Waislamu wote kushiriki Sensa - Mufti

Mufti Issa Shaaban Simba, Sheikh Mkuu wa Tanzania ametoa kauli murua kabisa ya kama kiongozi wa BAKWATA.

Sensa ya mwisho ya 1967 iliyokuwa ina harufu za kikoloni kutugawa kwa makundi ya dini, kabila haina mashiko mwaka huu 2012. Hivyo kama kuna taasisi au mtu anayetumia takwimu za mwaka 1967 ni vizuri kuainisha kuwa ni miaka 45 tangu sensa ya mwisho iliyokuwa na vipengele vya dini na haina mashiko sasa.

Serikali, taasisi na watu binafsi sasa ni wakati wa kusonga mbele na kuachana na kutaka kujua dini ipi ina idadi ya watu wangapi hilo tuwaachie taasisi zao za dini kufanya jambo kwani serikali haina dini.

Wapo watakaopingana na Mufti Issa Shaaban Simba, mfano watakaosema mbona Uingereza ktk sensa yao wanataka kujua dini ya mtu hivyo nasi tuige. Uingereza ni nchi ya Kikristo (Church of England), Malkia/Mfalme ni Kiongozi mkuu wa Church of England, bendera ya England ina symbol ya Msalaba na tumeona ktk Euro 2012 football competition washabiki wa England wamebeba bendera yenye Msalaba kuainisha kiaina kuwa ni nchi ya mfumo Kristo.

Uingereza wanataka kujua dini ya wakaazi wa Uingereza kwa vile wakaazi wenye dini nyingine kama Uislamu, Uhindu, Budhha n.k ni watu wenye rangi, desturi tofauti na Waingereza asilia (Asilimia zaidi ya 90 ya wakaazi wa Uingereza ni watu weupe wanaojibainisha na Ukristo hata kama si waumini wa kwenda Kanisani).


Sisi Tanzania asilimia 99 ya wakaazi wa Tanzania ni wa rangi nyeusi, mila na desturi zinaingilia kwa sana hivyo hatuna haja ya kuwa na kipengele cha dini ktk sensa kuwatambua watu wa dini nyingine (Rangi) kama Uingereza, sisi hatuna hofu ya wageni wa rangi nyingine (dini nyingine) kubadilisha U-Tanzania wetu.


Mufti Issa Shaaban Simba, Sheikh Mkuu wa Tanzania na BAKWATA wanastahili kupewa pongezi kwa kufunguka kwa staili ya umoja wa Tanzania kwanza na pia wadau wote kuwa makini na kutumia takwimu za sensa zilizopitwa na wakati kama sensa ya mwaka 1967 yenye harufu ya kasumba ya mkoloni kutugawa.
 
Naunga mkono kauli ya Mufti kwani kama ndugu zangu wanamalalamiko yeyote sehemu husika ya kuonyesha hasira ni kwenye mchakato wa katiba na si kususia sensa.
 
Huyo ni Mufti wa waislam au Mufti wa Bakwata?

Pasi na shaka ametoa tamko Hilo amewaomba wana Bakwata wenzake.

Hivi ule unafiki unaokatazwa na dini ya kiislam una mipaka gani?

Kwa mfano wewe, kuna wakati watu wote wenye majina ya kiislam unawaita waislam (Remember Mohamed Said's thread?) na sasa kuna hawa walioko ndani ya Bakwata na wana majina ya kiislam, pamoja na Mufti wao, je leo hii sio waislam? Sio unafiki huo?
 
Baraza la bakwata latoa tamko kuwataka waumini kushiriki katika sensa ya mwaka huu ili kuiwezesha serkali kuendelea kuboresha mahitaji ya watanzania,pia sheikh mkuu amewaambia waendelee kutetea mambo yao ya msingi

Nawaheshimu sana viongozi wote wa dini au makundi yoyote yale, wanaoona busara ya sisi watanzania wote bila kujali dini zetu, makabila yetu na maeneo tutokayo, kuishi kwa kuelewana, kushirikiana na kuvumiliana katika mambo tunayotofautiana. Kwa vyovyote watu wengine watakavyosema, lakini Simba kama kiongozi wa jamii ya kiislam ametoa kauli ya busara.

Ombi langu kwa waislam, msikubali kuongozwa na watu wenye kuchochea utengano wa jamii yetu, maana ni kwa kuwa na viongozi hao, husababisha uislam kudhihakiwa au kutukanwa. Tufikirie na kutatua matatizo yetu kama watanzania na siyo kama watu wa vikundi fulani. Unyonge na shida za watanzania hazichagui dini wala kabila bali huwapata watanzania wote, tunahitaji juhudi za pamoja kuweza kuzishinda. Hakuna atakayeshinda kwa vile ni mkristo, muislam au mpagani bali kwa umoja wetu kama watanzania.
 
Mufti ametangaza kupitia TBC1 na amewataka Waislam Kukubali kuhisabiwa.

Mnavyomtaja MUFTI wa TANZANIA unaitaja serikali ya Tanzania
Hata siku moja hajawahi kusimama na akatetea wazi wazi maslahi ya waislamu katika nchi hii.
YEYE NI SEHEMU YA SERIKALI NA BAKWATA YAKE
 
attachment.php
 
Hivi ushawahi kuona Dr.Ulimboka anaandama kutetea maslahi ya walimu?? Bila shaka noo, ni kazi ya Mukoba hiyo kiongozi wao. Sasa huyu mufti simba yeye ni kiongozi wa waislamu hata siku moja atetee maslahi ya waislamu hakuna sasa huyu kiongozi wao au kibaraka wa serikali?? Na serikali wanajua huyo zuzu na kichwani hamba elimu ndio mana anaburuzwa, kwa bahati mbaya sana wazee wachache ndio wanaomsikiliza but majority ya waislamu wanamuona kituko kwa u-puppet wake
 
Bila kutanguliza utanzania wetu, umoja, mshikamano, tukaweka hekima pemben, iman na din zetu ni bure wala hazina maana.

Mgawanyiko wa kimakundi na itikadi tukichochewa na wanasiasa bila sisi kujijua ni hatari inayolinyemelea taifa letu na kwa kasi kubwa tunaelekea kuzim.

Waislam hawapaswi kwa maana yoyote kumtafuta mchawi miongoni mwao. Wasikubali kugawanywa na kirahisi wakagawanyika, wakachukiana na hata kutengana.

Kwanza ilikuwa mfumo kristo, ikaja cdm chama cha kidin, na sasa bakwata na makundi ya waislam. Nin maana yake? Kwa nin?

Adui no-1 wa yote haya ni ccm na serikali yake. Baada ya kuwachochea wanainchi kuichukia chadema kwa misingi ya ukanda, ukabila na udin sasa ni zam ya wislam kugawanywa kwa malengo yale yale- wapate kuendeleza utawala wao kwa urahisi zaid.

Shekhe mkuu yupo sahihi, tuhesabiwe. Kama waislam msipotafakali kumtambua adui wa wote yaani serikali, basi mtafaruku na kutifuana kutazaa Bakwata nyingine, nahapo nikupotea zaidi.

Kushindwa kwa sera za ccm kutukomboa na umaskin..
 
Mnavyomtaja MUFTI wa TANZANIA unaitaja serikali ya Tanzania
Hata siku moja hajawahi kusimama na akatetea wazi wazi maslahi ya waislamu katika nchi hii.
YEYE NI SEHEMU YA SERIKALI NA BAKWATA YAKE

hii ni hatari mnapingana wenyewe kwa wenyewe na kuitana makafiri,kiasi cha kudharau viongozi wenu wa ngazi za juu. Leo mnasema mufti anatumikia serikali,bakwata ya serikali. Kesho sijui mtakuja na gia gani.!
 
Huyu mufti ni muelewa sana na amesema haoni sababu ya waislam kugomea sensa.

Kwa matamshi ina maana sheikh ponda alikurupuka sana.

Na washauri waislam kuiga na kufuata na kumsikiliza mufti .
Takwimu za watu ni pamoja na idadi yao, taarifa zao pamoja na maeneo wanamo toaka swala la dini na makabila ni muhimu kwani kama sio muhimu mbona kwenye baadhi ya taasisi za kiserikali ( kwenye form za kujiunga na shule za sekondary ( form5) hata mm nilijaza ) vipengele hivyo vimo sasa iweje visiwepo kwenye sensa
kama ni kwaajili ya kupanga miradi ya maendeleo je nikwanini miradi hiyo haiwanufaishi walio wengi (masikini) miradi mingi inawanufaisha vigogo na ipo pale kwa maslahi yao
 
Hivi ushawahi kuona Dr.Ulimboka anaandama kutetea maslahi ya walimu?? Bila shaka noo, ni kazi ya Mukoba hiyo kiongozi wao. Sasa huyu mufti simba yeye ni kiongozi wa waislamu hata siku moja atetee maslahi ya waislamu hakuna sasa huyu kiongozi wao au kibaraka wa serikali?? Na serikali wanajua huyo zuzu na kichwani hamba elimu ndio mana anaburuzwa, kwa bahati mbaya sana wazee wachache ndio wanaomsikiliza but majority ya waislamu wanamuona kituko kwa u-puppet wake

alichaguliwa na nani km kichwani hakuna elimu? Vp wapga kura wake? Chekechea?
 
Hii yote ni TBC ,waislam tulitulia,ila karibu tasisisi zate za Umma zinendeshwa kwa mfumo kristu,mara TBC watuombe radhi mara BARAZA LA MITIHANI watuombe radhi,tuwe makini sana na mabo ya kiroho,kipengele cha dini SENSA NO lakini MAJUMBA yaibada YES hii mushkili sana,waslam 5 wanaweza kuswali msikiti mmoja lkn wakristu mpaka mkanisa 3, wana madhehebu mengi,sisi wengi ni SUNI,kwahiyo wingi wa makanisa utatafsiwa vibaya,cha ajabu POLISI unaulizwa dini gani,USAHILI unaulizwa dini gani,Paspoti unaulizwa dini gani,kujiunga na VYUO unaulizwa dini gani, kama wamebadilisha itakua hivi karibuni,me nilijaza,MAHAKAMANI unaulizwa dini gani?JIULIZENI KAMA SELI
KALI INAGAWA VIWANJA VIPYA NANI ATAFAIDIKA?KWASABABU HAWAJUI WINGI WA WATU KWA IMANI ZAO, WATAANGALIA WINGI WA NYUMBA ZA IBADA,HAPO SASA WATAENDELEA KUTUPIGA CHANGA LA MACHO.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom