Waislam wanapaswa kuunga mkono hoja ya Katiba mpya kwa nguvu zao zote ili hoja zao za kuanzishwa kwa Mahakama ya Kadhi ziweze kujadiliwa kwa uwazi na ikiwezekana zitambuliwe rasmi. Kitendo kinachofanywa hivi sasa kutaka kuzianzisha mahakama hizo kinyemela hazitawasaidia sana.
Kwa Watanzania wote, tunahitaji Katiba mpya ambayo itaweka kila kitu bayana, katiba itakayo linda haki zetu wananchi, kupunguza Madaraka ya Rais (wajao) na kuweka mstakabali wa taifa letu hasa masuala ya Muungano.
Nawashauri Waislam wajitokeze zaidi wabebe bango ili katiba hii tuliyoachiwa na Wakoloni wa Kiingereza na kubandikwa viraka kibao, iondolewe na kuweka Katiba yetu itakayoweka usawa wa kuabudu ( why sunday a holiday and not friday), usawa wa kushiriki kwenye siasa na kuiweka nchi yetu kwenye mstari tutakaopenda wote kwa pamoja.
Kwa Watanzania wote, tunahitaji Katiba mpya ambayo itaweka kila kitu bayana, katiba itakayo linda haki zetu wananchi, kupunguza Madaraka ya Rais (wajao) na kuweka mstakabali wa taifa letu hasa masuala ya Muungano.
Nawashauri Waislam wajitokeze zaidi wabebe bango ili katiba hii tuliyoachiwa na Wakoloni wa Kiingereza na kubandikwa viraka kibao, iondolewe na kuweka Katiba yetu itakayoweka usawa wa kuabudu ( why sunday a holiday and not friday), usawa wa kushiriki kwenye siasa na kuiweka nchi yetu kwenye mstari tutakaopenda wote kwa pamoja.