nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
WAKATI KIPROTICH AKIIBUKA NA SHILINGI MILION 200 UGANDA KWA KUSHINDA MEDALI OLIMPIKI, WASHIRIKI WA TANZANIA WAREJEA NA VISINGIZIO.
- 16 August 2012
Rais Yoweri Museveni wa Uganda ameiagiza Wizara ya Elimu na Michezo nchini humo kuhakikisha wanamichezo wa Uganda wanaoshinda medali katika ngazi ya Afrika na zaidi ya hapo wanapata usaidizi kutoka serikalini na pia kupatia ajira katika taasisi za serikali haswa Jeshi, Polisi, Magereza, Mamlaka ya Wanyamapori na Idara za Usalama.
Museveni pia ameagiza Wizara hiyo kujenga kituo cha kisasa cha mafunzo cha michezo katika eneo la Sebei ndani ya mwaka mmoja na kusema wanamichezo walioajiriwa na serikali wanatakiwa kupewa muda zaidi wa kufanya mazoezi mbali majukumu yao ya kazi.
Rais Museven alimkabidhi mshindi wa medali ya dhabu katika michezo ya Olimpik Stephen Kiprotich hundi ya shilingi milioni 200 na kuamuru fedha hizo ziwe zimeingia kwenye akaunti ya siku hiyo hiyo.
MO BLOG: Wanamichezo wa Tanzania hongereni kwa kushiriki; lakini kusema ukweli kamati nzima ya Olimpiki ya Tanzania mnajisikiaje? Mtatoa sababu mpaka lini? Kuacha kutalii na Mizigo.
Hizo pesa ni sawa na $ 80,000 ni zaidi ya Wamarekani wao ukipata Gold wanapewa $ 25,000
Wapendwa Wamerudi Mizigo Kibao; Wametakata Walishiriki nusu siku wakakaa London siku 18 Mapumzikoni