Waislam Dodoma watoa Tamko kumwombea mwislam mwenzao Gaddafi

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
WAUMINI wa dini ya Kiislamu mkoani Dodoma, wamewataka Watanzania kupuuza uvumi kuhusu mgogoro wa Libya, badala yake, wametaka kuungana na kumuombea kiongozi huyo adumu madarakani.

Wito huo ulitolewa juzi na Sheikh wa Mkoa wa Dodoma, Mustafa Rajabu Shabaan, ambaye alisema hakuna machafuko nchini Libya bali kinachotokea ni kikundi kidogo alichokiita cha kihuni kinachopanga kumuondoa, Kanali Muammar Gaddafi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, Sheikh Shaaban alisema tamko la Waislam wa Mkoa wa Dodoma ni kuwataka wenzao nchini na duniani, kuhakikisha hawaungi mkono kikundi hicho cha kihuni.

Sheikh Shaaban alisema kinachofanyika ni baadhi ya watu ambao wanapenda kunywa pombe na kutumia dawa za kulevya, walioko mpakani mwa nchi hiyo na Misri ndio walioanzisha fukuto hilo.

“Mimi ni nina shahada ya sheria ambayo niliipata Libya, nina ufahamu mzuri wa uongozi wa Gadaffi, ni mtu wa upendo kwa watu wake na nimekuwa nawasiliana na wenzangu huko wanasema machafuko ni ya mji mmoja tu, sio nchi nzima,” alisema Sheikh Shaaban.

Kiongozi huyo alisema licha ya kuongoza nchi yake vizuri kwa kwa muda mrefu, Kanali Gaddafi amekuwa na mchango mkubwa kwa mataifa mbalimbali.

Kanali Gaddafi amejenga msikiti mkubwa mjini Dodoma na nchini Uganda. Pia, alifadhili ujenzi wa msikiti wa Butiama, baada ya Baba wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Nyerere kumuomba.

Source: Mwananchi
 
Pilipili usizozila zakuwashiani?
Hilo tamko sasa litawasilishwa kwa nani?...Kama vipi watume ujumbe wa waganga na warozi kumzindika kama walivyofanya wakenya!
Jamani kuna mambo pressing mengi mno nchini ambayo yanahitaji tuyalaani na kuyasemea kwa wenye hatamu za nchi..tunapata wapi hii ya kusemea mambo ya Libya?
 
sipendi kuamini, sitaki kuamini na hata nikilazimishwa sikuabli kuamini kuwa Libya hakuna mgogoro mkubwa na kuwa Dikteta Gadhafi anapendwa sana na watu wake.
 
I hope this is a joke! CDM na Wakristo wameweza kuwashahuri Walibya kuandamana kumwondoa Gadhafi? Kweli kuna tatizo hapo huo msikiti Dodoma. Here we go again...
 
Sheikh: degree ya sheria,Gadafi mtu safi, macahafuko yako mji mmoja, wahuni na watumia madawa ya kulevya ndo wanaleta vurugu, i dought uwezo wa Sheik kuelewa mambo, haangalii hata TV,
 
Mkuu MM Libya ni movement ya kukinai utawala...sikupata kufika Libya physical lakini kihistoria nimeitembelea hii nchi...kiuchumi imepaa,miundombinu,hali ya maisha ya watu as well...Gadafi ni dikteta, sawa! Huyu mfalme wa amani JK na amani yake ametufikisha wapi?
 
Huyu shehe anafikiri kuwa na degree ndio kuwa na uelewa mkubwa ubwabwa kweli.
 
Sheikh Shaaban alisema kinachofanyika ni baadhi ya watu ambao wanapenda kunywa pombe na kutumia dawa za kulevya, walioko mpakani mwa nchi hiyo na Misri ndio walioanzisha fukuto hilo.
i

Inasikitisha kiongozi wa dini kusema uongo mkubwa kama huu. Haiwezekani watu 600,000+ wanaoishi Benghazi (almost wote Waislam) wote wawe walevi na drug addicts.
 
Siwezi kuamini haya hawa watu tuwaite vipi wajinga wapumbavu mabwege mazuzuzu mambumbumbu au wanafiki. Ama kweli upanga kwa upanga ndio imani. Hao wanaokufa sio watu bali mtu ni huyu mwendawazimu Gaddaffi. Futeni kauli yenu maana hata ulimwengu utawashangaa. No wonder Membe hajasema kitu. Hivi Tz. kuna viongozi au kuna walevi hii siamini masikiio macho na fikra zangu. Mlaaniwe yes i said mlaaniwe mliotoa tamko.
 
Wana Jf, kila mara huwa nakumbusha kuwa hoja hujibiwa kwa hoja. Inapojibiwa kwa hisia(emotion) basi hupoteza muelekeo.
Voingozi wa dini ni wanadamu kama walivyo wanadamu wengine, tena wapo viongozi waliooza kiimadili kuliko waamuni wao. Inategemea kiongozi huyo yupo wapi na anawaumini wenye uelewa kiasi gani.
Hoja hapa ni kumwambia sheikh kuwa kama hao ni wahuni je Tunisia, Algeria, Morocco, Egypt, Bahrain, Jordan na hata Saudia ambako king amefanya mabadiliko kuepeuka Jasmine revolution, je nako wanakula vidonge.? Ukisoma hoja za sheikh, haraka utatambua kuwa uwezo wake wa kufikiri na kupata habari ni finyu sana. Kama ilivyo CCM kule vijijini inapowaambia watu tumeleta maendeleo na watu wakapiga makofi ndivyo ilivyo katika jamii zetu zenye uelewa finyu! hatuwezi kukataa ukweli huu.

Ninachosisitiza hapa ni kuwa suala hilo lisifanywe au lisiunganishwe na imani za dini. Hao mamilion ya watu mideast wangemsikia sheikh wa dodoma pengine wangezimia wote. Lakini hata hapa JF na Tanzania kwa ujumla na pengine ndani ya msikiti huo wa sheikh kuna maelfu ya waislam waliochukizwa na kushangazwa na kauli ya sheikh. Hatutawatendea haki kama kauli ya mtu mmoja itafungamanishwa na imani za mamilioni ya watu. Kauli hii ni yake na sidhani kuwa ni ya waislam. Kama alivyowahi kusema Askofu kilaini, JK ni chaguo la mungu, ile imebaki kuwa kauli yake na si kauli ya Wakristo. Tujaribu kuchambua hoja zaidi kuliko kuweka mbele hisia zetu au kutowatendea haki wasiojihusisha na kauli za baadhi ya watu.
 
Huyu shehe sijui shehe ni muongo, mimi hapa nilipo nipo na jamaa wa Libya anasema ndugu zake na wazazi wake wapo ndani hawatoki watu huko hawalali. Kama hakuna vita anawataka watanzania wawaombee kwa sababu gani au amechanganikiwa. Halafu ndugu watanzania mtu kama huyu ni wakuchapa bakora na sijui amapewaje uongozi wa dini. Jana waziri wa mambo ya ndani alisema nini alipokuwa anaongea na waandishi wa habari kuhusu watanzania wanaoishi Libya.
 
mada za uchochezi sio issue. kifacti Gadaffi ili kuokoa maisha yake akimbie Libya ila hukumu ya kuua watu ipo pale pale kwa wanadamu na maulana watu wamemchoka kwa tabia zake hadi mawaziri , wabunge , wanajeshi na mabalozi wamemtosa lakini iweje Dodoma akubariwe kama nabii Wamshauri akikimbia libya afikie Dodoma for his last Destination..Muhahahahaaha
 
Sijui kwa nini mna jisumbua kuchambua hilo tamko. The answer is in between the lines.

Kanali Gaddafi amejenga msikiti mkubwa mjini Dodoma na nchini Uganda. Pia, alifadhili ujenzi wa msikiti wa Butiama, baada ya Baba wa Taifa, marehemu Mwalimu Julius Nyerere kumuomba.

Need they say more?
 
Sijui kwa nini mna jisumbua kuchambua hilo tamko. The answer is in between the lines.



Need they say more?

I thought Nyerere despised Gaddafi (whole Kagera war fiasco..) why would he ask for a msikiti..from him or anyone for that matter.

anyways, sheh mlevi huyo useless kabisa.
 
kwa hiyo ni halalai kuuwa mende na panya wa Libya kwa sababu aliwajengea misikiti waswahili wa Dodoma. habar nkjema ni kwamba Gaddafi lazima ang'oke. ameuwa mende na panya wengi sana. Mungu siyo **** hata amuache. lazima aondoke tena kwa aibu kubwa (kwa kutembezwa mtaani uchi wa mende). ni suala la muda tu. kama vipi hao w,ashehe wa Dom watafute msaada wa msikiti kwa mtu mwingine.
 
I thought Nyerere despised Gaddafi (whole Kagera war fiasco..) why would he ask for a msikiti..from him or anyone for that matter.

anyways, sheh mlevi huyo useless kabisa.

Sometimes as a leader you must put your ego aside for your people. Maybe aliona msikiti huo uta wanufaisha wananchi wake wa Kiislamu. In politics there is no permanent friend or enemy.
 
sio ajabu ndugu, pale dodoma kunamsikiti mkubwa sana unaitwa MSIKITI WA GADAFI, NDIO MSIKITI WA MKOA, so washatekwa na material things, they don't reason. Hv Dodoma na Libya waislam wa ukweli wapo wap? Tena libya ndio wapo jiran na kabuli la mtume kabisa, na sharia kule ndio sheria mama!
 
Back
Top Bottom