Babu Ubwete
Senior Member
- Jan 26, 2008
- 169
- 29
KUna wingi wa wageni katika NGO's za hapa Tanzania ukianza na volunteers,wakenya,wazimbabwe,wadosi, waghana,na wapopo. Hivi kweli hakuna reguratory body yoyote inayoangalia hawa wageni maana wengi wao wamekuja kutafuta riziki na wanalipwa dola nyingi kwa kazi ambazo watanzania wanaweza kuzifanya. Umefika wakati Tanzania ibaki kwa watanzania mambo yanayoendelea Ivory coast kiini chake ni wageni wengi kukimbilia nchini mwao. Serikali ijaribu kuangalia upya ni kwanini tuna wageni wengi kwa njia ya NGO's , investment ambao wanakuja kufaidi nchini mwetu kwani hili ni sawa na Time bomb, Tuna Universities nyingi zinazalisha graduates lakini ukiangalia top management ya Foreign banks,insurance & accounting firms, Telecom companies ni wageni hili tuliondoe haraka. Na kwenye Katiba liwepo.