Wagombea mtoto baada ya kupeana talaka

kilimasera

JF-Expert Member
Dec 2, 2009
3,068
268
WALIOKUWA wanandoa kwa muda wa miaka minne mfululizo wamejikuta wakihatarisha maisha ya mtoto wao kwa kumjeruhi kwa kumgombani kama mpira wa kona huku kila mmoja akihitaji kubaki na mtoto huyo baada ya kutalakiana
Sakata hilo la kugombea mtoto lilitokea juzi maeneo ya Tabata Kimanga ambapo watalaka hao walikuwa wakigombani mtoto wa kiume aliyekuwa na umri wa miaka mitatu

Hali hiyo ilizuka tu mwanaume huyo anayefahamika kwa jina la Muhsin [36] kumpa talaka mke wake aliyefahamika kwa jina moja la Feti [28]

Sakata la kugombani mtoto huyo lilizuka wakati mwanamke huyo alipofika nyumbani kwake hapo kuchukua kilichochake akiwa na jopo la wasindikizaji ili aweze kupisha maisha mapya ya mume wake huyo

Hali ilibadilika baada ya mke huyo kuandaa nguo za mtoto huyo ili aweze kuondoka nae anakoenda na ndipo aliamsha mashetani yaliyolala ya mwanaume huyo na kumtaka amuache mtoto huyo hali iliyofanya mwanamke huyo apinge na kutaka kukimbia nae ndipo walipoanza kugombania motto kila mmoja akivuta mkono wake na kumuweka mtoto huyo katika kipindi kigumu ambapo mtoto huyo alikuwa katika hali mbaya ya kuvutwa kati ya wazazi wake hao wawili

Hali hiyo ilifanya majirani waishio karibu na nyumba hiyo kuingilia kati hata hivyo haikusaidia kitu huku kila mmoja akihitaji kuishi na mtoto huyo

Hata hivyo mwanaume huyo hakukubaliana na hali hiyo hali iliyofanya akaripoti kwa Mwenyekiti waSerikali za mtaa anapoishi na kupigia simu baadhi ya wazee wa familia wa pande zote mbili ili aweze kupata msaada juu ya sakata hilo

Imedaiwa mwanaume huyo alikuwa anagoma mtoto huyo asiondoke kwa kuwa mwanamke huyo alishatangaza kuondoka nchini hali iliyofanya mwanaume huyo kugoma mtoto huyo kuondoka na mama yake huyo
Hadi nifahamsihe inaondoka maeneno hayo majira ya saa 10 jioni iloiacha wanandoa hao wakiwa katika hali ya ututa huku kila mmoja akihitaji kuishi karibu na mtoto huyo
 
Back
Top Bottom