Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Nasema maandamano yangefanyika yangekuwa yanaidhalilisha sana dini ya kiislam,viongozi wake,waumini wake,kitabu chake[Quran] na Mtume wake Muhamad SAW kwasababu zifuatazo.
[1] Waislamu wanataka kuandamana kwasababu serekali ya CCM imeshindwa kuanzisha mahakama ya Kadhi.Ukweli ni kwamba Serekali ya CCM imewaruhusu waislam waanzishe na kuiendesha mahakama ya kadhi wenyewe kwasababu ni sehemu ya ibada yao [waislamu].Ni ajabu kubwa kuona wanazuoni tena waliobobea kuendelea kudai mahakama ya kadhi ilihali serekali imesharidhia kuanzishwa kwake.
[2] Waislamu wa Tanzania wanajua wazi CCM imekuwa ikiwadanganya wananchi kwa muda mrefu katika mambo mabali mbali,inashangaza sana kusikia viongozi wa waislam hawakuona haja ya kuandamana wakati mabilioni ya EPA,Meremeta,ununuzi wa radar,ndege ya rais,mikataba ya madini na ufujaji wa fedha kwenye maidara ya serekali ukifanyika.Akili yangu inakataa kuamini kwamba viongozi wa waislamu leo hii wanagundua CCM ni waongo kwasababu tu wameshindwa kuvunja katiba ya JMT kwa kuingiza mahakama ya kadhi.Viongozi wa aiana hii kamwe hawataweza kuwakomboa waislam kwasababu wanashindwa kuwaeleza ukweli waumini wao kwamba mahakama ya kadhi inaweza kuanzishwa na waislamu wenyewe bila kutegemea fadhila za serekali.
Umeongea pointi tupu ndugu yangu! Haya mambo ya kulazimisha Serikali "ifuge ndevu, kuvaa kanzu na kuvaa kibaraghashia" hayafai kabisa kwa nchi yetu, yatatuletea vurugu huko mbeleni na patakuwa hapakaliki!