only83
JF-Expert Member
- Oct 15, 2010
- 5,343
- 2,525
...Habari ambazo ni za uhakika nilizozipata juzi ijumaa ni kuwa wahadhiri wa chuo kikuu cha Dodoma wanaendelea kulalama juu ya maisha magumu na kunyanyaswa na DVC PFA Prof.Shabaan Mlacha...Mteule huyu wa raisi ameendelea kuwatesa na kutowatendea haki wafanyakazi wa chuo kile hasa wale upande wa Taaluma.....Na kwa takribani miezi sita tayari amekwisha watimua karibu wahadhiri 6 tena wengi wao bila hata kufata utaratibu wa sheria za kazi.Na uongozi wa chuo hiki umeendelea kutoa vitisho kuwa kama mnataka yawakute ya wenzenu wa Ustawi wa jamii gomeni muone.Katika kikao chao walichofanya siku ya Alhamisi inasemekana baadhi ya wahadhiri waliongea kwa uchungu na kwa hisia kali juu ya manyanyaso hayo,na wengine kuapa kuwa ni bora sasa kufukuzwa kuliko kuendelea kuona hali hii ikiendelea....nje ya tabia ya kufukuza ambayo sasa imekuwa kama desturi ya vyuo vya umma,madai mengine ya msingi kwa hawa wahadhiri ni kukaa muda mrefu bila promotion,na hata wale waliopata promotion bado mishahara yao haijabadilika..na la pili ni lile ni juu ya tofauti ya mishahara kati ya UDOM na vyuo vingine vya umma,ambalo lilipigiwa kelele hata kwenye mgomo wa kwanza ambao Waziri Pinda alikuja kusuluhisha..baya zaidi wakati wa mgomo wa kwanza Prof Mlacha ndio alikuwa anamaliza mkataba wake wa kwanza,wakati wahadhiri na wanafunzi wapo kwenye mgomo wa kumtoa huyu mungu mtu Prof Mlacha huku nyuma ikulu ilikuwa inasaini nae mkataba wa miaka mingine minne..kwangu mimi hii ni dharau kubwa kwa hawa wahadhiri...
Maadhimio:
Taarifa nilizozipata ni kuwa wahadhiri hao watachukua hatua zifuatazo ili kurudisha heshima iliyopotea kwa muda hapa chuoni;
Source:mwanachama wa UDOMASA...
Maadhimio:
Taarifa nilizozipata ni kuwa wahadhiri hao watachukua hatua zifuatazo ili kurudisha heshima iliyopotea kwa muda hapa chuoni;
- Wamewapa menejimenti mpaka tarehe 28/01/2012 kujua hatma ya promotion na malimbilizo ya mishahara yao,ambapo inaonekana kuna kurushiana mpira kati ya Hazina,UDOM na wizara kwa upande mwingine..
- Kutoa tamko kwa vyombo vya habari ili watanzania na umma wa dunia ujue maovu na unyanyasaji unaofanyika pale UDOM kwa muda mrefu sasa...
- Kutangaza mgogoro na uongozi wa chuo wa milele mpaka hapo watakapofanya maamuzi ya kuwatimua viongozi wakubwa hasa DVC PFA...
- Kuingia kwenye mgomo usio na kikomo wakati wa mitihani ya mwisho wa semister ili kuwaonyesha wanafunzi na watawala namna ambavyo hawatendewi haki....
- Kuwahasa watanzania kuwa UDOM sio mahala salama na pazuri pa kufanya kazi kwasasa...na hata wale wenye mawazo ya kutafuta kazi UDOM wajue na wawe wamejiandaa kuingia JEHANAMU ya mateso na taabu...
Source:mwanachama wa UDOMASA...