Tosha
Member
- Aug 18, 2011
- 72
- 19
Wanabodi kama tujuavyo Raisi Jakaya Kikwete amealika taasisi mbalimbali na wadau wampelekea mapendekezo ya majina ya watu ambao atafikiria miongoni mwao awateuwe wawe wajumbe wa Tume ya kukusanya maoni na kuandika rasimu ya katiba mpya! Nadhani haitakuwa vibaya kama tukijadili na kupendekeza nani anatufaa katika tume hii sauti zetu zina maana sana hata kama hatutapeleka rasmi lakini wengi wanatapita na kusoma humu hviyo naamini watatusikia tu.
Tume inahitaji watu MAKINI, WASIKIVU na WANAOJALI MASLAHI ya TAIFA. Kwa kuanza napendekeza wafuatao ambao sio wabunge na nadhani kati yao wangefikiriwa watatusaidia katika kuyajari maslahi mapana ya taifa letu :
Katiba ni jukumu letu sote tujenga misingi ya sasa na ya baadaye!tuna nafasi ya pekee sana ambayo HISTORIA haitacha kutusahau na kutuhukumu.
Je wewe mdau ungependa nani awemo katika kamati ya katiba?
Tume inahitaji watu MAKINI, WASIKIVU na WANAOJALI MASLAHI ya TAIFA. Kwa kuanza napendekeza wafuatao ambao sio wabunge na nadhani kati yao wangefikiriwa watatusaidia katika kuyajari maslahi mapana ya taifa letu :
- Wanahabari: Ayubu Ryoba, Hamisi Dambaya, Rosemary Mwakitwange na Joseph Mihangwa
- Wanataaluma: Prof. Chris Peter Maina, Mugongo Fimbo, Dr. Masumbuko Lamwai, Dr. Frola Kessy, Dr. Vicensia Shule, Dr.Honest Prosper Ngowi na Bashiru Ally
- Asasi za Kiraia: Jefred Myenzi, Usu Mallya, Ananelia NKya…
- Kutoka JF: Pasco wa JF ... Vyama vya Siasa: Prof.Mwasiga Baregu, Dr. Sekondo Mvungi na Prince Bagenda…
- Wanamichezo: Filbert Bayi…
- Wanasanii: Chemudu Ngwao, Irine Sanga na John Kitime…
- Viongozi wa Dini: Sheikh Mkuu wa Dar es Salaama-alhad Mussa Salum, Pd.Stevene Kaombwe
- Walemavu(physical challenged):...
- Wafanyabiashara:...
- Wanafunzi:...
- Wafanyakazi:..
- ...
Katiba ni jukumu letu sote tujenga misingi ya sasa na ya baadaye!tuna nafasi ya pekee sana ambayo HISTORIA haitacha kutusahau na kutuhukumu.
Je wewe mdau ungependa nani awemo katika kamati ya katiba?