Mallaba
JF-Expert Member
- Jan 30, 2008
- 2,554
- 47
Akihutubia maelfu ya wakazi wa Musoma, Zitto alisema kuwa lengo la kufanya ziara katika Jimbo la Musoma ni kutaka kuhamasisha wakazi wa mji huo kumchagua mgombea ubunge wa Chadema, Vincent Nyerere katika Uchaguzi Mkuu ujao.
Wakati Dk Slaa anatafuta kura za urais mimi nimeamua kuzunguka Tanzania kutafuta wabunge ambao tutaweza kufanya nao kazi ili kutetea maslahi ya Watanzania na kati ya wabunge ninaowahitaji mmojawapo ni Vincent Nyerere, alisema Zitto huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu.
Alisema ili Watanzania waweze kuondokana na umasikini uliokithiri miongoni mwao hawana budi kufanya mabadiliko ya uongozi ambapo alidai kuwa chama pekee kinachoweza kuwakomboa ni Chadema.
Zitto alisema kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita chama hake kimeweza kuibua kashfa mbalimbali, lakini wahusika hawajakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola.
Bila Chadema msingejua mambo yaliyofanywa Benki Kuu, bila Chadema msingejua Richmond na ilitakiwa watu hawa wachukuliwa hatua. Naomba safari hii mtupatie dola, Jeshi na Mahakama tuwatumikie kwa uadilifu , alifafanua Zitto.
Zitto aliwaomba wananchi kukichagua chama chake ili watuhumiwa wote waweze kuchukuliwa hatua za kisheria kazi amabyo alidai kuwa haiwezi kuifanywa na CCM.
Watu wa Musoma, siamini macho yangu tangu nianze kuzunguka sijahutubia watu wengi kiasi hiki, hivyo nawaomba kwa kutumia uwingi huu mkipigie kura Chadema katika Uchaguzi Mkuu ujao ili tuweze kuwatumikieni na hatimaye kufaidi maliasili zilizopo nchini, alisema Zitto.
Akizungumzia sula la vurugu katika zoezi zima la kampeni mjini hapa, Zitto alilitaka Jeshi la Polisi mkoani hapa kufanya uchunguzi wa haraka na
kuhakiskisha kuwa watu wanohusika katika vurugu hizo wanafikishwa katika vyombo vya sheria.
Zitto alisema amesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu kujichukulia sheria mkononi kwa kuwakata watu mapanga kwa ajili ya kura hali amabyo alisema kuwa inatishia amani na usalama wa wakazi wa Musoma na Tanzania kwa ujumla.
Namtaka RPC, OCD na RCO kufanya uchungzi wa haraka na kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanakamatwa na wanafikishwa katika vyombo vya sheria ili sheria ichukua mkondo wake, hatuwezi kuwamaga damu kwa ajili ya watu wachache wenye uchu wa madaraka, alisema.
read more here
Wakati Dk Slaa anatafuta kura za urais mimi nimeamua kuzunguka Tanzania kutafuta wabunge ambao tutaweza kufanya nao kazi ili kutetea maslahi ya Watanzania na kati ya wabunge ninaowahitaji mmojawapo ni Vincent Nyerere, alisema Zitto huku akishangiliwa na umati mkubwa wa watu.
Alisema ili Watanzania waweze kuondokana na umasikini uliokithiri miongoni mwao hawana budi kufanya mabadiliko ya uongozi ambapo alidai kuwa chama pekee kinachoweza kuwakomboa ni Chadema.
Zitto alisema kwa kipindi cha miaka mitano iliyopita chama hake kimeweza kuibua kashfa mbalimbali, lakini wahusika hawajakamatwa na kufikishwa katika vyombo vya dola.
Bila Chadema msingejua mambo yaliyofanywa Benki Kuu, bila Chadema msingejua Richmond na ilitakiwa watu hawa wachukuliwa hatua. Naomba safari hii mtupatie dola, Jeshi na Mahakama tuwatumikie kwa uadilifu , alifafanua Zitto.
Zitto aliwaomba wananchi kukichagua chama chake ili watuhumiwa wote waweze kuchukuliwa hatua za kisheria kazi amabyo alidai kuwa haiwezi kuifanywa na CCM.
Watu wa Musoma, siamini macho yangu tangu nianze kuzunguka sijahutubia watu wengi kiasi hiki, hivyo nawaomba kwa kutumia uwingi huu mkipigie kura Chadema katika Uchaguzi Mkuu ujao ili tuweze kuwatumikieni na hatimaye kufaidi maliasili zilizopo nchini, alisema Zitto.
Akizungumzia sula la vurugu katika zoezi zima la kampeni mjini hapa, Zitto alilitaka Jeshi la Polisi mkoani hapa kufanya uchunguzi wa haraka na
kuhakiskisha kuwa watu wanohusika katika vurugu hizo wanafikishwa katika vyombo vya sheria.
Zitto alisema amesikitishwa na kitendo cha baadhi ya watu kujichukulia sheria mkononi kwa kuwakata watu mapanga kwa ajili ya kura hali amabyo alisema kuwa inatishia amani na usalama wa wakazi wa Musoma na Tanzania kwa ujumla.
Namtaka RPC, OCD na RCO kufanya uchungzi wa haraka na kuhakikisha kuwa watuhumiwa wanakamatwa na wanafikishwa katika vyombo vya sheria ili sheria ichukua mkondo wake, hatuwezi kuwamaga damu kwa ajili ya watu wachache wenye uchu wa madaraka, alisema.
read more here