Waislamu wote kushiriki Sensa - Mufti

Comi

JF-Expert Member
Oct 2, 2011
3,328
955
Baraza la bakwata latoa tamko kuwataka waumini kushiriki katika sensa ya mwaka huu ili kuiwezesha serkali kuendelea kuboresha mahitaji ya watanzania,pia sheikh mkuu amewaambia waendelee kutetea mambo yao ya msingi
SHEIKH Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba ametoa msimamo wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), akiwataka Waislamu wote nchini kushiriki Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu.

Mufti Simba ameonya kile baadhi ya waislam kufanya uchochezi kwa wananchi ili wasishiriki zoezi la sensa na kusema BAKWATA haihusiki.

Akisisitiza umuhimu wa Waislam kujitokeza kuhesabiwa, Mufti Simba alisema, "Mimi kama kiongozi wa Waislamu natoa wito kwa Waislamu wote hapa nchini, kushiriki kwa ukamilifu katika zoezi la Sensa litakalofanyika nchini mwetu."

Aliongeza: "Katika nchi yetu Sensa zimefanyika nyingi miaka ya nyuma na hazikuhusishwa na dini wala ukabila, ni jambo lililo zoeleka na kukubalika na wote''

Ameonya wale wote wanaochochea waislam kukwamisha juhudi za serikali kwa minajili ya udini.


Source: Mwananchi | Jambo leo | Habari Leo
 
Simba hatishwi kwa kumnyoshea kidole, sasa waseme kwanini wamebatilisha kauli yao ya kususia sensa! Je kile kipengele cha Dini kimewekwa?
Baraza la bakwata latoa tamko kuwataka waumini kushirikia katika sensa ya mwaka huu
 
wakuu hivi kadi za bakwata zinapatikana wapi na nijiunge? Pia nijulushwe vizuri na vikao vya chama pamoja na chaguzi za ndani za chama bila kusahau na katiba ya chama niijue.

Msaada plz..........

Dah... Kaka/dada upo serious kweli?
 
Huyu mufti ni muelewa sana na amesema haoni sababu ya waislam kugomea sensa.

Kwa matamshi ina maana sheikh ponda alikurupuka sana.

Na washauri waislam kuiga na kufuata na kumsikiliza mufti .
 
mimi nilisema miongoni mwao kuna watu wenye akili c kila muislam ni masikini wa kufikiri naona wachache wasiofuta mkumbo na walio na uelewa mpana wametoa mawazo yao na hatimaye masheikh kuelewa maana ya sensa nawapongeza hao wachache
 
wakuu hivi kadi za bakwata zinapatikana wapi na nijiunge? Pia nijulushwe vizuri na vikao vya chama pamoja na chaguzi za ndani za chama bila kusahau na katiba ya chama niijue.

Msaada plz..........

bakwata siyo chama kama unavyofikiria ila ni baraza la kiislam wa tanzania, mwislam yeyote aliyeko tz na yeye pia yumo katika baraza hilo kama yeye si wa upande tofauti kwani kwa sasa hivi waislam wamevunjika vipande vipande kama wakristu ndiyo maana utasikia kuna waabi,alqaeda n.k
 
BAKWATA haijatoa kauli hiyo na huu ni UZUSHI! Mufti Simba hajazungumza tena baada ya kuitaka serikali kuweka kipengele cha dini kwenye sensa. Naomba Mod aitoe hii post ya kizushi. JF si mtandao wa wazushi kama mtoa mada hapo. BAKWATA chini ya Muft wametoa waraka ukisainiwa na muft juu ya kugomea sensa.

Habari hii kuwa BAKWATA wamegeuka ni ya kizushi na haina ukweli wowote na haina msingi zaidi ya kutaka kuwagawa waislam Tanzania.

Kuna kakikundi kanajiita IPF ni ka wanafiki ambako si mara ya kwanza kutumika tunawajua tunawatambua!
 
Mufti ametangaza kupitia TBC1 na amewataka Waislam Kukubali kuhisabiwa.
 
SHEIKH Mkuu wa Tanzania, Mufti Issa Shaaban Simba ametoa msimamo wa Baraza Kuu la Waislamu Tanzania (Bakwata), akiwataka Waislamu wote nchini kushiriki Sensa ya Watu na Makazi itakayofanyika Agosti 26, mwaka huu.

Mufti Simba ameonya kile baadhi ya waislam kufanya uchochezi kwa wananchi ili wasishiriki zoezi la sensa na kusema BAKWATA haihusiki.

Akisisitiza umuhimu wa Waislam kujitokeza kuhesabiwa, Mufti Simba alisema, "Mimi kama kiongozi wa Waislamu natoa wito kwa Waislamu wote hapa nchini, kushiriki kwa ukamilifu katika zoezi la Sensa litakalofanyika nchini mwetu."

Aliongeza: "Katika nchi yetu Sensa zimefanyika nyingi miaka ya nyuma na hazikuhusishwa na dini wala ukabila, ni jambo lililo zoeleka na kukubalika na wote''

Ameonya wale wote wanaochochea waislam kukwamisha juhudi za serikali kwa minajili ya udini.


Source: Mwananchi | Jambo leo | Habari Leo
 
Katika kigeugeu kipya Bakwata kwa kupitia sheikh mkuu wametangaza kuunga mkono sensa (soma chini, chanzo Daily news online). Ila msimamo wao uko palepale kudai kipengele cha udini kiwekwe humo.

Mi binafsi sioni tija kwenye hilo na mawazo yangu ni kuwa baada ya hapo hawa watu ambao wamepofushwa na kufungwa uelewa wao na kuona kila kitu kwa kutumia tafsiri na darubini ya dini zao hawaitakii mema nchi yetu.

Ni wazi kuwa pinde dhamira yao itapotimia basi hapo wataanza kuishinikiza serikali na taasisi zake kuwa lazima uteuzi wa nafasi nyeti na ajira ziendane na uwiano wa kidini badala ya kuangalia ufanisi na uwezo wa watu kufanya kazi hizo, na baadae kudai pia wapewe ruzuku kufundisha au kujenga nyumba zao za ibada. Si unajua tena binadamu haridhiki ukimpa kidole kesho atakuja dai mkono na zaidi na zaidi!

Ni kwa dhana hiyo napendekeza kama serikali ikiwakubalia kwa huo upuuzi, basi sisi wapenda maendeleo tujaze kwenye hiyo sensa kuwa dini yetu ni uenyeji hata kama ni waislam au wakristo maana hakuna tija yeyote kwenye hilo au tuache hilo swali wazi, huu ni upuuzi tu tusiendekeze...

Kuna watu wanadai eti oo mbona UK au US wanacho hicho kipengele kwenye sensa zao, hizo nchi asilimia kubwa ni wakristo na hizi dini nyingine ni minority na nyingi waumini wake ni wageni na nia halisi ni kuona jinsi gani ya kuwahudumia wageni huko. Sasa hapa kwetu sidhani kama waislamu au wakristo ni minority au hata wageni ni wazi kuwa wengi wao ni wenyeji na priority ya serikali yetu ni kuleta maendeleo kwa wote sio group fulani la watu.

Uenyeji / Uasili Juu!, tuweke hilo mbele...Down with udini na utengano kwenye taifa letu!

[h=2]Bakwata: We are not against census[/h][h=3]The National Muslim Council of Tanzania, Bakwata, has declared that it is not against the national population census and urged the faithful to actively participate.[/h]
Mufti Sheikh Issa Shaaban bin Simba told journalists in Dar es Salaam on Monday that Bakwata understood the importance of conducting a population census.“We have nothing against the core reasons of the census. What we are against is the recent habit of people who don’t have the mandate of conducting and doing it on tribal and religious basis,” he said.
Sheikh Simba said that he wanted every Muslim to take part in the exercise. He, however, demanded to know from the government where it obtained statistics on the number of Muslims and Christians that had been posted in the national website.
“Census has been conducted on numerous occasions; that is known.
What is also known is that the government doesn’t conduct it along tribal and religious lines; we need to know where the statistics came from this time,” he said.The Mufti called upon the government to formulate a law that will take to task anyone who isn’t authorized to conduct a census and also to task those doing it along tribal and religious lines when the government has already abolished it.
He said that the council felt there was need to state their position, especially since in recent days there are many people who have come out airing the advantages and disadvantages of the census.
By MASEMBE TAMBWE, Tanzania Daily News


PS: kwenye nyekundu nimeangalia national website sijaona hiyo data mufti anayozungumzia, kama kuna mtu anajua tafadhali tuelekezane.
 
Ritz, tume ya katiba, kombo, njiwa leta mironjo hapa mje mseme mufti anatumiwa...

Bado najiuliza ni kwanini wanaotetea uamsho na uislam kwamba wanaonewa ni pro ccm tu? Tafakari...
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom