TheChoji
JF-Expert Member
- Apr 14, 2009
- 4,974
- 15,310
Zamani ilikuwa mtu ukipata wageni mnakaa mnapiga stori, mnapeana habari za miaka tele na kufurahi pamoja. Siku hizi hali ni tofauti. Mkishasalimiana tu kinachofuata ni kukodoa macho kwene tv. We unajaribu kuanzisha topic ili angalau muongee lakini wapi bwana.. wageni macho pima kwn screen. Wengine ndio kwaanza wanashika rimoti na kuanza kuchagua channel wanazopenda wao. Jamani, mmekuja kunisalimia au kuangalia tv? Mi kuanzia sasa nikipata wageni nazima tv!