Kama tunavyojua ni ukweli usiopingika kuwa CCM itatumia mbinu nyingi kutaka kuiba kura ili ionekane imeshinda. Nakumbuka mwaka 1995 wakati Balozi paul ndobo akigombea jimbo la musoma kupitia NCCR-Mageuzi. CCM walipoona kwamba Paul ndobo ameshinda walienda katika kituo cha kuhesabia kura na kutaka kubadilisha matokeo. Thank God Paul ndobo mwenyewe alikuwepo pale kituoni na baada ya mabishano makubwa paul ndobo aliwaambia CCM atakaye taka kubadilisha matokeo ya kura kinyume na yalivyo nitampiga risasi hapahapa!! na ccm walipoona mzee ndobo hatanii walikubaliana matokeo yawe kama yalivyo na hapo ndobo akatangazwa mshindi. Waungwana ebu naomba mnifahamishe sasa utaratibu huu wa wagombea kuwepo katika vituo ulishafutwa? Pia jambo jingine naomba tutoe ushauri kwa chadema jinsi gani watalinda kura zao!