Waislam Kigoma wacharuka, hawamtaki RC

Tusipokuwa waangalifu Taifa letu litaingia pabaya sana kwa kuangaliana kwa majina yetu....Ukiitwa Mohamed utakosa haki ya kusaidiwa na kushirikiana na Richard,Tukimaliza hapo tutaangaliana kwa rangi,Yule Sabogo,Rostam au Abood hatokuwa na haki sawa na kina Mwasakafyuka,Rwegasira au Ntagazwa..Sumu hiyo ni mbaya na tuikemee,inaanza kama Utani lakini matokeo yake ni mabaya sana.

Jirani zetu Kenya walianza kulaumiana kwa ubaguzi wa kimakabila,na baadaye kila uteuzi wa Mzee Kibaki ukatafsiriwa kuwa ni njia ya kuimarisha kabila moja na kudhoofisha mengine,Katiba ikabadilishwa kumuondolea Rais uwezo wa kuteua bila kuulizwa,kwani sasa teuzi zote lazima zipitie kwenye Bunge.Juzi kwa kuondoa hali hiyo ya kupigiana kelele kwa makabila Rais kamteua Jaji Mkuu Mkenya mwenye asili ya kihindi.Hali hiyo imesababisha kero kubwa,kwani Bunge limekutana na kujadili kwamba Rais amekiuka utaratibu wa Katiba kwa kutomshirikisha Waziri Mkuu katika Uteuzi huo.Inawezekana kwamba kuna ukweli kwamba Rais alipindisha utaratibu,lakini ukiangalia nyuma ya pazia Ubaguzi wa kikabila ndio umekuwa uchochezi mkubwa katika siasa za jirani zetu

Tuogope Tatizo hilo la kubaguana kwa kuangalia Udini,Rangi au makabila...Katika Katiba yetu mpya kuwepo na pendekezo la kutoshirikisha namna yoyote ya Ubaguzi wa namna hiyo na Utendaji wa Serikali,kwani Serikali haina dini.Katika Kipindi hichi cha Uongozi wa Awamu ya Nne kumekuwa na malalamiko mengi ya Teuzi kuegemea Upande wa dini moja zaidi,tuondoe mawazo hayo ili tujenge Taifa lisiloendeshwa kwa mashinikizo ya kidini.

Waislamu wa Kigoma wamekuwa wakali,kwa sababu tu watendaji wao wakuu kiserikali Mkoani wote ni Wakristo.Tuwaelimishe wananchi hao,ili waangalie Utendaji kazi wa mtumishi na si dini yake.hapa chini naorodhesha baadhi ya watendaji wa Serikali Mkoani kigoma

1); Mkuu wa Mkoa - Joseph Simbakalia.

2);Mkuu wa Wilaya Kigoma - John Mongela.

3);Mkuu wa Wilaya Kibondo - Danhi Makanga.

4);Mkuu wa Wilaya Kasulu - Betty Machangu.
 
Tusipokuwa waangalifu Taifa letu litaingia pabaya sana kwa kuangaliana kwa majina yetu....Ukiitwa Mohamed utakosa haki ya kusaidiwa na kushirikiana na Richard,Tukimaliza hapo tutaangaliana kwa rangi,Yule Sabogo,Rostam au Abood hatokuwa na haki sawa na kina Mwasakafyuka,Rwegasira au Ntagazwa..Sumu hiyo ni mbaya na tuikemee,inaanza kama Utani lakini matokeo yake ni mabaya sana.

Jirani zetu Kenya walianza kulaumiana kwa ubaguzi wa kimakabila,na baadaye kila uteuzi wa Mzee Kibaki ukatafsiriwa kuwa ni njia ya kuimarisha kabila moja na kudhoofisha mengine,Katiba ikabadilishwa kumuondolea Rais uwezo wa kuteua bila kuulizwa,kwani sasa teuzi zote lazima zipitie kwenye Bunge.Juzi kwa kuondoa hali hiyo ya kupigiana kelele kwa makabila Rais kamteua Jaji Mkuu Mkenya mwenye asili ya kihindi.Hali hiyo imesababisha kero kubwa,kwani Bunge limekutana na kujadili kwamba Rais amekiuka utaratibu wa Katiba kwa kutomshirikisha Waziri Mkuu katika Uteuzi huo.Inawezekana kwamba kuna ukweli kwamba Rais alipindisha utaratibu,lakini ukiangalia nyuma ya pazia Ubaguzi wa kikabila ndio umekuwa uchochezi mkubwa katika siasa za jirani zetu

Tuogope Tatizo hilo la kubaguana kwa kuangalia Udini,Rangi au makabila...Katika Katiba yetu mpya kuwepo na pendekezo la kutoshirikisha namna yoyote ya Ubaguzi wa namna hiyo na Utendaji wa Serikali,kwani Serikali haina dini.Katika Kipindi hichi cha Uongozi wa Awamu ya Nne kumekuwa na malalamiko mengi ya Teuzi kuegemea Upande wa dini moja zaidi,tuondoe mawazo hayo ili tujenge Taifa lisiloendeshwa kwa mashinikizo ya kidini.

Waislamu wa Kigoma wamekuwa wakali,kwa sababu tu watendaji wao wakuu kiserikali Mkoani wote ni Wakristo.Tuwaelimishe wananchi hao,ili waangalie Utendaji kazi wa mtumishi na si dini yake.hapa chini naorodhesha baadhi ya watendaji wa Serikali Mkoani kigoma

1); Mkuu wa Mkoa - Joseph Simbakalia.

2);Mkuu wa Wilaya Kigoma - John Mongela.

3);Mkuu wa Wilaya Kibondo - Danhi Makanga.

4);Mkuu wa Wilaya Kasulu - Betty Machangu.

Hapa ndio nashindwa kuelewa, kama wote wangekuwa ni Waislamu napo pangekuwa na tatizo hata kama uongozi unaotolewa ni mbovu vile vile?
 
Vitu kama hivi vinatokea...........viongozi wako kimya.........vyombo vya habari vinafanya/chochea huu upuuzi (wenye madhara huko mbeleni) ya ubaguzi vinaachwa vikiendelea...........

Well, lets wait and see.............
 
dont quote huyu mdini namba 1, huwezi kunyamanzisha watu leo kijana , kikwete ni system , mfumo kristo upo kwenye system ya nchi,kuanzia kuwa na ubalozi wa vatikan hadi kuwa na MOU kati ya serikali na makanisa , kuanzia kuwadhulumu vijana wa kiislamu waliofaulu miaka ile hadi kuJA KUAJIRI KWA KIGEZO CHA UDINI, HAYA TULIYASEMA HATA kabla ya kikwete na tutaendelea kusema hadi tuutokomeze mfumo kristo katika nchi tuliyoitafutia uhuru wenyewe wakati ninyi mkiwa vibaraka wa wazungu! tunashukuru na hawa wa BAKWATA wanaanza kuelewa baada ya ninyi kujionesha katika sura yenu halisi huko Arusha, sisi tulishawaona kabla na tulishasema kabla hamjaropoka Arusha
We ukifa leo hii kwa hayo matamshi yako na mitazamo utakuwa jehanamu ya moto kwani matamshi yako si mazuri kabisa. Udini ulionao si wa kumcha Mungu bali ni wa uharibifu kabisa.Hivyo muombe Mungu akusamehe na amuondoe huyo roho mchafu sana uliyenae ili ukifa ufike peponi.
 
Tusipokuwa waangalifu Taifa letu litaingia pabaya sana kwa kuangaliana kwa majina yetu....Ukiitwa Mohamed utakosa haki ya kusaidiwa na kushirikiana na Richard,Tukimaliza hapo tutaangaliana kwa rangi,Yule Sabogo,Rostam au Abood hatokuwa na haki sawa na kina Mwasakafyuka,Rwegasira au Ntagazwa..Sumu hiyo ni mbaya na tuikemee,inaanza kama Utani lakini matokeo yake ni mabaya sana.

Jirani zetu Kenya walianza kulaumiana kwa ubaguzi wa kimakabila,na baadaye kila uteuzi wa Mzee Kibaki ukatafsiriwa kuwa ni njia ya kuimarisha kabila moja na kudhoofisha mengine,Katiba ikabadilishwa kumuondolea Rais uwezo wa kuteua bila kuulizwa,kwani sasa teuzi zote lazima zipitie kwenye Bunge.Juzi kwa kuondoa hali hiyo ya kupigiana kelele kwa makabila Rais kamteua Jaji Mkuu Mkenya mwenye asili ya kihindi.Hali hiyo imesababisha kero kubwa,kwani Bunge limekutana na kujadili kwamba Rais amekiuka utaratibu wa Katiba kwa kutomshirikisha Waziri Mkuu katika Uteuzi huo.Inawezekana kwamba kuna ukweli kwamba Rais alipindisha utaratibu,lakini ukiangalia nyuma ya pazia Ubaguzi wa kikabila ndio umekuwa uchochezi mkubwa katika siasa za jirani zetu

Tuogope Tatizo hilo la kubaguana kwa kuangalia Udini,Rangi au makabila...Katika Katiba yetu mpya kuwepo na pendekezo la kutoshirikisha namna yoyote ya Ubaguzi wa namna hiyo na Utendaji wa Serikali,kwani Serikali haina dini.Katika Kipindi hichi cha Uongozi wa Awamu ya Nne kumekuwa na malalamiko mengi ya Teuzi kuegemea Upande wa dini moja zaidi,tuondoe mawazo hayo ili tujenge Taifa lisiloendeshwa kwa mashinikizo ya kidini.

Waislamu wa Kigoma wamekuwa wakali,kwa sababu tu watendaji wao wakuu kiserikali Mkoani wote ni Wakristo.Tuwaelimishe wananchi hao,ili waangalie Utendaji kazi wa mtumishi na si dini yake.hapa chini naorodhesha baadhi ya watendaji wa Serikali Mkoani kigoma

1); Mkuu wa Mkoa - Joseph Simbakalia.

2);Mkuu wa Wilaya Kigoma - John Mongela.

3);Mkuu wa Wilaya Kibondo - Danhi Makanga.

4);Mkuu wa Wilaya Kasulu - Betty Machangu.

Mkuu upo sahihi ila tunacho waomba Waislam Kigoma walete ushahidi wa kutowajibika kwa viongozi hao ili tujue kua maamuzi yao ni sahihi au si sahihi.
 
Watanzania walishagawika siku nyingi tu.....haya ni matokeo tu........hebu naombeni kwa mtu mwenye fikra za kina kabisa itawekana vp waislam tu katika nchi hii ndio waonekana hawajasoma? Unless labda mniamie mtu kuwa mwislam anakuwa na DNA ya kufeli kielimu na nyanja nyingine.....kwa mtu mwenye kufikiria kwa mizania atakubaliana nami kuwa hii haiwezi kuwa ajali lazima kuna namna!........................
watu tulishagawika kwa kuwekewa mazingira ya kuwa tulivyo sasa! waliotakiwa kwenda shule enzi zile serikali ya mkoloni ilitaka shule ziendeshwe na missionaries na serikali ilitoa fungu kubwa kwa ajili ya hilo.......bahati mbaya na Nyerere alirithi hicho hicho

Katika jamii fulani kuwa na watu wengi wanaopendelea kitu fulani kuliko jamii nyingine si lazima kuwe na ubaguzi wa kulipangia hilo. Mazingira anayoishi mtu huwa yana athari kubwa sana, na kuondokana na hilo ni lazima kuwe na jitihada za wahusika wenyewe kuondokana na mazingira ya kale. Hii ndiyo sababu ya kuona wachezaji wengi wazuri wa mpira wa miguu hutoka katika mataifa fulani tu, haina maana Mungu kawanyima mataifa mengine kipaji hicho, bali mazingira yao hayaviendelezi vipaji hivyo. Ni sababu hizo hizo utaona nchi kama DRC kuna wanamuziki wengi, au familia za wafugaji huendelea kuwa wafugaji, familia za wafanyabiashara wanaendelea kuwa wafanyabiashara, n.k.

Mtoto anapomwona Baba yake na Mama wakirudi wanasoma magazeti au vitabu, ni lazima na yeye atajitahidi kujua kusoma na kuandika ili na yeye aweze kuona na kuelewa hicho ambacho wazazi wake huwa wanakipata katika magazeti au vitabu. Mtoto ambaye akiamka asubuhi anaona Baba yake anakuwa wa mwisho kuamka asubuhi, kuna uwezekanao mkubwa atakapokuwa mkubwa naye atafanya hivyo hivyo, akifikiria ukiwa Baba, wewe ni wa mwisho kuamka.

Suala la kuwa na proportion kubwa ya waislam, hasa vijijini, bila elimu ni la mazingira waliyoyakuta na kukulia kuliko kufikiria kuwa ni ubaguzi. Mgawanyiko huu wala siyo wa kidini tu lakini hata kimakabila na kimaeneo. Leo hii ukifanya utafiti ni dhahiri utagundua kuwa makabila fulani na mikoa fulani watu wake wamesoma zaidi ukilinganisha na baadhi ya makabila na mikoa mingine. Hawakufanyiwa ubaguzi, bali mazingira waliyokulia ndiyo yanayowafanya kufikiria ni jambo gani muhimu maishani mwao, na ndiyo wanayoyapa umuhimu.

Hakuna shule ya kikristo iliyopewa hela na serikali ya kikoloni. Kwanza wamisionari wa mwanzo kila walipofika walianzisha shule ili kuwapata watu wenye elimu waliyoitaka waweze kusaidia huduma ya kanisa, na kuelewa kile walichokuwa wakiwafundisha. Kwa upande wa Waarabu, kwa bahati mbaya sana, licha ya uwezo waliokuwa nao, walipokuja Afrika hawakushughulika na masuala ya elimu wala afya, hiyo iliathiri sana mtazamo wa jamii ya kiislam katika masuala ya Elimu si kitu ambacho kilionekana ni muhimu kutoka kwa wale waliokuwa wakiwafundisha dini.

Kinachonishangaza sana ni juu ya waislam kutozitambua jitahada za Mwl J.K. Nyerere katika kubadilisha hali iliyokuwepo. Mwalimu alitaafisha shule zote za kanisa ili watu wote wasome, sasa kutokutambua jitihada hizo, hilo linanishangaza sana. Walitaka afanye nini zaidi ya hivyo? Najua waislam waliokuwa na dhamira na walioiona elimu Dunia ni muhimu kwa ustawi wa binadamu, waliitumia nafasi hiyo, na ndiyo maana kuna waislam wengi tu ni Doctors (PhD), profs, na n.k. na gap hiyo ya tofauti ya elimu kati ya wakristo na waislam, kama ilivyo kati ya wahaya na wahehe, wachaga na wasukuma, watu wa mikoa ya Kagera na Ruvuma, Mbeya na Rukwa, inazidi kupungua kila kukicha maana wananchi walio wengi wanajua umuhimu wa elimu dunia kwa sasa kuliko siku za huko nyuma.
 
Mungu wangu sijawi kuyaelewa madai ya hawa jamaa. kila wakitoa tamko huwa naona yota tupu. jamani
 
Kwa hili la viongozi wa kigoma ndo mwamuunga mkono jk sivo?si mmekuwa mkiponda kila kitu kuhusu yeye.
Kama nguvu ya wanakigoma haiwataki so be it WAONDOSHWE TU.
 
Kwa hili la viongozi wa kigoma ndo mwamuunga mkono jk sivo?si mmekuwa mkiponda kila kitu kuhusu yeye.
Kama nguvu ya wanakigoma haiwataki so be it WAONDOSHWE TU.
 
Hivi kuna anayezijua dhulma zote zinazodaiwa na waislamu nchini Tanzania? Itapendeza kama zikianikwa hapa tujaribu kuzijadili na kuangalia uhalisia/ukweli wake.

ANGALIZO: Si vema kutumia lugha za matusi ama kejeli, binafsi SIJAWAHI KUONA HAPA JF WAKIWABEZA CHRISTIANS kwa mithili ya (hawakusoma hao, mbumbumbu, watu wa ubwabwa, tende zimewashibisha etc). Lakini iwaje waislamu ndio waandamwe kwa SEMI hizo? kwa nini tusitumie busara tu za 'kutokubwabwaja' bali kuheshimiana kiimani zetu? I hope it won't cost a thing kwa kutowakejeli wenzako.
 
kama kuwa Mkuu wa nchi (Rais wa nchi) inakuwezesha kupendelea watu wa dini yako basi hapa Tanzania tungepata tabu sana kwani hadi sasa tangia uhuru marais wakristo wamekuwa wawili na waislamu wawili. zama za ukristo Rais mkristo angependelea wakristo na zama za waislamu wangependelea waislamu.

Mimi sishangai sana kwa sababu marais wakristo wanalaumiwa kupendelea dini yao na Marais waislamu wanalaumiwa kupendelea watu wa dini zao. Jambo hili ni la kukosa akili tu za kufikiri kwa kina.
 
Mwaka 2010 wanafunzi 10 bora wa kidato cha nne wote ni wakristo ni Rais yupi kapendelea? na mbaya zaidi wametoka shule za kanisa huku za serikali zikiachwa nyuma.

Mimi nasomesha watoto wangu shule nzuri kwa kipato changu kidogo wala serikali halipi ada ya wanangu kwa kuwa najua siku moja wakipata elimu watakuwa watu fulani katika jamii yetu. Siku hizi elimu nzuri inapatikana katika mashule binafsi huko kwa watu binafsi serikali haihusiki kusomesha watoto wa kikiristo wala kiislamu. je, ni wangapi hapa JF tunashindana kupeleka watoto huko. Ni makosa kudhani wote wanaopeleka watoto shule nzuri ni matajiri bali wapo wanaojinyima kusudi watoto wao waende shule bora zaidi.

Dunia ni ajabu sana unaweza kuchukua muda mrefu kutafuta makosa ya mwenzio yakachukua sehemu kubwa ya muda wa maisha yako wakati hivi sasa ni soko huria mashindano ya watu si lazima yaanzie serikalini bali hata majumbani mwetu kwa juhudi zetu wenyewe.
 
Nchi hii ya ajabu sana, watu kama akina Sabodo ni mwislamu lakini amejenga hadi makanisa, Mengi ni mkristo kajenga hadi miskiti, Mkapa alitoa chuo cha shirika la TANESCO morogoro kuwa chuo cha kiislamu wakati majengo hayo yalikuwa ya watanzania wote na Nyerere amejenga miskiti ukiwemo wa kijijini kwako Butiama lakini bado watu wanajenga hoja za udini... ni upumbavu wala sio ujinga wa hali ya juu kabisa.

Hapa tungeweza kuwa tunaongelea mambo ya maana kwa mfano, chuo cha kiislamu cha Morogoro kimetoa matunda tuliyotarajia au bado na kama bado nini kifanyike ili kiwe chuo chenye nguvu ya kuinua waislamu. Je, kwa nini seminari za Kiislamu hazifanyi vizuri kuliko shule za kanisa, nini kifanyike? Je, Rais aliopo naye anapendelea wakristo?

Suala la tofauti ya wakristo na waislamu katika ajira haliwezi kuja kwa miujiza ni tatizo la kweli lakini chanzo chake ni tofauti zetu katika elimu na ili liishe zijengwe hoja ambazo hazitaendelea kutugawanya wakristo na waislamu. Mwisho wa siku tutafikia shule za wakristo hawasomi waislamu na shule za waislamu hawasomi wakristo. Hali hii itaongeza tatizo zaidi badala ya ufumbuzi.
 
Nchi hii ya ajabu sana, watu kama akina Sabodo ni mwislamu lakini amejenga hadi makanisa, Mengi ni mkristo kajenga hadi miskiti, Mkapa alitoa chuo cha shirika la TANESCO morogoro kuwa chuo cha kiislamu wakati majengo hayo yalikuwa ya watanzania wote na Nyerere amejenga miskiti ukiwemo wa kijijini kwako Butiama lakini bado watu wanajenga hoja za udini... ni upumbavu wala sio ujinga wa hali ya juu kabisa.

Hapa tungeweza kuwa tunaongelea mambo ya maana kwa mfano, chuo cha kiislamu cha Morogoro kimetoa matunda tuliyotarajia au bado na kama bado nini kifanyike ili kiwe chuo chenye nguvu ya kuinua waislamu. Je, kwa nini seminari za Kiislamu hazifanyi vizuri kuliko shule za kanisa, nini kifanyike? Je, Rais aliopo anapendelea wakristo?

Suala la tofauti ya wakristo na waislamu katika ajira haliwezi kuja kwa miujiza ni tatizo la kweli lakini ili liishe zijengwe hoja ambazo hazitaendelea kutugawanya. Mwisho wa siku tutafikia shule za wakristo hawasomi waislamu na shule za waislamu hawasomi wakristo. Hali hii itaongeza tatizo zaidi badala ya ufumbuzi.

Wako kwa kazi maalumu hao wadini! Nia kubwa ni kututoa kwenye hoja za msingi zenye maslahi ya taifa kwa kutoa Matamko yasiyo na tija! badala ya kujadili matatizo tuliyo nayo ya umeme, ufisadi na kushuka kwa viwango vya elimu tutakuwa busy na kujadili matamko yasiyo na kichwa wala miguu ili mradi tupoteze track. Hivi nchi inaongozwa na matamko?
 
hata aliyeleta mada hii hapa ukimuuliza alisoma shule ipi na akatupatia jina la mwalimu mkristo ambaye aliwapendelea wakristo wenzake hatakuwa na jibu kwa kuwa tu ameamua kuwa mtumwa wa historia yake mwenyewe anataka kutugawanya watanzania kwa makundi ya waislamu na wakristo.

Jamani hebu tuulizane hivi likianzishwa baraza la usuluhishi la taifa litakalohitaji waislamu walionyanyaswa kielimu na Nyerere wajitokeze na kama wapo mbona hawatajwi kwa majina na shule walizosoma na walimu waliowafundisha? kuna wakati nashangaa sana hivi waislamu kama Rais Kikwete, Prof. Lipumba, Kigoma malima na wengine wengi waliosoma shule za kanisa waliwezaje kufanikiwa na uislamu wao tena kipindi cha nyerere? Na ajabu na kweli waislamu wengi waliosoma shule za kanisa enzi za mwalimu ndio wamefanikiwa zaidi kiuongozi kuliko wale waliosoma shule za serikali enzi za Nyerere. Je, na hili limekaaje? Je, walitengwa na kanisa? kama ndio waliwezaje kumaliza shule?
 
Nyerere aliunganisha taifa la kiislamu la Zanzibar na Tanganyika. Hii imekaaje kama ni kweli alikuwa anachukia maendeleo ya waislamu?
 
Nyerere ana bahati mbaya sana, wakristo wanamlaumu kwamba alitaifisha shule zao za misheni ( za kanisa) ili kuwasaidia waislamu baada ya kugundua wako nyuma mara baada ya kupata uhuru na waislamu wanasema Nyerere alitunyima elimu. Halafu baadaye Nyerere akaanza kuwapendelea wakristo mashuleni. Hii imekaaje?

Wapo wanaofikiri Nyerere alifanya kosa au kitendo kibaya kutaifisha mashule na mahospitali ya wakristo lakini wazalendo wanaona kilikuwa ni kitendo cha ujasiri sana katika kuwapa elimu sawa watanzania wote.
 
Mchana huu waislam wa Kigoma wametoa tamko kali kuhusu dhulma walizofanyiwa na wanaouita "mfumo Kristo". wamemlaani Nyerere na wote wanaoendeleza dhulma. Nimeambiwa redio Imaan ilirusha matangazo laivu wakimtaka Rais Jk awafukuze kazi Mkuu wa mkoa, ma dc wa wilaya zote za kigoma. kwa wale waliolipata kwa ukamilifu tafadhali tumwagieni data

Huku siyo kuchanganya dini na siasa kama walivyofanya maaskofu wa Arusha? Mbona sijasikia wakishauriwa kuvua kanzu na vibandiko ili waingie kwenye majukwaa rasmi ya siasa?
 
Wako kwa kazi maalumu hao wadini! Nia kubwa ni kututoa kwenye hoja za msingi zenye maslahi ya taifa kwa kutoa Matamko yasiyo na tija! badala ya kujadili matatizo tuliyo nayo ya umeme, ufisadi na kushuka kwa viwango vya elimu tutakuwa busy na kujadili matamko yasiyo na kichwa wala miguu ili mradi tupoteze track. Hivi nchi inaongozwa na matamko?

Kama wewe ulivyo na kazi maalum kutoa kashfa kwa waislamu na uislamu ili watu wabaki wanajadili ujinga wako usio na faida kwa nchi

Besides kuna shida gani kama wananchi wametoa tamko lao ambao ni uhuru wao wa kikatiba

Walianza wakristo na waraka wao ndio wamewasha moto...inabidi mkubali kusikiliza wote ok..painful truth
 
Back
Top Bottom