa mengine yanaitamani hii hali ya 'utulivu' tuliyo nayo. wanajua dhahiri kuwa ni kiini macho tu na ni sawa na moto wa pumba. ili tusifike huko, CCM aidha ijipange KIZALENDO ama wale wazalendo wajitoe tu. mtaona watu watakavyotapatapa
 
Wana Great Thinker,
Kwa maoni yangu na ushauri wangu kutokana na hii mada/topic, mimi naona tatizo lipo kwenye Katiba ya Nchi, naona Katiba inampa Nguvu na Madaraka makubwa Rais ambaye ndie Mwenyekiti wa Chama ambacho kinatawala.
Tunapaswa kuwa na Katiba ambayo inawapa wananchi nguvu ya kuwawajibisha Viongozi, hata Rais asipo/wasipo fanya kazi au kutimiza wajibu wao. Bado tuna kazi kubwa ya kubadilisha Katiba kutoka Mfumo wa chama kimoja kwenda Vyama vingi ingawa Katiba yetu tunaiwekea viraka hapa na pale.
Uoga wa viongozi wetu wa kutoa maoni, ushauri kwa kuhofia Usalama wao na familia zao na biashara zao na mali zao, na kufanya Siasa kama ni njia ya kutafuta ulaji, ili mradi mkono uende kinywaji.
 
Wana Great Thinker,
Kwa maoni yangu na ushauri wangu kutokana na hii mada/topic, mimi naona tatizo lipo kwenye Katiba ya Nchi, naona Katiba inampa Nguvu na Madaraka makubwa Rais ambaye ndie Mwenyekiti wa Chama ambacho kinatawala.
Tunapaswa kuwa na Katiba ambayo inawapa wananchi nguvu ya kuwawajibisha Viongozi, hata Rais asipo/wasipo fanya kazi au kutimiza wajibu wao. Bado tuna kazi kubwa ya kubadilisha Katiba kutoka Mfumo wa chama kimoja kwenda Vyama vingi ingawa Katiba yetu tunaiwekea viraka hapa na pale.
Uoga wa viongozi wetu wa kutoa maoni, ushauri kwa kuhofia Usalama wao na familia zao na biashara zao na mali zao, na kufanya Siasa kama ni njia ya kutafuta ulaji, ili mradi mkono uende kinywaji.

mkuu unadhani kwa mchakato wa katiba unaoendelea kuna jambo jema lolote mbele?
 
Magamba igawanyike mara ngapi bana!!!? we husikii Lowassa ana kundi lake, Membe ana kundi lake, Mkapa ana kundi lake, Sitta ana kundi lake. Magamba imeshagawanyika miaka mingi iliyopita.
 
thats y nikasema ni unafiki kuendelea kulamba miguu ya wakubwa kwa kuogopa changamoto

siyo unafiki, wale wazuri wachache waliopo CCM wanafikiri muda bado wana matumaini ya kuibadilisha CCM ambayo bado ni chama makini kiitikadi na kinadharia. Haya matumaini bado ni makubwa kiasi fulani, lakini yakianza kufifia kabisa katika miaka miwili ijayo maamuzi mazito yatachukuliwa...kinachoiunganisha CCM sasa hivi ni matumaini kama haya waliyonayo makundi yote ndani ya CCM. Nyerere alisema wapinzani wa kweli watatoka CCM..tukae tusubiri
 
Magamba igawanyike mara ngapi bana!!!? we husikii Lowassa ana kundi lake, Membe ana kundi lake, Mkapa ana kundi lake, Sitta ana kundi lake. Magamba imeshagawanyika miaka mingi iliyopita.
Kwa hiyo tusubiri kusambaratika sio?
 
siyo unafiki, wale wazuri wachache waliopo CCM wanafikiri muda bado wana matumaini ya kuibadilisha CCM ambayo bado ni chama makini kiitikadi na kinadharia. Haya matumaini bado ni makubwa kiasi fulani, lakini yakianza kufifia kabisa katika miaka miwili ijayo maamuzi mazito yatachukuliwa...kinachoiunganisha CCM sasa hivi ni matumaini kama haya waliyonayo makundi yote ndani ya CCM. Nyerere alisema wapinzani wa kweli watatoka CCM..tukae tusubiri
Red
Miaka 50 bado unasema tuamini katika nadharia za ccm na itikadi zake? Hapo umechemsha. Au una tafsiri nyingine ya nadharia?

Black
Hata kina Dr Slaa Wametokea ccm, hivyo tayari kuna upinzani wa kweli ambao chimbuko lake ni ccm
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom