Kilembwe
JF-Expert Member
- Aug 19, 2009
- 2,056
- 1,598
Mkuu umesahau kuwa Kilinjiko iko Kilimanjaro na sifa ya mkoa huo kiakili inajulikana, wamezoa kusoma kwa tabu na kutumia ufahamu kwa mambo ya kujiendeleza. Kule Kilimanjaro hakuna kudekea elimu, wao wanaitafuta kwa kuwa walishajua kupitia maneno ya Mungu kuwa "Ikamateni sana Elimu.....). Nyie Quran inasemaje kuhusu elimu dunia?
Asante kwa kunikumbusha kuwa Kilinjiko iko Kilimanjaro, so nafikiri basi seminari zote za kiislam ziangalie Kilinjiko imewezaje kukwepa panga la Ndalichako kama kweli lipo! Kuhusu Quran tukufu inasema nini juu ya elim duni, ni kuwa Quran haikubagua elimu , Muhamad ( rehema za mwenyezi Mungu ziwe juu yake), alipokuwa anapewa utume kitu cha kwanza aliambiwa" IQRA" yaani "SOMA", hakuambiwa "SOMA QURAN" la hasha aliambiwa soma, na kwa tafsiri yake ni kuwa asome kila kitu kwa kilatini wanasema"DOCEBIT VOS OMNIA", na ndio maana nae aliwakumbusha waislamu kwa kuwaambia" Itafuteni Elimu hata kama ni Uchina", na ushahidi wa kuwa Waislam wa Mwanzo enzi za Muhamad walikuwa wasomi wazuri, angalia historia ya tiba hasa katika nchi za Hispania na Ulaya kwa ujumla wake, angalia pia Chuo Kikuu cha kwanza Afrika kilijengwa kule Ghana na mtawala wao aliye itwa Mansa Kankan Mussa, huyu alijenga chuo hiki baada ya kutoka kuhiji Makka na alijionea muamko wa elimu kule! ndio maana mimi nashangaa haya yanayoendelea hapa!