Waionaje Kili Stars ya kina Julio/Master?

kocha wa jkt oljoro au mtibwa wangefaa maana timu zao zinafanya vema
 
anasumbuliwa na usimba/uyanga. safari hii naona kaita wavuta ganja wenzake. mia

mkuu huo u simba na u yanga unaoongelea hapo ni upi umefuatilia selection yake kwa makini kwa maoni yangu nadhan utakuwa umekosea kidogo, kama cjakosea yanga wanawachezaji wawili tu(nurdin na kado) na anayecheza ni nurdin kwan kado hana tofauti na mtazamaji. Inshort labda uzungumzie kitu kingine na uyanga au usimba
 
mkuu huo u simba na u yanga unaoongelea hapo ni upi umefuatilia selection yake kwa makini kwa maoni yangu nadhan utakuwa umekosea kidogo, kama cjakosea yanga wanawachezaji wawili tu(nurdin na kado) na anayecheza ni nurdin kwan kado hana tofauti na mtazamaji. Inshort labda uzungumzie kitu kingine na uyanga au usimba
Simba wa sasa na wale legion timu ina kama 12 hivi.
 
hahahahahaa, hiyo ni timu ya kocha mmojawapo kati ya walioteuliwa kuiongoza kili statz (Julio), nimeshangaa zaidi kitendo cha kumuita Said Maulid kwenye kambi, huyu mtu si ameshaanza kuzeeka kisoka, sasa wanamwita ili iweje......kwa nini basi wasingeita walau wachezaji kadhaa wa timu ya vijana ili kuwapa uzoefu?........ hao ndio makocha wetu wazawa...ngoja tuone kitakachotokea.

kusema ukweli mimi ni moja kati ya wanaopinga kuendekezwa kwa makocha wa kigeni, na kama ingetokea kocha mzawa akapewa timu, ningempendekeza Jamhuri kwa kigezo cha uzoefu na uwezo wa kuwajengea ari wachezaji. Ila kwa mwendo anaoenda nao kwenye Challenge plus tuhma za kuleta unazi kwenye kuunda timu, nimepungukiwa na imani kabisa!
 
kusema ukweli mimi ni moja kati ya wanaopinga kuendekezwa kwa makocha wa kigeni, na kama ingetokea kocha mzawa akapewa timu, ningempendekeza Jamhuri kwa kigezo cha uzoefu na uwezo wa kuwajengea ari wachezaji. Ila kwa mwendo anaoenda nao kwenye Challenge plus tuhma za kuleta unazi kwenye kuunda timu, nimepungukiwa na imani kabisa!
Unazi na pia ameshaover take Mkwasa,maana yeye ndio msemaji mpanga timu na mpiga porojo mkuu.
 
Wamenifurahisha kwa kumleta Boban na kuachana na kasumba za makocha wazungu...na amini chini ya Julio timu itakuwa na hamasa maana hii kazi ya kuamasisha anaiweza sana....

huu ushabiki wa kijinga ndio unatupeleka kuteua timu mbovu mbovu! BOBAN! BOBAN! Mbona hakuonyesha cha ajabu siku na Rwanda????????? TENA alikuwa CHOKI Mbaya!
 
Shida ya mpira wa bongo sio ya kutatuliwa leo au kesho. Mfano,amekuja Guardiola,au Ferguson,ama wakachanganyika wote na kumuongeza Mourinho,kwamba sasa tutafika hadi fainali kombe la CAF...Achilia mbali kushiriki kombe la Dunia! Haiwezekani,na ni ndoto za asubuhi.... Kuna wakati nadhani,kuliko kutapatapa kama kipofu gizani,mara kocha wa kigeni,mara mzawa ndiyo suluhisho,mara kikosi kinabadilishwa mara kwa mara,mara wachezaji hawajitumi,mara hawana vipaji,mara wana viwango vidogo,mara TFF ndiyo tatizo,n.k... Kwa kuwa tunakubaliana hatujui ugonjwa gani unaolisumbua soka letu... Maoni yangu,ni kuundwa TUME! Tumeshuhudia tume mbalimbali zikifanya kazi nzuri,kwa kufichua udhaifu,uzembe, mianya,na kutoa ushauri/ mapendekezo juu ya suala husika. Nami naishauri Serikali,iteue tume kwa ajili ya kuturudisha kwenye ramani ya soka la kimataifa..
 
Julio mjinga sana kajaza simba hata uwezo hawana,eti Juma Jabu wa kumzidi Oscar Joshua? Kapombe wa kumnyima namba Taita? Cpingi uwezo wa Kazimoto,Kaseja na Nyoso..
 
Julio mjinga sana kajaza simba hata uwezo hawana,eti Juma Jabu wa kumzidi Oscar Joshua? Kapombe wa kumnyima namba Taita? Cpingi uwezo wa Kazimoto,Kaseja na Nyoso..
Hata Kazimoto hana match fitness,alikuwa majeruhi kwa muda mrefu.
 
Mkwasa na Julio nao... Mkongwe Saidi Maulidi wangemuacha, muda wake umekwisha. Afadhali badala yake wangemchukua John Boko kwa manufaa ya sasa na ya baadaye. Nadhani kuna kujuana hapo...
Thomas Ulimwengu naye aache uchoyo na tamaa.
 
Mkwasa na Julio nao... Mkongwe Saidi Maulidi wangemuacha, muda wake umekwisha. Afadhali badala yake wangemchukua John Boko kwa manufaa ya sasa na ya baadaye. Nadhani kuna kujuana hapo...
Thomas Ulimwengu naye aache uchoyo na tamaa.
Jionee haya kwenye Kili Stars:
1.Juma Kaseja-Simba
2.Shomari Kapombe-Simba
3.Juma Nyoso-Simba
4.Juma Jabu-Simba
5.Mwinyi Kazimoto-Simba
6.Haruna Moshi-Simba
7.Ramadhani Chombo-Azam/Simba
8.Saidi Mauluid-Simba/Yanga
9.Nurdin Bakari-Simba/Yanga
10.Mbwana Samatta-TP Mazembe/Simba
11.Mussa Mgosi-DC Motema Pembe/Simba
12Said Morad-Azam/Simba
13.Shaaban Nditi-Mtibwa/Simba
14.Wachezaji wa Coastal-Julio/Simba
Kwa nini watu wasizomee timu ya upendeleo ya Julio?
 
Inakuwaje Coastal Union inatoa wachezaji 3 wakati wako mkiani mwa ligi ilhali timu kama Oljoro JKT haina hana mmoja?

Kocha anamteua mchezaji kwa kutumia vigezo mbali mbali kimojawapo kikiwa ni kumfahamu mchezaji uwezo wake uwanjani. Na hili linawezekana sana akimuona mwenyewe mchezaji akifanya mazoezi na kucheza katika mechi za kimashindano. Coastal kuwa mkiani haimaanishi kuwa wachezaji woote hawana uwezo wa kuchezea timu ya Taifa ya Tanzania Bara/Tanganyika(Kilimanjaro Stars). Kwani wachezaji watatu tu ndio wanoichezea Coastal union! Pempua zaidi mkuu. Pili shaurini makocha kuhusu wachezaji wanaofaa kuchezea timu mzipendazo kwa kufuata utaratibu(huku mkitoa vigezo vinavyoeleweka kulingana na wakati uliopo).
 
Kocha anamteua mchezaji kwa kutumia vigezo mbali mbali kimojawapo kikiwa ni kumfahamu mchezaji uwezo wake uwanjani. Na hili linawezekana sana akimuona mwenyewe mchezaji akifanya mazoezi na kucheza katika mechi za kimashindano. Coastal kuwa mkiani haimaanishi kuwa wachezaji woote hawana uwezo wa kuchezea timu ya Taifa ya Tanzania Bara/Tanganyika(Kilimanjaro Stars). Kwani wachezaji watatu tu ndio wanoichezea Coastal union! Pempua zaidi mkuu. Pili shaurini makocha kuhusu wachezaji wanaofaa kuchezea timu mzipendazo kwa kufuata utaratibu(huku mkitoa vigezo vinavyoeleweka kulingana na wakati uliopo).
Kwa mchezaji ambae timu yake iko mkiani,tegemea kwamba udhaifu wa timu hiyo umechangiwa na wachezaji,hivyo kwa viwango vyao hawafai kuchezea timu ya taifa.
 
Kwa mchezaji ambae timu yake iko mkiani,tegemea kwamba udhaifu wa timu hiyo umechangiwa na wachezaji,hivyo viwangio vyao hawafai kuchezea taifa.

Hoja yako(kwangu mimi) inakuwa na uzito, endapo ligi ambayo Coastal Union inashiriki ingekuwa inaendeshwa kwa "fair play" ndani ya uwanja na nje ya uwanja. Mara ngapi tumesikia malalamiko ya Timu zenye vipato vidogo inkiwemo Coastal (katika ligi ya Tanzania bara/Tanganyika) kulalamika kuwa zinaonewa na marefa (kwa marefa kuzibeba timu kubwa Simba na Yanga n.k baada ya kula rushwa i.e najua issue ya refa Kazi unaikumbuka). Hoja yako ni 'ideal' katika ligi za nyumbani(Vodacom league) .
 
Hoja yako(kwangu mimi) inakuwa na uzito, endapo ligi ambayo Coastal Union inashiriki ingekuwa inaendeshwa kwa "fair play" ndani ya uwanja na nje ya uwanja. Mara ngapi tumesikia malalamiko ya Timu zenye vipato vidogo inkiwemo Coastal (katika ligi ya Tanzania bara/Tanganyika) kulalamika kuwa zinaonewa na marefa (kwa marefa kuzibeba timu kubwa Simba na Yanga n.k baada ya kula rushwa i.e najua issue ya refa Kazi unaikumbuka). Hoja yako ni 'ideal' katika ligi za nyumbani(Vodacom league) .

Tatizo la waamuzi si kwa Tz/Tg pekee ni swala la Afrika na dunia kwa ujumla,lakini wenzetu angalau wanaweza kuchagua wachezaji kwa vigezo sahihi.
 
Leo tunaisubiri timu YETU ishinde.
1.Juma Kaseja-Simba
2.Shomari Kapombe-Simba
3.Juma Nyoso-Simba
4.Juma Jabu-Simba
5.Mwinyi Kazimoto-Simba
6.Haruna Moshi-Simba
7.Ramadhani Chombo-Azam/Simba
8.Saidi Mauluid-Simba/Yanga
9.Nurdin Bakari-Simba/Yanga
10.Mbwana Samatta-TP Mazembe/Simba
11.Mussa Mgosi-DC Motema Pembe/Simba
12Said Morad-Azam/Simba
13.Shaaban Nditi-Mtibwa/Simba
14.Wachezaji wa Coastal-Julio/Simba
Kwa nini watu wasizomee timu ya upendeleo ya Julio?[/QUOTE]
 
Back
Top Bottom