Waganda na Kiswahili

Mwanitu

JF-Expert Member
Feb 19, 2010
1,036
592
Nimejikuta nikijiuliza kwa nini waganda amekuwa wagumu sana kukikubali kiswahili? Ningetegemea wawe mbele zaidi hasa ukizingatia wamekuwemo Kwenye uanzilishi wa jumuia yetu na Vilevile kiswahili sio lugha ambayo Kabila moja linaweza likadai kuwa ni lugha yake peke yake.

Je, ni kwa sababu ya kasumba ya kuamini kuwa lugha ya waliokuwa watawala waingereza ndio bora? Je, ni kwa kuwa wanajiona wao ni Taifa kubwa kwa vile walikuwa na watawala wakubwa toka enzi yaani Kambaka Kingdom kwa hiyo wangependa wote tuzungumze kiganda?

Je, Kenya imekikubali kiswahili kirahisi zaidi kwa sababu kinazungumzwa sana mombasa? Nashangaa nchi kama Kongo na Rwanda kuonekana kukikubali kiswahili zaidi kuliko waganda,inaweza kuwa sababu gani?

Wajuzi tujuzeni.

Karibuni.
 
Uganda kiswahili ni lugha ya kwenye majeshi, I mean
askari wengi wa Uganda wanapenda kiswahili wakiamini ni lugha ya amri...kwa mfano...fungua mlango nyama wewe..kaa chini.....mikono juu...n.k ni amri za kijeshi ambazo ni common saana kwa askari wa kiganda.

Hii imepelekea raia kuona kiswahili ni lugha ya kushurutisha na kukandamiza wanyonge, hivyo wameikacha.
 
Kuna mahali nilisoma wanasema wamekichukia Kiswahili kwa sababu ya Idi Amini na maaskari wake kipindi anatawala Uganda.
Sasa hiyo ni enzi zile ,kizaz cha sasa hakikuwepo enzi za idd Amin.Ni maamuzi ya serikali yao kukomalia kiswahili mbona kagame amebadilisha toka France to English as official language! Utawala Wa idd Amin haina mashiko kwa sasa
 
Wanganda wengi wanaamini kuwa kiswahili ni lugha ya wezi na majambazi.ndo maana wengi wao hawakipendi, na wanaotumia kiswahili uganda wengi wao ni sector ya polisi na wanajeshi wanatumia ata wakiwa kazini ....ile kauli ya " leta pesa" kutoka kwa majambazi hiyo ndio inawachanganya sana.
 
Nimejikuta nikijiuliza kwa nini waganda amekuwa wagumu sana kukikubali kiswahili? Ningetegemea wawe mbele zaidi hasa ukizingatia wamekuwemo Kwenye uanzilishi wa jumuia yetu na Vilevile kiswahili sio lugha ambayo Kabila moja linaweza likadai kuwa ni lugha yake peke yake.

Je, ni kwa sababu ya kasumba ya kuamini kuwa lugha ya waliokuwa watawala waingereza ndio bora? Je, ni kwa kuwa wanajiona wao ni Taifa kubwa kwa vile walikuwa na watawala wakubwa toka enzi yaani Kambaka Kingdom kwa hiyo wangependa wote tuzungumze kiganda?

Je, Kenya imekikubali kiswahili kirahisi zaidi kwa sababu kinazungumzwa sana mombasa? Nashangaa nchi kama Kongo na Rwanda kuonekana kukikubali kiswahili zaidi kuliko waganda,inaweza kuwa sababu gani?

Wajuzi tujuzeni.

Karibuni.
It [Kiswahili] was born in Tanzania, grew up in Mombasa- Kenya, got sick in Uganda and it died in Congo!
 
Wanaokataa Kiswahili ni Wabaganda ambao ndio haohao wanataka lugha yao na serikali yao ya Kichifu ipate mamlaka zaidi! kitu ambacho Waganda wengine hawakitaki!
 
nawakubali waganda, ni kiganda mwanzo mwisho mjini na vijijini. bora wao wana cha kujivunia. niliwahi kuuliza baadhi wakasema wao kiswahili watajifunzia wapi, maana hata kiingereza ni kwa walienda shule. labda walazimishwe kujifunza mashuleni
 
Nikweli uganda kuna kabila nyingi kama kiganda, kinyakole, kisoga nk.sasa shida inakuja kwamba %kubwa ni kabila la kiganda ambao wanathamini sana mira na desturi kuliko kitu chochote. Mpaka wanataka kumlazimisha museveni atumie kiganda as a medium of instructions shuleni sasa hapo jiulize kiswahili kitapokeleewa
 
Kuna mahali nilisoma wanasema wamekichukia Kiswahili kwa sababu ya Idi Amini na maaskari wake kipindi anatawala Uganda.
Ni kweli kipindi cha IDDI amin askari wake walitumia kiswahili kuamrisha na kushurutisha RAIA
 
Kiswahili hakina nafasi Uganda kwa sababu nyingi mlizotaja lkn pia majority of Ugandans preffer to use Kiganda or English because Kiganda as a language as many speakers in Uganda than any other Langunge.
Also the Kingdom hestate to insist its people to learn Kiswahili because of the historical fates associated to Kiswahili Speakers at the Kabakas palace. It is a long story members next time
 
Sasa hiyo ni enzi zile ,kizaz cha sasa hakikuwepo enzi za idd Amin.Ni maamuzi ya serikali yao kukomalia kiswahili mbona kagame amebadilisha toka France to English as official language! Utawala Wa idd Amin haina mashiko kwa sasa
Lakini Bado kifaraca ndo ruga inayotumika maoficini. Serikari kutoa armi haimainiashi kuwa ndo mwisho mwa lugha kutumiwa
 
Wanaokataa Kiswahili ni Wabaganda ambao ndio haohao wanataka lugha yao na serikali yao ya Kichifu ipate mamlaka zaidi! kitu ambacho Waganda wengine hawakitaki!
Na wewe nawe waonekana hujui chochote kuhusu machief( Kabaaka)/ (waganda)

kwanza pata elimu kuhusu utawala wa Kabaaka/chief na matumizi ya lugha kwa nchi ya Uganda
 
Wanganda wengi wanaamini kuwa kiswahili ni lugha ya wezi na majambazi.ndo maana wengi wao hawakipendi, na wanaotumia kiswahili uganda wengi wao ni sector ya polisi na wanajeshi wanatumia ata wakiwa kazini ....ile kauli ya " leta pesa" kutoka kwa majambazi hiyo ndio inawachanganya sana.
Niliongea na waganda wachache, waliniambia pamoja na yote, wanajeshi wa Amin walitumia Kiswahili na kukifanya kuhusishwe na watu wenye elimu ndogo au wasio na elimu. Wanadharau Kiswahili ndiyo maana hawapendi kujifunza. Wanaume wa kiganda wanaamini wanawake wa Kiswahili ni wazuri wa kupika na kitandani lakini hawatakushauri maswala ya maendeleo.
 
Back
Top Bottom