VUTA-NKUVUTE
JF-Expert Member
- Nov 25, 2010
- 6,135
- 17,802
Baada ya kutafakari karibu kwa robo ya maisha yangu,nimegundua kuwa maendeleo ya nchi kama Tanzania hayatakuja ikiwa tutaendelea kuhisaniwa kwa kiwango kilichopo.Viongozi wetu wanajisahau mno.Si wana uhakika kuwa kuna mtu atatoa fedha? Wahisani wangetuacha kidogo tujipime uwezo wetu.Changamoto tutakazozipata zitatufanya tuwe na adabu na hehima kwa kila mmoja.Viongozi watakuwa wabunifu na wachapakazi tafauti na sasa ambapo wao ni wafanya anasa wakubwa! Wahisani watuache kwanza.Watuache tujishikishe na tushikishane adabu.Kipato chetu tunacho,misaada ya nini sasa? Amini nawaambia,haitaendelea nchi hii hadi tutakapotalikiwa na Wahisani!